Bronty
Member
- Sep 26, 2011
- 60
- 38
Nimekaa ofisini mara kaja kijana mtanashati kufatilia ishu zake, kanipiga jicho na mie nikarudishia la aibu lakini akaondoka, nafika home kila nikijigeuza namwazia yeye, baada ya siku tatu anakuja ofisini, hajanikuta akaacha kitu kwa mwenzangu narudi lunch napewa kufungua nakuta pipi na chocolate, bila namba, kesho yake kaja tena kaishia reception, kamwachia receptionist ujumbe anisalimie, nikaanza kupoteza mawazo
Baada ya wiki nakutana nae mlimani city kanialika samakisamaki sijajiuliza mara mbili tukala, tukapeana contact kesho yake hakupiga , inayofata nikamrukia,ilikuwa ijumaa kaniita happy hour mahala, yaani namwangalia kwa mahaba nishampenda tayari kabla hata hajasema, ananiangalia naona kanielewa. tukatoka tumeongozana mpaka kwake
Mahaba niliyopewa hapo sipati kukwambia, sikutaka kuweka pozi wala nini coz nilijua namuhitaji sana na kama mbwai na iwe mbwai,wiki nzima ilikuwa ni mahaba tu jamani, nikaona kama naishi angani peke yangu na mpenzi wangu, nikapumua nikajua baada ya muda mreeeefu wa kusubiri hatimaye Mungu kanishushia lulu, baada ya wiki mbili kaniita dinner ananiambia anasafiri kusoma nje ya nchi atakaa huko mwaka na nusu.....nililia sana jamani nikajiona sina bahati sababu kilichonitokea ni Love at the first site, yaani ni muda mfupi but i was sure its him, just him for the rest of my life.....
Baada ya wiki kaondoka,now im happy to tell you anarudi baada ya kumngojea muda wote huo, process zote walifanya wazee wake tunakuja funga ndoa, napenda kuwaambia wasichana wenzangu wajue kusoma mioyo yao coz siku ya kwanza tu nilipomwona mapigo yalicheza
ya moyo na nilijua ndio yeye tu, anarudi mahbuba wangu sijui itakuwaje nitakapompokea Mungu anisaidie iwe perfect.......thats my story...maoni na ushauri unakaribishwa, im excited hapa naandika machozi yananitoka.....
Nawakilisha
Baada ya wiki nakutana nae mlimani city kanialika samakisamaki sijajiuliza mara mbili tukala, tukapeana contact kesho yake hakupiga , inayofata nikamrukia,ilikuwa ijumaa kaniita happy hour mahala, yaani namwangalia kwa mahaba nishampenda tayari kabla hata hajasema, ananiangalia naona kanielewa. tukatoka tumeongozana mpaka kwake
Mahaba niliyopewa hapo sipati kukwambia, sikutaka kuweka pozi wala nini coz nilijua namuhitaji sana na kama mbwai na iwe mbwai,wiki nzima ilikuwa ni mahaba tu jamani, nikaona kama naishi angani peke yangu na mpenzi wangu, nikapumua nikajua baada ya muda mreeeefu wa kusubiri hatimaye Mungu kanishushia lulu, baada ya wiki mbili kaniita dinner ananiambia anasafiri kusoma nje ya nchi atakaa huko mwaka na nusu.....nililia sana jamani nikajiona sina bahati sababu kilichonitokea ni Love at the first site, yaani ni muda mfupi but i was sure its him, just him for the rest of my life.....
Baada ya wiki kaondoka,now im happy to tell you anarudi baada ya kumngojea muda wote huo, process zote walifanya wazee wake tunakuja funga ndoa, napenda kuwaambia wasichana wenzangu wajue kusoma mioyo yao coz siku ya kwanza tu nilipomwona mapigo yalicheza
ya moyo na nilijua ndio yeye tu, anarudi mahbuba wangu sijui itakuwaje nitakapompokea Mungu anisaidie iwe perfect.......thats my story...maoni na ushauri unakaribishwa, im excited hapa naandika machozi yananitoka.....
Nawakilisha