Mwl Nyerere Alistahili kupewa nobel prizes

Mbogela,
Speak for yourself. Sijawahi kuquestion sababu za kwenda vitani na Uganda na hata hapa JF wanaoquestion au walioquestion wana agenda zao. Kila Mtanzania makini anajua sababu za kupigana na Idi Amin. Na katika vijiji vya ujamaa ni watu kama wewe mnaoamini bila ushahidi kuwa kuna binadamu walioliwa na simba. Naona mnajaribu kuandika historia upya.

Sababu tunazo na uwezo tunao lakini naomba uniambie sababu hizo, kwa ujumla sababu zilitengenezwa.

Turudi kwenye Nobel Prize. Bw. Nobel katika harakati zake aligundua formula mchanganyiko wa chemicals ambazo ukiziunganisha pamoja zilikuwa explosive kwa ajili ya kupasulia miamba kwenye migodi ya madini.

Kutokana na ufumbuzi huu alipata sifa na pesa nyingi sana. Lakini bahati mbaya wakati huo suala la amani lilikuwa tete, serikali zikatumia Formula ya Bw. Nobel kutengeneza mabomu ambayo yalitumika kuua watu na kusababisha madhara makubwa sana duniani ikiwemo uharibifu wa mazingira.

Bw. Nobel alisikitishwa sana kwa hilo, akajilaumu kwanini alidiriki hata kufikiria hiyo formula, alijua itarahisisha maisha sasa imakuwa kinyume imeharakisha maisha.

kwa hiyo kurekebisha hili alianzisha mfuko utakao wahamasisha vijana kubuni vitu vipya vitakavyosaidia kuleta amani na Ndio Nobel Peac Prize.

My Take: Kwa hiyo suala sio kushiriki kwenye kuikomboa africa kama mnavyodai, lakini kubuni njia mpya itakayoiwezesha afrika kukomboka bila vita. Sasa ukiangalia JKN hakuhamasisha kusimamisha vita ila alihamasisha vita kwa kuruhusu nchi za kusini mwa afrika kuweka kambi za mafunzo nchini mwake. Hii ni kinyume na Nobel Peace prize.

Nyerere hakutengeneza mazingira na vijiji vyake vya Ujamaa bali waliharibu mazingira kucreate vijiji na kudisturb equal system.

Akina Ysuph Lule wamewekwa kuzuizini
Akina Tuntemeke Sanga waliwekwa kizuini nchini mwao
Akina Toga (mbunge wa Iringa) waliwekwa kizuizini. Utampaje huyu Peace Prize.

Nimesoma Vitabu vya JKN, Kwame Nkrumah, nimeipenda filosofia yao, walikuwa na malengo mazuri, lakini bado hawaendani na malengo ya Nobel Peace Prize.
 
Sababu tunazo na uwezo tunao lakini naomba uniambie sababu hizo, kwa ujumla sababu zilitengenezwa.

Turudi kwenye Nobel Prize. Bw. Nobel katika harakati zake aligundua formula mchanganyiko wa chemicals ambazo ukiziunganisha pamoja zilikuwa explosive kwa ajili ya kupasulia miamba kwenye migodi ya madini.

Kutokana na ufumbuzi huu alipata sifa na pesa nyingi sana. Lakini bahati mbaya wakati huo suala la amani lilikuwa tete, serikali zikatumia Formula ya Bw. Nobel kutengeneza mabomu ambayo yalitumika kuua watu na kusababisha madhara makubwa sana duniani ikiwemo uharibifu wa mazingira.

Bw. Nobel alisikitishwa sana kwa hilo, akajilaumu kwanini alidiriki hata kufikiria hiyo formula, alijua itarahisisha maisha sasa imakuwa kinyume imeharakisha maisha.

kwa hiyo kurekebisha hili alianzisha mfuko utakao wahamasisha vijana kubuni vitu vipya vitakavyosaidia kuleta amani na Ndio Nobel Peac Prize.

My Take: Kwa hiyo suala sio kushiriki kwenye kuikomboa africa kama mnavyodai, lakini kubuni njia mpya itakayoiwezesha afrika kukomboka bila vita. Sasa ukiangalia JKN hakuhamasisha kusimamisha vita ila alihamasisha vita kwa kuruhusu nchi za kusini mwa afrika kuweka kambi za mafunzo nchini mwake. Hii ni kinyume na Nobel Peace prize.

