Regia Mtema
R I P
- Nov 21, 2009
- 2,970
- 864
Leo katika kikao cha Bunge cha jioni wakati wabunge wakichangia hoja ya Uchumi Mheshimiwa Paul Kimiti ameaga rasmi Bunge kwa kujifagilia kwa mafanikio aliyoyapata.Kimiti ameleza kuwa maekuwa Mbunge kwa kipindi cha miaka 30 na wakati anaingia Bungeni alikuwa ana ajenda kuu nne kwa wananchi wake wa jimbo la Sumbawanga Mjini.Amedai kuwa agenda zake zilikuwa ni Elimu,Afya,Barabara na Maji. Amejifagilia kuwa ameweza kutekeleza ajenda zote kwa kiwango cha ufanisi.Amedai alipokuwa akiingia Bungeni Halmashauri yake ilikuwa ina shule nne(4) tu za Sekondari lakini sasa zimefikia ishirini na tano(25) hivyo anajipongeza sana kwa hilo. Hapa mimi ndipo paliponigusa hayp mengine ya Afya,Barabara na Maji sitayaongelea ninaongelea hili la Elimu.
Hoja zangu ni hizi..
1. Kwa kipindi cha miaka 30 kuongeza shule 21 ni kitu cha kujivunia?shule zenyewe ambayo majengo yake yako chini ya kiwango.Give me a break Kimiti,21 tu unajisifia.Je yeye kwa kipindi cha miaka hii 30 ameongeza nyumba ngapi.miradi mingapi,magari mangapi? na kipato chake kimependa kwa kiwango gani?naamini atakuwa amefanikiwa kwa almost 99% ya maratajio yake kiuchumi n.k.Je hayo mafanikio yake binafsi yako proportional na haya ya shule 21?
2. Shule hizi 21 alizoongeza kwa kipindi cha miaka 30 zina walimu wa kutosha?vifaa vya kufundishia na kujifunzia je?zina maktaba?madarasa yanaubora kiasi gani?
3.Tangu kuanzishwa kwa shule hizi ni wanafunzi wangapi wameenda kidato cha tano na sita kwa kiwango cha division one na two?
Mwisho,nimefurahishwa na uamuzi wake wa kujitoa mwenyewe kwenye sistimu bila kusubiri sistimu imteme..Ningefurahi zaidi kama ningemsikia na Hon Malecala naye akiaga Bungeni kwamba hatagombea tena,sorry kwa nitakaowakwaza kwa kusema hili..
Hoja zangu ni hizi..
1. Kwa kipindi cha miaka 30 kuongeza shule 21 ni kitu cha kujivunia?shule zenyewe ambayo majengo yake yako chini ya kiwango.Give me a break Kimiti,21 tu unajisifia.Je yeye kwa kipindi cha miaka hii 30 ameongeza nyumba ngapi.miradi mingapi,magari mangapi? na kipato chake kimependa kwa kiwango gani?naamini atakuwa amefanikiwa kwa almost 99% ya maratajio yake kiuchumi n.k.Je hayo mafanikio yake binafsi yako proportional na haya ya shule 21?
2. Shule hizi 21 alizoongeza kwa kipindi cha miaka 30 zina walimu wa kutosha?vifaa vya kufundishia na kujifunzia je?zina maktaba?madarasa yanaubora kiasi gani?
3.Tangu kuanzishwa kwa shule hizi ni wanafunzi wangapi wameenda kidato cha tano na sita kwa kiwango cha division one na two?
Mwisho,nimefurahishwa na uamuzi wake wa kujitoa mwenyewe kwenye sistimu bila kusubiri sistimu imteme..Ningefurahi zaidi kama ningemsikia na Hon Malecala naye akiaga Bungeni kwamba hatagombea tena,sorry kwa nitakaowakwaza kwa kusema hili..