Mwikwabe anashauri waziri Masha achunguzwe kuhusu EPA na Deep Green

Lunyungu

JF-Expert Member
Aug 7, 2006
8,873
1,894
Na Ashauri Waziri Masha achunguzwe EPA

Kada machachari wa CCM aliyehamia Chadema hivi karibuni, Mwita Mwikabe, amevishauri vyombo vya dola kuanza kumchunguza Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha endapo alihusika na wizi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).

Amesema kwa kuwa Masha alikuwa mmoja wa Wakurugenzi kwenye kampuni ya Deep Green iliyochota Sh. bilioni 10 kwenye akaunti ya EPA, lazima ahojiwe na ikibainika alihusika afikishwe mahakamani kuungana na wenzake 20.

Akizungumza na Nipashe jana, Mwikabe alisema Masha ameanza kutoa vitisho vya wanaoandika habari za ufisadi.

``Kabla ya kuanza kutishia watu wanaopiga vita ufisadi, lazima tujue uhusuika wake Deep Green, kampuni iliyoko kwenye kundi la mafisadi...Masha anaanza kujihami ili mambo yake yasianikwe kwa kutishia watu,`` alisema Mwikabe ambaye hivi karibuni alikuwa Katibu wa UVCCM Mkoa wa Tanga.

Aidha, alisema watu wote waliohusika katika wizi wa fedha za umma, wamekuwa maadui wakubwa wa vyombo vya habari kutokana na kufichua uovu wao.

Wakati huo huo, Mwikabe alimshangaa Katibu Mkuu wa CCM Yusuf Makamba kwa kudai kuwa mjadala wa EPA umefungwa.

Alisema Makamba hastahili kutoa kauli kama hiyo kwani chama chake ndicho kinatuhumiwa kwa makosa yaliyotokea na kuisababishia serikali hasara ya mabilioni.

Alisema mtuhumiwa hawezi kuwa hakimu kwenye kesi yake mwenyewe.

``Walengwa kama Kagoda Agriculture Ltd hawajakamatwa halafu unasema mjadala umefungwa? yeye ni nani mpaka afunge mjadala,`` alisema Mwikabe.

Hivi karibuni, Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Reginald Mengi, amemtuhumu Waziri mmoja wa Serikali ya Awamu ya nne kuwa ameagiza abambikiwe kodi bandia ya kiasi kikubwa atakachoshindwa kulipa ili hatimaye afilisiwe.

Alisema Waziri huyo ameahidi kunyamanzisha kabisa kutokana na kupigia kelele ufisadi.

Mengi alisema Waziri huyo amekuwa akijigamba kuwa atanyamanzisha kwa kuhakikisha anafilisiwa kama alivyofilisiwa tajiri mmoja huko Urusi.

Mengi alisema Waziri huyo anadai kuwa vyombo vyake vya habari vimekuwa mstari wa mbele kupiga vita ufisadi, jambo ambalo kwa maoni yake siyo zuri na linawanyanyasa baadhi ya watu.

``Nilitarajia Waziri huyo msomi sana angefahamu jinsi vyombo vya habari vinavyofanyakazi...anayeamua nini kiandikwe na nini kisiandikwe ni mhariri wa gazeti ambaye taaluma yake ni uandishi wa habari na si mmiliki,``.alisema.

Alisema ingawa tayari amemsamehe Waziri huyo lakini anapaswa kujua kuwa asiyekemea maovu katika jamii anakuwa sehemu ya maovu hayo.

Alisema Waziri huyo na wale ambao wamekuwa wakimtumia ujumbe wa vitisho lazima wakumbuke kuwa hata wakifanikiwa kunyamanzisha yeye (Mengi), moto wa kupiga vita ufisadi uliokwishawashwa katika akili za watanzania hauwezi kuzimika kamwe.
SOURCE: Nipashe
 
Mwikwabe wewe sema maana unaijua siri ya CCM ulikuwa ndani kabisa kwenye chungu .Tueleze nasi tutakaa nyuma yako kukulinda ama njoo hapa JF mwaga sie tutasambaza.
 
