Habari zinazotangazwa na Katibu wa CHADEMA mkoani Tabora Athumani Mohamed Athumani kupitia WAPO redio anasema mwili wake umeonekana katika hali ya kutatanisha kwa kuwa unaonekana umekaushwa na una mafuta meusi,na inaonekana alivunjwa shingo na kwenye magoti kuna hali inayoonyesha alipigwa,lakini hadi leo ni siku tisa lakini mwili wake hakuliwa na wanyama au ndege ili hali mwili huo umekutwa vichakani kuliko na wanyama na ndege isitoshe inasemekana hela zake amekutwa nazo japo hakuzitaja ni shilingi ngapi.anasema mwili ni kama umepigwa shoti ya umeme,wana JF hilo limekaaje?