mtendaji wa kijiji
JF-Expert Member
- Jul 3, 2012
- 533
- 114
Kama kweli wabunge wa bunge la Jamhuri ya Muungano ya Tanzania wanajali maslah na wapo kwaajili ya kutetea haki za wananchi wao. Tunaomba jumatatu 30/07/2012. SPIKA Asimamishe shughuli zote Na kujadili swala la mgomo wa waalimu. Aidha hatutarajii kusikia majibu ya kipumbavu kutoka kwa Spika wala Lukuvi wala Werema kudai kuwa Swala hili lipo mahakamani. Kimsingi swala ambalo limesha anza kusikilizwa mahakamani ndo halitakiwi kuzungumziwa. Hili la waalimu bado halijaanza kusikilizwa kwani juzi ijumaa mahakama ilitaka pande zote mbili zikapange hoja zake vizuri ili jumanne zipokelewe mahakamani. Leo ni jumatatu, kesho juma4 hoja za pande mbili ndo zitapelekwa mahakamani. Tunaomba bunge litimize wajibu wa kuisimamia serikali. Hoja hii ikikataliwa tunategemea kuwaona wabunge wa vyama vyote wakitoka Bungeni ili kutoa msimamo wao nje ya Bunge. Mama ana Makinda jiandae kususiwa Bunge kama huna utu na kama huna watoto wanaoathirika na mgomo huu