Hivi, wewe serikali yetu ya Tanganyika inakuhusu nini? Kila mada lazima uchomekeze serikali ya tanganyika, serikali ya Tanganyika. Kwani Kikwete ni rais wa wapi? Kwani jeshi la ulinzi wa wananchi wa Tanzania linatoka Zanzibar? Na kama huna uraia wa Tanzania huku unafuata nini? Hakuna mitandao ya Kiarabu ambayo unaweza kujiunga nayo? Eee boo!Nafikiri waTanganyika ni waoga sana. wamekuwa waoga hata kujadili namna ya kuunda Serikali yao ya Tanganyika.
Kumbukeni ukumbi wa Zanzinet ni ukumbi wa wote kama ilivyo Jamii forum. Kila mtu kwa kufuata masharti ya ukumbi una haki ya kujiunga na kutoa michango yao ya mawazo.
Mfano mimi sina uraia kabisa wa Tanzania lakin kumbi zote nipo na nachangia kama kawaida.
Acheni woga kama mnaona yamewauma basi jiungeni huko muweke mambo sawa.
Kumbukeni HAKUNA SIMBA BILA YANGA.