Ndugu Mwikwabe,
Kwanza nakupa pongezi kwa kujitoa kutoka CCM. Umeonesha ni jinsi gani unaipenda nchi yako kwani CCM iko pale kuimaliza nchi na wala si kuilinda na kuijenga nchi.
Tutakuhitaji sana hapa JF katika kujua undani wa CCM na serikali yake chafu ili tuweze kuibamiza toka kila upande. KARIBU SANA
 
Amesema kwa kuwa Masha alikuwa mmoja wa Wakurugenzi kwenye kampuni ya Deep Green iliyochota Sh. bilioni 10 kwenye akaunti ya EPA, lazima ahojiwe na ikibainika alihusika afikishwe mahakamani kuungana na wenzake 20.

- Inaonekana huyu Mwikabe ni kichwa huyu, maana hachanganyi maneno na kurusha hukumu bila facts.
 
Na Ashauri Waziri Masha achunguzwe EPA

Kada machachari wa CCM aliyehamia Chadema hivi karibuni, Mwita Mwikabe, amevishauri vyombo vya dola kuanza kumchunguza Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha endapo alihusika na wizi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).

Amesema kwa kuwa Masha alikuwa mmoja wa Wakurugenzi kwenye kampuni ya Deep Green iliyochota Sh. bilioni 10 kwenye akaunti ya EPA, lazima ahojiwe na ikibainika alihusika afikishwe mahakamani kuungana na wenzake 20.

Akizungumza na Nipashe jana, Mwikabe alisema Masha ameanza kutoa vitisho vya wanaoandika habari za ufisadi.

``Kabla ya kuanza kutishia watu wanaopiga vita ufisadi, lazima tujue uhusuika wake Deep Green, kampuni iliyoko kwenye kundi la mafisadi...Masha anaanza kujihami ili mambo yake yasianikwe kwa kutishia watu,`` alisema Mwikabe ambaye hivi karibuni alikuwa Katibu wa UVCCM Mkoa wa Tanga.

Aidha, alisema watu wote waliohusika katika wizi wa fedha za umma, wamekuwa maadui wakubwa wa vyombo vya habari kutokana na kufichua uovu wao.

Wakati huo huo, Mwikabe alimshangaa Katibu Mkuu wa CCM Yusuf Makamba kwa kudai kuwa mjadala wa EPA umefungwa.

Alisema Makamba hastahili kutoa kauli kama hiyo kwani chama chake ndicho kinatuhumiwa kwa makosa yaliyotokea na kuisababishia serikali hasara ya mabilioni.

Alisema mtuhumiwa hawezi kuwa hakimu kwenye kesi yake mwenyewe.

``Walengwa kama Kagoda Agriculture Ltd hawajakamatwa halafu unasema mjadala umefungwa? yeye ni nani mpaka afunge mjadala,`` alisema Mwikabe.

Hivi karibuni, Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Reginald Mengi, amemtuhumu Waziri mmoja wa Serikali ya Awamu ya nne kuwa ameagiza abambikiwe kodi bandia ya kiasi kikubwa atakachoshindwa kulipa ili hatimaye afilisiwe.

Alisema Waziri huyo ameahidi kunyamanzisha kabisa kutokana na kupigia kelele ufisadi.

Mengi alisema Waziri huyo amekuwa akijigamba kuwa atanyamanzisha kwa kuhakikisha anafilisiwa kama alivyofilisiwa tajiri mmoja huko Urusi.

Mengi alisema Waziri huyo anadai kuwa vyombo vyake vya habari vimekuwa mstari wa mbele kupiga vita ufisadi, jambo ambalo kwa maoni yake siyo zuri na linawanyanyasa baadhi ya watu.

``Nilitarajia Waziri huyo msomi sana angefahamu jinsi vyombo vya habari vinavyofanyakazi...anayeamua nini kiandikwe na nini kisiandikwe ni mhariri wa gazeti ambaye taaluma yake ni uandishi wa habari na si mmiliki,``.alisema.

Alisema ingawa tayari amemsamehe Waziri huyo lakini anapaswa kujua kuwa asiyekemea maovu katika jamii anakuwa sehemu ya maovu hayo.

Alisema Waziri huyo na wale ambao wamekuwa wakimtumia ujumbe wa vitisho lazima wakumbuke kuwa hata wakifanikiwa kunyamanzisha yeye (Mengi), moto wa kupiga vita ufisadi uliokwishawashwa katika akili za watanzania hauwezi kuzimika kamwe.
SOURCE: Nipashe

Ha, ha, ha, Mwita Mwikwabe.

Siamini kama huyu jamaa anamaanisha kwa kuyasema haya kwa Bosi wake na ndio maana natilia mashaka hata kuhamia kwake CHADEMA naona kama ni mtu aliyetumwa kuja kuiboma CHADEMA.

