Mzawadie unaemjali crank box kwa tzs 15,000/= tu!!

futikamba

JF-Expert Member
Jan 18, 2010
243
13
Habari JF?

CRANK BOX NI JENERETA NDOGO YA MKONO YENYE UWEZO WA KUWASHA TAA 3 ZA LED.
HAITUMII BETRI, MAFUTA YA TAA, UMEME WA JUA AU WA TANESCO KUCHAJI.
Crank Box inatumia nguvu zako tu!!
Ina teknolojia rahisi na makini. Unahitaji dakika moja tu kuchaji.
Inatumia DYNAMO kutengeneza nguvu ya umeme inayohifadhiwa kwenye CAPACITOR kwa zaidi ya masaa 2.

Vijijini kwetu tumewaacha ndugu na jamaa ambao bado wanatumia vibatari, kandili, mishumaa na hata wengine kulala giza kwa kukosa mwanga. Wanafunzi wanashindwa kusoma wakitoka shule kwa sababu hawana mwanga tegemezi.

Je, unatumia kiasi gani kila wikiendi kutoka na marafiki zako?
Je, ni kiasi gani cha pesa unatumia bila ulazima/mpango wowote?
Je, unamkumbuka yule ndugu yako mwenye shida hata ya chakula?

CRANK BOX NI MKOMBOZI.


Betri, Mishumaa na Kandili ni hatari kwa afya zetu, zinachafua mazingira & ni gharama kumudu.
Bei za mafuta zimepanda sana, vivyo hivyo bei za chakula na bidhaa nyingine sokoni.
Ukimpatia nduguyo zawadi ya crank box, utakuwa umemuokoa sana.
Ataweza kuhifadhi takriban kiasi cha shilingi TZS: 60,000/= ikiwa ni gharama ya mafuta ya taa kwa mwaka pamoja na gharama nyinginezo nyingi zinazofanana na hizo!!
Ataepuka maradhi yatokanayo na moshi wa kandili na vibatari. Na ataweka mazingira yake safi!!

Muonyeshe unamjali, mnunulie crank box kwa TZS 15,000/= tu na utazidishiwa maradufu!!

Tutembelee:Tupo Mbezi Beach - Tanki bovu karibia na Gates of Paradise Hotel.
Au wasiliana nasi kupitia 0715 997688/ 0785 997688
TANZANIA HOME POWER SYSTEMS - LIGHTING THE NATIONS
 
Heshima kwako Futikamba.

CRANK BOX imetengenezwa wapi au ni wewe mwenyewe umitengeneza inaweza kucharge simu,unaweza kutumia radiao ndogo badala betri.
Vipi matengenezo,spare na nk.Kwa sisi tulio mbali na Dar tunawezaje kuipata,je kuna wakala wenu Arusha.Hii kitu si vijijni nadhani hata mijini inaweza kusaidia hasa TANESCO unaokatika katika kila mara.
 
Heshima kwako pia Ngongo,

Hii crank box imetengenezwa Netherlands & ina uwezo wa kuwasha taa tu. Kwa matengenezo na spare utawasiliana na sisi. Na kama ukihitaji, tafadhali tupigie simu au tuma e-mail kupitia tanhompowersys@gmail.com kuweka order yako. Kwa walioko mikoani tutawatumia hapo free of charge na kwa wale waliopo DSM tafadhali, fika dukani kwetu Mbezi Beach - Samaki karibia na Hotel ya Gates of Paradise. KARIBUNI NYOTE!!
 
Heshima kwako pia Ngongo,

Hii crank box imetengenezwa Netherlands & ina uwezo wa kuwasha taa tu. Kwa matengenezo na spare utawasiliana na sisi. Na kama ukihitaji, tafadhali tupigie simu au tuma e-mail kupitia tanhompowersys@gmail.com kuweka order yako. Tutakutumia hapo ulipo free of charge.

Heshima kwako Futikamba,

Je hakuna namna umnaweza kufanya ikaweza kucharge simu moja kwasababu mahali ninapotaka kuipeleka kuna tatizo hilo sana tafadhali.
 
Asante Ngongo,
Kwa sasa Crank Box ina uwezo wa kuwasha taa tu, tutafanyia ushauri wako kazi na kuleta updates hapa hapa JF.
 
Asante Ngongo,
Kwa sasa Crank Box ina uwezo wa kuwasha taa tu, tutafanyia ushauri wako kazi na kuleta updates hapa hapa JF.

Heshima kwako Futikamba,

Mkuu kama Crank box inaweza kuwasha taa tatu lazima pia itaweza kucharge simu niko tayari kununua hata tatu moja kwaajili ya kuwasha taa na nyingine kwaajili ya kucharge simu tu.Ninataka kupeleka shamba tayari ninatumia solar power mara nyingi Inveter imekuwa ikiaribika.


 
Karibu ngongo.
Tafadhali tuwasiliane kupitia hiyo e-mail niliyokupa hapo kwa maelezo zaidi. Asante kwa ushirikiano wako.
 
Back
Top Bottom