Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,318
- 33,125
Binaadam ameumbwa akiwa mwenye uwezo wa kumudu kufanya mambo mbali mbali kwa kutumia mwili wake. Mwili wa binaadam umegawika katika viungo tofauti: Kuna viungo vya kutoa sauti (Vocal), kuna viungo vya kusikia (Audio) kuna viungo vya kuonea(Visual) na kuna viungo vinavyomuwezesha kujisogeza huku na huku (Mobile). Zaidi ya yote hayo kuna ubongo ambao unadhibiti na kurekebisha mwendo wa viungo vyote (Central Organism) pamoja na kuwa na uwezo wa kupokea habari, kuzihifadhi, kuzichambua, kufikiri na kubuni.
Ubongo wa binaadam ni sehemu ya muhimu ya mwili ambao ndio unamuongoza yeye, sio tu katika kudhibiti nafsi bali katika kutekeleza jambo lolote analotaka kulifanya ama kwa mwili wake au kwa kutumia akili yake.
Viungo vya mwili wa binaadam vina kazi mbili kubwa:
1. Sensory Motor: Kupokea taarifa na kuipeleka kwenye ubongo. Ubongo huichambia taarifa na kuichukulia hatua au kuihifadhi.
2. Psycho Motor: Uwezo wa viungo kufanya kazi mbali mbali baada ya kuamrishwa na ubongo itekeleze kazi hio.
MAISHA YA BINAADAM NA MAZINGIRA YAKE
Maisha ya mwanadam hupita katika daraja 5 muhimu nazo ni :-
a) Misha ya tumboni kwa mama.
b) Maisha ya mikononi kwa mama.
c) Utoto.
d) Utu uzima.
e) Uzee
a) Maisha ya Tumboni kwa Mama
Mtoto hufanyika wakati wa mbegu ya mwanamme inapokutana na mbegu ya mwanammke. Baada ya kufanya tendo la ndoa katika kipindi cha dakika 15 hadi 30 tangu manii ya mwanamme kumuingia mwanammke, mbegu za uzazi za mwanamme hufika katika ua la uzazi la mwanammke lililochanua ambalo kawaida huchanua katika kipindi cha wiki moja na nusu tangu kumaliza hedhi. Katika kipindi hicho mbegu ya uzazi ya mwanamme ikimuingia mwanammke na kufika kwenye ua, mwanamke atashika mimba.
Katika kipindi cha saa 24, mbegu ya uzazi ya mwanamme hupenya ndani ya mbegu ya mwanammke, na kwa muda wa siku 7 mbegu hugeuka na kuwa tonge la damu.
Katika kipindi cha mwezi mmoja tonge la damu hukuwa na kuwa pande zito la damu na huziba mfereji wa kupitia damu ya hedhi.
Kidogo kidogo pande hilo la damu hugeuka na kuwa pande la nyama, katika kipindi cha siku 40 pande la nyama huwa kiumbe chenye uhai wake wala sio sehemu ya umbo la mama. Kiumbe hicho hupata chakula na hewa kutoka kwa mamayake, kidogo kidogo kiumbe hicho hukua na kutoa sehemu nyengine za viungo vya mwili wake. Katika kipindi hicho mtoto huanza kuota mishipa yake ambayo ndio inayomuwezesha kuota sehemu tofauti za viungo vyake na hatimae mishipa ambayo hupitisha chakula katika sehemu za viungo hugeuka na kuwa mifupa. Mpaka kumalizika siku 90, viungo vyote vya mtoto vinakuwa vimeshakamilika kuumbwa.
Katika hatua inayofuata mtoto hukuwa na kuanza kucheza kwa kuhangaika au kujivuta vuta akiwa katika fuko la uzazi. Kwa kufanya hivo mtoto anapata nafasi ya kuchezesha mwili wake na huzidi kukuwa.
Baada ya kupindi cha pili cha siku 90 kumalizika, (Allah S.W) Mwenyeezi Mungu humleta malaika ambae huja na kitabu na kuandika mambo yote amabayo anayoyaahidi kuyatekeleza wakati atakapoletwa ulimwenguni tangu kuzaliwa hadi siku ya kufa. Kila kitu kinaandikwa katika kitabu.
Katika kipindi hiki mtoto hujitayarisha kuja ulimwenguni na inapofika siku 45 tangu alipojiwa na Malaika, (Allah S.W) Mwenyeezi Mungu humleta Malaika kwa mara nyengine tena ambae kwa mara hii humtoa uhai wake kwa siku 15 ili mwili wake uwe tohara kutokana na madhambi ya mama yake. Kwani kwa muda wote alioko tumboni alikuwa akiishi kama ni sehemu ya mamayake na alikuwa akila chakula kinachotokana na mamayake, chakula ambacho kinaweza kuwa kimechumwa kwa njia ya halal au kwa njia ya haram.
