Mzee Faraj Katalambula Amefariki Dunia

Hammie rajab, elvis musiba, ben mtobwa na sasa faraj katalambula. Nani wa kuziba pengo lao katika uandishi wa riwaya?
 
Magwiji wote sasa wamepukutika.. EDIE GANZEL, HAMIE RAJAB, ELVIS MUSIBA, SS BAWJ, BEN R MTOBWA, sasa FARAJ KATALAMBULA. R.I.P Mzee wa kazi ulale pema peponi AMIN.
 
sisi wa kizazi hiki pendwa wengi hatumjui mtu huyu..wengi tunawajua akina Ben mtobwa..vitabu kama njama na kulipa kisasi,roho ya paka na maraika wa shetani.wausika willy Gamba na joram kiango..jamaa nitamkumbuka.
R.I.P MZEE
 
R.I.P in peace Mzee Katalambula, wana Tabora tumepoteza hazina kubwa0

Mwenyezi MUNGU ailaze roho ya marehemu, Amen
 
Huyu jamaa kumbe ni Prof. sasa? Una maanisha Hassan Katalambula? Nakumbuka kuwasiliana naye miaka ya 90 wakati Tanzanet imeanzishwa na kuanza kukutanisha Watanzania dunia nzima.

Katalambula uandishi wake hadi leo nashindwa kujua kama alisoma sana vitabu vya James Hadley Chase au alikuwa akiangalia sana film za kijasusi za USA. Kwa kweli jamaa aliweza sana kutunga kitabu ambacho kingeliweza sana kutokea kwenye mazingira yetu kwa wakati ule. Tofauti na Musiba ambaye aliingiza sana vikorombwezo ambavyo labda kwa leo ndiyo ungelisema vinawezekana na kuwa jambo la kawaida ila si kwa miaka ile.

Nina imani kuna siku atakuja FILM Director mzuri na kutengeneza film yenye hadhi ya KATALMBULA.

Kama jamaa angeliwezeshwa, nisingelishangaa kuwa angelikuwa kachukuliwa Hollywood au Bollywood kuandika film.

Ndugu yangu Sikonge,

Hassan Katalambula ni Profesa hapo COET-UDSM; ni mtu mwenye roho nzuri sana na ana akili sana kama ndugu yake marehemu Faraji Hussein Hassan Katalambula.

Binafsi nilifurahia sana tunzi za merehemu Katalambula kwa vile alikuwa anatukuza sana nyumbani. Hadithi zake zote lazima zilikuwa zinagusa vitongoji vya Tabora kwa namna moja ama nyingine; kwa mfano hadithi zake nyingi zilitumia sana eneo la mtaa wa Rufita, kulikokuwa na makao makuu ya Tabora Jazz enzi hizo, na vile vile kijiji cha Igalula ambako ndiko asili ya ukoo wake.

Kwenye ubunifu wa hadithi kweli Faraji aliwazidi waandishi karibu waote wa kitanzania ukiachiwa wachache sana waliokuwa katika kariba yake, kwa mfano Shaaban Robert, Yule mzeni aliyendika kitabu cha Kuli, na Profesa Kezilahabi ambaye alikuwa anaandika si kama mbunifu bali kama mwanazuoni wa uandishi. Wengine wote waliobaki ama walikuwa wantafasri vitabu vya akina Nick Carter na James Hadley Chase, au walikuwa wanajitahidi lakini walikuwa hawajafikia kiwango cha Faraji Hussein Hassan Katalambula.
 
RIP mzee Katambula, hakuna kitabu kilichonifutia kama Simu ya kifo, nakumbuka ile heading " Amekufa anacheka"! yule mzee alipowekewa sumu kwenye sigara. Pili pilipili sikumbuki vizuri lakini nadhani pia nilikisoma!
 
Nilizoma riwaya zake za Simu ya Kifo na Pili Pilipili. Nakumbuka majarida yake ya Film Tanzania hasa lililokuwa likizungumzia "Kesi ya Wakenda." Faraj Hussein Hassan Katalambullah alikuwa akipenda kupataja kwao Igalula katika hadithi zake hasa akizungumzia safari za treni kwa kuwa Igalula ni mojawapo ya vituo vya reli ya kati.

Pumzika kwa amani ndugu yetu Katalambullah.
 
I believe Pili Pilipili was and to me is the best Play, yaani ukiisoma ile kitu huwezi weka chini hadi last page, tumepoteza shujaa wengi wa waliobakia ni wale wa kukopi na kupesti hadithi toka kwenye mtandao..... sorry kwa wanaomfahamu vizuri hivi ndie huy huyu alieandika na ile riwaya ya SIRI ya SIFURI???

Siri ya Sifuri imeandikwa na Mohammed Said Abdulla maarufu kama Bwana MSA. Na yeye ni mwandishi mahiri wa vitabu kama Kisima cha Giningi, Mke mmoja waume watatu, Mzimu wa watu wa kale na vyengine nimesahau.
 
Nilizoma riwaya zake za Simu ya Kifo na Pili Pilipili. Nakumbuka majarida yake ya Film Tanzania hasa lililokuwa likizungumzia "Kesi ya Wakenda." Faraj Hussein Hassan Katalambullah alikuwa akipenda kupataja kwao Igalula katika hadithi zake hasa akizungumzia safari za treni kwa kuwa Igalula ni mojawapo ya vituo vya reli ya kati.

Pumzika kwa amani ndugu yetu Katalambullah.

Na kwa miaka ile nilikuwa nikiwaza sana siku moja nitasafiri kwa treni na kupitia vituo hivyo. Vitu kama hivi vya kimaandishi ndivyo vinavyohamasisha utalii wa ndani.

Kwa kweli enzi zile tulikuwa tunalisubiri kwa hamu gazeti la Filam Tanzania na kufuatia hadithi zilizokuwamo. Gazeti moja likisomwa sijui na watu wangapi. Hata sijui utamaduni ule kwa nini generation mpya haikuendeleza.

Pumzika kwa amani Mzee Katalambula
 
  • Thanks
Reactions: 3D.

Similar Discussions

Back
Top Bottom