Nyerere hakutengeneza mazingira na vijiji vyake vya Ujamaa bali waliharibu mazingira kucreate vijiji na kudisturb equal system.

Akina Ysuph Lule wamewekwa kuzuizini
Akina Tuntemeke Sanga waliwekwa kizuini nchini mwao
Akina Toga (mbunge wa Iringa) waliwekwa kizuizini. Utampaje huyu Peace Prize.

Nimesoma Vitabu vya JKN, Kwame Nkrumah, nimeipenda filosofia yao, walikuwa na malengo mazuri, lakini bado hawaendani na malengo ya Nobel Peace Prize.
Who was the war mongerer between Nyerere, Veerwoed, Ian Smith and the the Portuguese colonialists? Ulitaka Nyerere awe Kamuzu Banda? Na yule mbunge wa Iringa hakuwa Toga bali ni Choga. He was not innocent by any measure of the imagination. Kuwaweka wakorofi kizuizini ili kudumisha amani na mshikamano wa Watanzania tangu lini limekuwa kosa? Leo matunda yake tunayaringia sote hata wale wasiokubaliana na sera za Nyerere. Tanzania ni nchi ya utulivu na amani.
 
kwanini pia hakuwa mwenyekiti wa OAU hadi 1985 alipokuwa naelekea kung'gatuka?Tukumbuke yeye nim mmoja wa waasisi wa OAU mwaka 1963.Hata huyu Iddi Amini alikuwa mwenyekiti 1977 nadahani.
 
kwanini pia hakuwa mwenyekiti wa OAU hadi 1985 alipokuwa naelekea kung'atuka?Tukumbuke yeye ni mmoja wa waasisi wa OAU mwaka 1963.Hata huyu Iddi Amini alikuwa mwenyekiti 1977 nadhani.
 
Nomination for the Nobel Prizes - Each year the respective Nobel Committees send individual invitations to thousands of members of academies, university professors, scientists from numerous countries, previous Nobel Laureates, members of parliamentary assemblies and others, asking them to submit candidates for the Nobel Prizes for the coming year. These nominators are chosen in such a way that as many countries and universities as possible are represented over time.
 
Nyerere hakutengeneza mazingira na vijiji vyake vya Ujamaa bali waliharibu mazingira kucreate vijiji na kudisturb equal system.
Alaa lakini Reagan, De Klerk, Perez na Rabin wao hawakuwa na wafungwa na walitengeneza mazingira ya equal system sio?
 
only single minded persons will ignore your statement which is true beyond doubt..............
jamani mwaka 1984 Desond Tutu alipata Nobel Peace prize, me nachoshangaa kuona mtu kama mwalim JK Nyerere hakuwahi kupata tuzo hiyo...sababu moja nayoona ni kwamba Mwalim alikua anapenda socialism, labda ndo maana hawakumpa...nikifika kwenye hayo mawazo napata pia wasiwasi na hizi tuzo.....nikiangalia Obama na JK Nterere na Tutu, hata mandela mwenyewe hawajafanya makubwa kwa waaFrica kama Nyerere....mnaonaje hili jamani? Me naona alistahili kupewa....
 
semenya Binafsi nimeshukuru na kufurahi na changamoto yako, lakini naomba kukuliza wewe mwenyewe ungekuwa kwenye kamati ya kuscreen watu wa kuwapa Nobel Prize ungeweza kumteteaje mwalimu JKN kuwa apewe na anastahili hiyo award/prize? Maana katika bandiko lako unasema kafanya mengi kwa bara la Africa mengi yepi? Nobel Prze zilianzishwa na mtu ambaye alilaani vita JKN alipigana vita na Uganda, vita ambayo hata hapa JF tumequestion mantiki yake. Sababu alizosema tulikuwa nazo za kwenda uganda leo hii wengi wetu hatuzioni?? wangapi walikufa Uganda? kwa kufa kiasi hicho cha watu tayari anakuwa disquliafied kupata NOBEL.