Baada kutoharishwa, Mwenyeezi Mungu humleta mtoto duniani akiwa tohara hana madhambi yoyote.
Ubongo wa binaadam ni sehemu ya muhimu ya mwili ambao ndio unamuongoza yeye, sio tu katika kudhibiti nafsi bali katika kutekeleza jambo lolote analotaka kulifanya ama kwa mwili wake au kwa kutumia akili yake.
Viungo vya mwili wa binaadam vina kazi mbili kubwa:
1. Sensory Motor: Kupokea taarifa na kuipeleka kwenye ubongo. Ubongo huichambia taarifa na kuichukulia hatua au kuihifadhi.
2. Psycho Motor: Uwezo wa viungo kufanya kazi mbali mbali baada ya kuamrishwa na ubongo itekeleze kazi hio.
MAISHA YA BINAADAM NA MAZINGIRA YAKE
Maisha ya mwanadam hupita katika daraja 5 muhimu nazo ni :-
a) Misha ya tumboni kwa mama.
b) Maisha ya mikononi kwa mama.
c) Utoto.
d) Utu uzima.
e) Uzee
a) Maisha ya Tumboni kwa Mama
Mtoto hufanyika wakati wa mbegu ya mwanamme inapokutana na mbegu ya mwanammke. Baada ya kufanya tendo la ndoa katika kipindi cha dakika 15 hadi 30 tangu manii ya mwanamme kumuingia mwanammke, mbegu za uzazi za mwanamme hufika katika ua la uzazi la mwanammke lililochanua ambalo kawaida huchanua katika kipindi cha wiki moja na nusu tangu kumaliza hedhi. Katika kipindi hicho mbegu ya uzazi ya mwanamme ikimuingia mwanammke na kufika kwenye ua, mwanamke atashika mimba.
Katika kipindi cha saa 24, mbegu ya uzazi ya mwanamme hupenya ndani ya mbegu ya mwanammke, na kwa muda wa siku 7 mbegu hugeuka na kuwa tonge la damu.
Katika kipindi cha mwezi mmoja tonge la damu hukuwa na kuwa pande zito la damu na huziba mfereji wa kupitia damu ya hedhi.
Kidogo kidogo pande hilo la damu hugeuka na kuwa pande la nyama, katika kipindi cha siku 40 pande la nyama huwa kiumbe chenye uhai wake wala sio sehemu ya umbo la mama. Kiumbe hicho hupata chakula na hewa kutoka kwa mamayake, kidogo kidogo kiumbe hicho hukua na kutoa sehemu nyengine za viungo vya mwili wake. Katika kipindi hicho mtoto huanza kuota mishipa yake ambayo ndio inayomuwezesha kuota sehemu tofauti za viungo vyake na hatimae mishipa ambayo hupitisha chakula katika sehemu za viungo hugeuka na kuwa mifupa. Mpaka kumalizika siku 90, viungo vyote vya mtoto vinakuwa vimeshakamilika kuumbwa.
Katika hatua inayofuata mtoto hukuwa na kuanza kucheza kwa kuhangaika au kujivuta vuta akiwa katika fuko la uzazi. Kwa kufanya hivo mtoto anapata nafasi ya kuchezesha mwili wake na huzidi kukuwa.
Baada ya kupindi cha pili cha siku 90 kumalizika, (Allah S.W) Mwenyeezi Mungu humleta malaika ambae huja na kitabu na kuandika mambo yote amabayo anayoyaahidi kuyatekeleza wakati atakapoletwa ulimwenguni tangu kuzaliwa hadi siku ya kufa. Kila kitu kinaandikwa katika kitabu.
Katika kipindi hiki mtoto hujitayarisha kuja ulimwenguni na inapofika siku 45 tangu alipojiwa na Malaika, (Allah S.W) Mwenyeezi Mungu humleta Malaika kwa mara nyengine tena ambae kwa mara hii humtoa uhai wake kwa siku 15 ili mwili wake uwe tohara kutokana na madhambi ya mama yake. Kwani kwa muda wote alioko tumboni alikuwa akiishi kama ni sehemu ya mamayake na alikuwa akila chakula kinachotokana na mamayake, chakula ambacho kinaweza kuwa kimechumwa kwa njia ya halal au kwa njia ya haram.
Baada kutoharishwa, Mwenyeezi Mungu humleta mtoto duniani akiwa tohara hana madhambi yoyote.