maganjwa
JF-Expert Member
- Sep 11, 2012
- 2,774
- 2,297
Ccm ya magufuli imewekeza zaidi kwenye kujaribu kuvuruga muungano wa ukawa kama ni dirisha la kuingilia ndani wameipata kupitia CUF na sasa LUMUMBA humu ndani wanachekelea.
Makosa makubwa anayofanya magufuli moja kuhamisha nguvu zake kwenye kuvuruga upinzani kitu amabayo mimi sidhani kama atafanikiwa badala yake wenzake wanaandaa namna ya kumpotezea mda ili asitumie nguvu kubwa kufanya mambo ya maendeleo na mwisho ataonekana ameshindwa kufikia malengo yake
pili ameshindwa kuajiri watanzania akisingizia wafanyakazi hewa wakati tunajua hela hana anashindwa kusema
Tatu elimu bure karibu inamshinda maana mambo yamekuwa hovyo mashuleni hela ina yotumwa ni kiduchu huku wakuu wa shule wanasukumiwa majukumu mengi huku hela hawana mpaka wanatia huruma. mitihani ya mock tayari imekosa hadhi yake
Nne kwa kuwa amedandia hoja ya ukawa na hakujiandaa wapi ana pata hela ya elimu bure jasho linamtoka kwa kuwa ufisadi uko pale pale waliofanya huo uozo amesema anawalinda wakatulie. Angalia IPTL ngoma bado kabisa mchwa ndo wamenoa makali nadhani wote tunajua habari ya hukumu ya juzi kuhusu sekeseke la IPTL.
Tano wafanyakazi wa umma ametuona kama watu wasiostahili kidogo chetu kama haki yetu amegoma kutupa nyongeza, kupandisha madaraja kisingizio ni wafanyakazi hewa lazima jpm ajue sisi ndo tunamjenga na kwa kuwa hatujali na ana hasira na sisi matokea yake ni yeye mwenyewe kutofanikiwa katika mambo yake anayopanga kwa kuwa wafanyakazi amewavunja moyo
Hivyo basi badala ya kuongeza ushawishi kwa watu ccm mdomdogo mtaani watu wana shindwa kuwaelewa na serikali yao ya vitisho kwa kuwa badala ya mambo kuboreka yanazidi kuharibika kila siku.
JPM anajaribu kuiokoa CCM na kaburi lakini anazidi kuipeleka shimoni ashukuru watanzania wengi hawajui nchi yao inaendeshwaje asingefanya anayoyafanya kwa wenzake na watanzania
Karibuni kwa mjadala
Makosa makubwa anayofanya magufuli moja kuhamisha nguvu zake kwenye kuvuruga upinzani kitu amabayo mimi sidhani kama atafanikiwa badala yake wenzake wanaandaa namna ya kumpotezea mda ili asitumie nguvu kubwa kufanya mambo ya maendeleo na mwisho ataonekana ameshindwa kufikia malengo yake
pili ameshindwa kuajiri watanzania akisingizia wafanyakazi hewa wakati tunajua hela hana anashindwa kusema
Tatu elimu bure karibu inamshinda maana mambo yamekuwa hovyo mashuleni hela ina yotumwa ni kiduchu huku wakuu wa shule wanasukumiwa majukumu mengi huku hela hawana mpaka wanatia huruma. mitihani ya mock tayari imekosa hadhi yake
Nne kwa kuwa amedandia hoja ya ukawa na hakujiandaa wapi ana pata hela ya elimu bure jasho linamtoka kwa kuwa ufisadi uko pale pale waliofanya huo uozo amesema anawalinda wakatulie. Angalia IPTL ngoma bado kabisa mchwa ndo wamenoa makali nadhani wote tunajua habari ya hukumu ya juzi kuhusu sekeseke la IPTL.
Tano wafanyakazi wa umma ametuona kama watu wasiostahili kidogo chetu kama haki yetu amegoma kutupa nyongeza, kupandisha madaraja kisingizio ni wafanyakazi hewa lazima jpm ajue sisi ndo tunamjenga na kwa kuwa hatujali na ana hasira na sisi matokea yake ni yeye mwenyewe kutofanikiwa katika mambo yake anayopanga kwa kuwa wafanyakazi amewavunja moyo
Hivyo basi badala ya kuongeza ushawishi kwa watu ccm mdomdogo mtaani watu wana shindwa kuwaelewa na serikali yao ya vitisho kwa kuwa badala ya mambo kuboreka yanazidi kuharibika kila siku.
JPM anajaribu kuiokoa CCM na kaburi lakini anazidi kuipeleka shimoni ashukuru watanzania wengi hawajui nchi yao inaendeshwaje asingefanya anayoyafanya kwa wenzake na watanzania
Karibuni kwa mjadala