Ukiangalia hotuba zake, tafuta hata You tube zipo utaioona hotuba moja anayosema kuwa aliombwa apatanishwe na Idd Amin lakini kwa maneno yake mwenyewe anasema aliwauliza watu wanaosema kuwa aache kumpiga Idd Amini kuwa walikuwa wapi??? Sasa Mkuu Nobel Prize haaziendi kwa Jicho kwa jicho, zinaenda kwa ukipigwa shavu la kushoto geuza la kulia.

Desmond Tutu siku moja alipokuwa anatembea mtaanzai aliona Mob wanamtandika kijana alienda akamwangukia juu akamfunika watu wakaanza kumpa kibano yeye mpaka alipookolewa na dola. Nelson Mandela alipoteza uraia wake kwa kuchoma Passport, kuna watu wameadnika Historia kubwa sana kama akina Steve Biko, Chris Hann, Bob Moses lakini bado hawajatambuliwa.

JKN alihamisha watu kutoka kwenye vijiji vyao kwa nguvu, watu wengi walipigwa na migambo, walichomewa nyumba zao, walipoteza mifugo, waliliwa na simba, acha waliokufa kwa maralia, Taifodi, vipindupindu kwenye maeneo waliyowekwa yasioyofaa kwa maisha ya Binadamu.

JKN alitaifisha mali za watu kwa azimio lake la arusha (hii ni sawa na anachofanya comrade Mugabe-Jongwe)

Pitia vigezo vya Nobel alafu toa mchanganuo cha alichofanya JKN kuweza kutunukiwa hiyo Prize. Ni Mtazamo Tu

Mbongela, Mtizamo wako mbovu, umefulia kimawazo na kimantiki. Mwezi mzima Watanzania na watu wengine duniani; nasema duniani kwa sababu kuna maadhimisho na Makongamano ya Kumbukumbu ya miaka 10 ya kifo cha Mwalimu yanafanyika Kimataifa nje ya nchi yetu kumu-enzi kwa yale aliyoyafanya. Sasa wewe ndugu yangu unayejaribu kutuletea utumbo huu ni dhahiri kwamba huna ulijualo kuhusu Mwalimu ama una chuki binafsi tu kwa sababu huenda uliguswa wewe ama nduguzo katika hayo uliyoyaeleza.

Tukija kwenye vita vya Uganda ambavyo unadai Mwalimu alipigana bila sababu. You are totally mistaken. Katika hiyo hotuba unayoizungumzia, Mwalimu alisema Umoja wa Mataifa na hata Umoja wa nchi Huru za Afrika hawakufanya lolote hata kukemea tu pale Idd Amin alipotangaza dhamira yake ya kutaka kumega kipande cha Tanzania na alipotishia kuipiga Tanzania hadi Dar es Salaam.

Unataka kutuambia kwamba wewe ulitaka Idd Amin aingie kuteka maeneo ya Tanzania na Mwalimu Nyerere akiwa Rais wa nchi Tanzania akae kimya tu kama mwanamke anayesubiri kupigwa makofi na mume mlevi? Chief Mkwawa alipigana na Wajerumani na Wahehe wengi walikufa katika vita hivyo. Wataka kutuambia kwamba kwa kuwa watu wengi walikufa katika vita na Wajerumani basi vita hivyo vilikuwa havina mantiki na Mkwawa asingestahili kupata tuzo lolote kwa kuwa watu walikufa?

Kwa hiyo, Desmond Tutu ni zaidi ya Mwalimu kwa sababu alimlalia na kumuokoa mtu mmoja tu! Usisahau kwamba Mwalimu alikuwa Rais wa nchi kumtaka aanze kulalia wanaopigwa mitaani ni utupu wa mawazo. Pia usituletee habari ya kugeuza shavu katika masuala ya uongozi na ulindaji wa maslahi ya nchi, haviendani. Pia, Mwalimu kama Rais wa nchi yake Tanzania alikuwa sawa kabisa na ambavyo Obama alivyo leo Rais wa nchi ya Marekani. Tofauti za kuona Rais wa Marekani ni zaidi kwa hiyo anastahili tuzo za aina hiyo na si Rais wa nchi ndogo kama Tanzania zinaletwa na fikra potofu tu. Nakubaliana na wanaosema kwamba tuzo hizo zina agenda za kisiasa ndani yake. Vita vya ukombozi Kusini mwa Afrika, jemadari wake mkuu alikuwa Mwalimu Nyerere. Kama watoaji wa Nobel Peace Prize wangelikuwa hawana ajenda zingine hili tu lingemfanya astahili kupata hiyo tuzo kuliko huyo aliyelalia mtu!

