Mzito Kabwela
JF-Expert Member
- Nov 28, 2009
- 18,857
- 7,615
Muimbaji wa vidole juu toka Kundi la Dar es Salaam Morden Taarab (pichani chini), Hashimu Said, amedaiwa kukimbiwa na mkewe, Zainabu Omary, Amani linashuka nayo.
Kwa mujibu wa chanzo makini cha Amani, mke wa Hashimu alianza kusikia habari za mumewe kuwa klozi na wanaume wenye tabia chafu kitambo ambapo alimkanya mumewe lakini jamaa huyo alimjibu kuwa ni maneno ya wakosaji waliolenga kurudisha nyuma maendeleo yake.
Kihabarishi hicho kilibainisha kuwa, tangu aunyake mchongo huo, waifu huyo wa jamaa amekuwa akihoji uhalali wa taarifa hizo hivyo kuibua malumbano miongoni mwao.
Kikaendelea kusambaza umbeya kuwa, baada ya kufanya utafiti na kutia majibu kibindoni, Zainabu aliamua kufunga virago na kuelekea nyumbani kwa wazazi wake jijini Tanga kwa lengo la kwenda kusaka ufumbuzi wa suala hilo.
Baada ya kuzinyaka nyiuzi hizo, Amani lilimwendea hewani Hashimu kupitia simu yake ya kiganjani ili kujibu mapigo ya ishu hiyo ambapo mbali na kukiri alisema kuwa ana imani mama watoto wake huyo iko siku atarejea.
Ni kweli mke wangu kanikimbia, yuko kwa wazazi wake Tanga, kama alikuwa anafanya utafiti juu yangu, basi majibu aliyoyapata siyajui, nina imani akifanya uchunguzi zaidi atarudi tu nyumbani, alisema Hashimu kwa masikitiko makubwa ya kummisi bebi wake.