birungi
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 391
- 16
Habari za leo wanajamii wenzangu.
jana katika kipindi cha tutashinda cha mzee wa upako channel 10 nilimsikiliza mwanzo mpaka mwisho.kilikua ni maswali na majibu kuhusu huduma yake na mipango kiujumla maana anatarajiwa kufanya mkutano mkubwa arusha.
katika maswali na majibu,mida ya saa 4:40 usiku aliulizwa swali kwamba analiongeleaje swala la dawa ya babu wa loliondo. kwanza akatolea mfano wa mfalme suleiman kwenye biblia na akasema tusiwe haraka kutoa maamuzi ya kukandia kitu au kusifia kitu,inabidi kukipa mda na kutafakari ndio mtu utamke.akaongeza kuwa kwa upande wake anaibariki dawa ya babu na atazidi kuiombea izidi kuwaponya watu,endapo tu haihusiani na ushirikina.kasema hajasikia masharti kuwa labda kainywe njia panda au rudi kinyumenyume au kupiga ramli,so iendelee kuponya watu.
pia aliongezea kuwa watanzania tusijiweke nyuma kiasi hichi.karibu dawa nyingi hata ulaya zinatengenezwa kwa mzizi. tusijiwekee fikra tu kwamba atakachovumbua mzungu ndio sahihi ila cha ngozi nyeusi ndio uongo.MUNGU ameamua kutukomboa tena kwa kupitia mwafrika. akasisitiza tunachoomba ni uzima wa wananchi maana afya ndio nguvu kazi na hitaji muhimu la wanadamu.sasa kama watu wanakunywa na kupona MUNGU na azidi kuibariki na hata huyo babu abarikiwe azidi kuponya watu alimalizia mchungaji.na pia anazidi kumuombea.atakua na mkutano arusha na amekaribisha watu waende kwa wingi kupata upako na waende loliondo kushushia dawa ya babu waponywe zaidi.maana dawa ya babu inatibu magonjwa matano ila yeye atakupa upako wa kibali kazini,kupata ajira,milango ya fedha,kuponywa mapepo,uwete na magonjwa mbalimbali.
kwa upande wangu niliridhishwa na uchambuzi alioutoa.
jana katika kipindi cha tutashinda cha mzee wa upako channel 10 nilimsikiliza mwanzo mpaka mwisho.kilikua ni maswali na majibu kuhusu huduma yake na mipango kiujumla maana anatarajiwa kufanya mkutano mkubwa arusha.
katika maswali na majibu,mida ya saa 4:40 usiku aliulizwa swali kwamba analiongeleaje swala la dawa ya babu wa loliondo. kwanza akatolea mfano wa mfalme suleiman kwenye biblia na akasema tusiwe haraka kutoa maamuzi ya kukandia kitu au kusifia kitu,inabidi kukipa mda na kutafakari ndio mtu utamke.akaongeza kuwa kwa upande wake anaibariki dawa ya babu na atazidi kuiombea izidi kuwaponya watu,endapo tu haihusiani na ushirikina.kasema hajasikia masharti kuwa labda kainywe njia panda au rudi kinyumenyume au kupiga ramli,so iendelee kuponya watu.
pia aliongezea kuwa watanzania tusijiweke nyuma kiasi hichi.karibu dawa nyingi hata ulaya zinatengenezwa kwa mzizi. tusijiwekee fikra tu kwamba atakachovumbua mzungu ndio sahihi ila cha ngozi nyeusi ndio uongo.MUNGU ameamua kutukomboa tena kwa kupitia mwafrika. akasisitiza tunachoomba ni uzima wa wananchi maana afya ndio nguvu kazi na hitaji muhimu la wanadamu.sasa kama watu wanakunywa na kupona MUNGU na azidi kuibariki na hata huyo babu abarikiwe azidi kuponya watu alimalizia mchungaji.na pia anazidi kumuombea.atakua na mkutano arusha na amekaribisha watu waende kwa wingi kupata upako na waende loliondo kushushia dawa ya babu waponywe zaidi.maana dawa ya babu inatibu magonjwa matano ila yeye atakupa upako wa kibali kazini,kupata ajira,milango ya fedha,kuponywa mapepo,uwete na magonjwa mbalimbali.
kwa upande wangu niliridhishwa na uchambuzi alioutoa.