Kuhusu Vijiji vya Ujamaa, ni kweli wapo watu waliohamishwa kwa nguvu n.k. lakini watu wenye akili tunajua kwamba hayo hayakuwa malengo wala maelekezo ya Mwalimu. Mwalimu tunayemfahamu asingaliweza kamwe kuagiza watu wahamishwe kwa nguvu ama wapigwe na kuchomewa nyumba zao. Kama ambavyo leo tunaimba wimbo wa watendaji ama wasaidiai wabovu ambao wanamuangusha Rais Kikwete katika dhamira yake ya maisha bora kwa kila Mtanzania, hivyo ndivyo ilivyokuwa katika utekelezaji wa sera ya Vijiji vya Ujamaa. Nia na madhumuni yalikuwa safi kabisa. Lengo lilikuwa ni kuwaweka wananchi waishi sehemu moja ili Serikali iweze kuwafikishia huduma za jamii kwa urahisi na wao waweze kufanya kazi zao kwa kushirikiana ili wajiletee maendeleo yao haraka. Siku hizi tunazungumzia habari za wananchi kujikwamua kiuchumi kwa kuungana kwenye vikundi k.m. Saccos, Vikoba, Msaragamba, n.k. Hayo yote yalikwishaanzishwa na Mwalimu katika sera yake ya Vijiji vya Ujamaa ni majina tu yanabadilishwa lakini lengo ni lile lile la wanyonge kuungana na kushirikiana katika mambo yao ya kujitafutia maendeleo kwa manufaa yao wenyewe.

Azimio la Arusha linakumbukwa na litaendelea kukumbukwa, kwa nini? Kwa sababu lilikuwa linatetea maslahi na mustakabali wa wanyonge walio wengi dhidi ya wachache waliokuwa wameanza kujipanga kutaka kutumia uwezo na madaraka waliyopewa kujinufaisha wenyewe na kuwasahau waliowapa madaraka yale. Ndani ya Azimio la Arusha kuna mwongozo wa maadili mema na miiko ya uongozi ambayo wanayo hata Marekani na nchi zingine ambazo tunatakiwa tuzisujudu.

Jamani, yeyote anayejaribu kumkandia Mwalimu ama kumpaka matope ni wazi anaonekana mgonjwa wa akili mbele ya jamii ya Kitanzania inayomuheshimu na kum-enzi Mwalimu kwa mengi mema aliyoyatenda ambayo kila Mtanzania amewahi kuguswa nayo kwa namna moja ama nyingine. Mbogela, acha bwana Mwalimu kalala kwa amani Mbinguni na Duniani ana WATETEZI!
 
Mwalimu ana NOBEL PEACE PRIZES nyingi tu toka mioyoni mwa WATANZANIA. Hakutufisadi wala kutuibia; wengi tuliweza kwenda shule kwa sera na mipango alioianzisha na kuisimamia vizuri;Tunaongea lugha moja kwa kuwa alilisimamia vizuri hili; alilinda na kusimamia vizuri maliasili na rasilmali zetu; Enzi zake ajira zilikuwa zinatusubiri kwa kuwa alianzisha TAASISI nyingi za UMMA ambazo tumeziua na kuziuza kwa bei ya kutupa;......
 
[ame="http://www.youtube.com/watch?v=aX0iymjJWvo"]http://www.youtube.com/watch?v=aX0iymjJWvo[/ame]
 
Mbongela, Mtizamo wako mbovu, umefulia kimawazo na kimantiki. Mwezi mzima Watanzania na watu wengine duniani; nasema duniani kwa sababu kuna maadhimisho na Makongamano ya Kumbukumbu ya miaka 10 ya kifo cha Mwalimu yanafanyika Kimataifa nje ya nchi yetu kumu-enzi kwa yale aliyoyafanya. Sasa wewe ndugu yangu unayejaribu kutuletea utumbo huu ni dhahiri kwamba huna ulijualo kuhusu Mwalimu ama una chuki binafsi tu kwa sababu huenda uliguswa wewe ama nduguzo katika hayo uliyoyaeleza.

Tukija kwenye vita vya Uganda ambavyo unadai Mwalimu alipigana bila sababu. You are totally mistaken. Katika hiyo hotuba unayoizungumzia, Mwalimu alisema Umoja wa Mataifa na hata Umoja wa nchi Huru za Afrika hawakufanya lolote hata kukemea tu pale Idd Amin alipotangaza dhamira yake ya kutaka kumega kipande cha Tanzania na alipotishia kuipiga Tanzania hadi Dar es Salaam.

Unataka kutuambia kwamba wewe ulitaka Idd Amin aingie kuteka maeneo ya Tanzania na Mwalimu Nyerere akiwa Rais wa nchi Tanzania akae kimya tu kama mwanamke anayesubiri kupigwa makofi na mume mlevi? Chief Mkwawa alipigana na Wajerumani na Wahehe wengi walikufa katika vita hivyo. Wataka kutuambia kwamba kwa kuwa watu wengi walikufa katika vita na Wajerumani basi vita hivyo vilikuwa havina mantiki na Mkwawa asingestahili kupata tuzo lolote kwa kuwa watu walikufa?

Kwa hiyo, Desmond Tutu ni zaidi ya Mwalimu kwa sababu alimlalia na kumuokoa mtu mmoja tu! Usisahau kwamba Mwalimu alikuwa Rais wa nchi kumtaka aanze kulalia wanaopigwa mitaani ni utupu wa mawazo. Pia usituletee habari ya kugeuza shavu katika masuala ya uongozi na ulindaji wa maslahi ya nchi, haviendani. Pia, Mwalimu kama Rais wa nchi yake Tanzania alikuwa sawa kabisa na ambavyo Obama alivyo leo Rais wa nchi ya Marekani. Tofauti za kuona Rais wa Marekani ni zaidi kwa hiyo anastahili tuzo za aina hiyo na si Rais wa nchi ndogo kama Tanzania zinaletwa na fikra potofu tu. Nakubaliana na wanaosema kwamba tuzo hizo zina agenda za kisiasa ndani yake. Vita vya ukombozi Kusini mwa Afrika, jemadari wake mkuu alikuwa Mwalimu Nyerere. Kama watoaji wa Nobel Peace Prize wangelikuwa hawana ajenda zingine hili tu lingemfanya astahili kupata hiyo tuzo kuliko huyo aliyelalia mtu!

Kuhusu Vijiji vya Ujamaa, ni kweli wapo watu waliohamishwa kwa nguvu n.k. lakini watu wenye akili tunajua kwamba hayo hayakuwa malengo wala maelekezo ya Mwalimu. Mwalimu tunayemfahamu asingaliweza kamwe kuagiza watu wahamishwe kwa nguvu ama wapigwe na kuchomewa nyumba zao. Kama ambavyo leo tunaimba wimbo wa watendaji ama wasaidiai wabovu ambao wanamuangusha Rais Kikwete katika dhamira yake ya maisha bora kwa kila Mtanzania, hivyo ndivyo ilivyokuwa katika utekelezaji wa sera ya Vijiji vya Ujamaa. Nia na madhumuni yalikuwa safi kabisa. Lengo lilikuwa ni kuwaweka wananchi waishi sehemu moja ili Serikali iweze kuwafikishia huduma za jamii kwa urahisi na wao waweze kufanya kazi zao kwa kushirikiana ili wajiletee maendeleo yao haraka. Siku hizi tunazungumzia habari za wananchi kujikwamua kiuchumi kwa kuungana kwenye vikundi k.m. Saccos, Vikoba, Msaragamba, n.k. Hayo yote yalikwishaanzishwa na Mwalimu katika sera yake ya Vijiji vya Ujamaa ni majina tu yanabadilishwa lakini lengo ni lile lile la wanyonge kuungana na kushirikiana katika mambo yao ya kujitafutia maendeleo kwa manufaa yao wenyewe.

Azimio la Arusha linakumbukwa na litaendelea kukumbukwa, kwa nini? Kwa sababu lilikuwa linatetea maslahi na mustakabali wa wanyonge walio wengi dhidi ya wachache waliokuwa wameanza kujipanga kutaka kutumia uwezo na madaraka waliyopewa kujinufaisha wenyewe na kuwasahau waliowapa madaraka yale. Ndani ya Azimio la Arusha kuna mwongozo wa maadili mema na miiko ya uongozi ambayo wanayo hata Marekani na nchi zingine ambazo tunatakiwa tuzisujudu.

Jamani, yeyote anayejaribu kumkandia Mwalimu ama kumpaka matope ni wazi anaonekana mgonjwa wa akili mbele ya jamii ya Kitanzania inayomuheshimu na kum-enzi Mwalimu kwa mengi mema aliyoyatenda ambayo kila Mtanzania amewahi kuguswa nayo kwa namna moja ama nyingine. Mbogela, acha bwana Mwalimu kalala kwa amani Mbinguni na Duniani ana WATETEZI!

Haya Nobel hiyoooo....mpe.
 
jamani mwaka 1984 Desond Tutu alipata Nobel Peace prize, me nachoshangaa kuona mtu kama mwalim JK Nyerere hakuwahi kupata tuzo hiyo...sababu moja nayoona ni kwamba Mwalim alikua anapenda socialism, labda ndo maana hawakumpa...nikifika kwenye hayo mawazo napata pia wasiwasi na hizi tuzo.....nikiangalia Obama na JK Nterere na Tutu, hata mandela mwenyewe hawajafanya makubwa kwa waaFrica kama Nyerere....mnaonaje hili jamani? Me naona alistahili kupewa....
kweli kabisa anastahili hata kama hayupo nasi kimwili kwani mchango wake ni mkubwa sana na hasa ukiangalia vigezo vya nobel
 
ila hii tuzo inautata sana embu soma hapa:

"Obama has been awarded this for his extraordinary efforts to strengthen international diplomacy and cooperation between people"

This is how Norwegian Nobel Prize Committee has described President Barrack Obama's achievements for world peace.

As soon as the announcement of the prize was made, controversy gripped the opinion centers of the world about his selection as a candidate for the award.

It has been only eight months since he has taken the office and the prize is awarded for the past efforts not the future potential of the candidates.

Much of the selection criteria of the candidates are shrouded in mystery. So much, so that the nominations are kept secret for 50 years. Unlike all the other Nobel prizes which are decided in Sweden and also awards ceremony that takes place in Stockholm – Sweden, the Nobel Peace prize is decided and awarded in Norway. Nobel Peace prize committee constitutes of five members, which are chosen by Norwegian Parliament.

The committee's first task regarding the selection of candidates is to send in the letters to distinguished persons globally requesting them to appoint candidates. By February the nominations are collected.

Once the committee has nominees, the short listing begins. The short list is ready for review by August and by October the finalist is announced to lift the prize in December in a ceremony in Oslo.

Unlike Nobel Prizes for other areas, the Nobel Peace prize has much to do with the subjective opinion of the members responsible for deciding and finalizing the candidates.

This year's choice is not only a shock for the world community at large but also the academics in Norway. The debate has picked so much heat that newspapers in Norway are of the opinion that peace prize should also be decided in Sweden like other prizes.
 
Unaweza kusema lolote kuhusu JKN lakini point ni moja tu he was phenomenon, a one time African leader with a clear purpose and vision. Kama jamaa wa Nobel hawajamuona au jina lake halijapelekwa mimi sijui. Alikuwa "mtu" bwana haka kama alipiganisha vita
 
Matatizo ya kuishi kwenye nchi yenye gazeti na Radio moja ya chama inayoimba Nyerere siku nzima basi mnafikiri Nyerere is the best kila kitu,alikuwa dikteta tuu ingawaje alikuwa sio muuaji,kwa akili zenu Nyerere na style yake ya CCM kushika hatamu na kampeni na jina la mgombea peke yake na kunyanganya watu mali zao kwa jina la azimio la Arusha,kuwaweka watu vizuizini bila kesi na nani asiyejua torture chamber ya St Peters eti apewe Nobel Prize na si ndio huyu ali engineer wizi wa kura Zanzibar then mnafikiri dunia haioni..kuweni serious kidogo!
 
Back
Top Bottom