Ila acha yangu yawe macho tuone.
 
Mwita kasema vyema sana .

Hii ndio huyu aliyekataa kuwa mfagizi ktk ofisi ya Nchimbi ?Walimfanyia fitna kutoa ofisi ya Tanga kuja kuwa secretary wa Nchimbi akagoma akidai yeye graduate hawezi kufanya kazi hiyo.
Wanaomjua naomba wanihakikishe kama ndio huyu maana huyu jamaa kama ndio yeye namjua akiwa sekondary pale Azania na nafikiri alishakuwa rais wa wanafunzi UDSM.
 
Mwita kasema vyema sana .

Hii ndio huyu aliyekataa kuwa mfagizi ktk ofisi ya Nchimbi ?Walimfanyia fitna kutoa ofisi ya Tanga kuja kuwa secretary wa Nchimbi akagoma akidai yeye graduate hawezi kufanya kazi hiyo.
Wanaomjua naomba wanihakikishe kama ndio huyu maana huyu jamaa kama ndio yeye namjua akiwa sekondary pale Azania na nafikiri alishakuwa rais wa wanafunzi UDSM.

Mutu he is the man .The very guy unaye muongelea.Wanao toa wasi wasi kwamba kaenda kwa kutumwa lazima waangalie pia mazungira ya yeye kutoka CCM.Hawezi kutoka wakati muhimu sana kama ule kwa CCM kisa katumwa .Waacheni wenye kujaribu kuikoa Tanzania wajaribu na wengine chongeni kwenye forum kuonyesha uchungu ambao hamnao .Mazingira ya kufanya siasa Tanzania nakuishi hapa ni magumu sana .Usione urahisi wa kuchonga hapa na unalala kwenye majumba ya wazungu huko Ulaya na US .Waacheni watu wenye nia ya dhati .
 
Mutu he is the man .The very guy unaye muongelea.Wanao toa wasi wasi kwamba kaenda kwa kutumwa lazima waangalie pia mazungira ya yeye kutoka CCM.Hawezi kutoka wakati muhimu sana kama ule kwa CCM kisa katumwa .Waacheni wenye kujaribu kuikoa Tanzania wajaribu na wengine chongeni kwenye forum kuonyesha uchungu ambao hamnao .Mazingira ya kufanya siasa Tanzania nakuishi hapa ni magumu sana .Usione urahisi wa kuchonga hapa na unalala kwenye majumba ya wazungu huko Ulaya na US .Waacheni watu wenye nia ya dhati .

Natusubiri tuone.Namfahamu Mwikwabe ila kwakuwa mtu sio jiwe...kuna kubadilika...lets wait and see
 
Natusubiri tuone.Namfahamu Mwikwabe ila kwakuwa mtu sio jiwe...kuna kubadilika...lets wait and see

Baba J una maana kwamba Mwikwabe ni kanjanja na opportunisty na atawaacha Chadema hoi ? Sasa who os to be trusted kwamba ni pure opposition maana kila mmoja lazima utasikia huyu katumwa mara analipwa na CCM nk .
 
Baba J una maana kwamba Mwikwabe ni kanjanja na opportunisty na atawaacha Chadema hoi ? Sasa who os to be trusted kwamba ni pure opposition maana kila mmoja lazima utasikia huyu katumwa mara analipwa na CCM nk .

- Wakuu tusiwe naive na wanasiasa, wote huwa ni ma-opportunists lakini give this kid a credit kwa sababu ni moja ya sababu kubwa ya kushindwa kwa CCM Tarime, sasa kama kweli CCM walimtuma ili aisadie Chadema kuwashinda Tarime, then kuna something hatujui kuhusu CCM.

- Binafsi I respect this kid kwa sababu ya kutoka at the right time na siku zote huongea the right words, na siamini kwamba Chadema walimnunua kama ambavyo huwa tunaambiwa hapa kiongozi wa upinzani anapohamia CCM huwa wamenunuliwa tu na njaa inawasumbua, siamini kuwa that is the case na this kid.

Wanasiasa wote huwa ni ma-oppurtunists.
 
- Wakuu tusiwe naive na wanasiasa, wote huwa ni ma-opportunists lakini give this kid a credit kwa sababu ni moja ya sababu kubwa ya kushindwa kwa CCM Tarime, sasa kama kweli CCM walimtuma ili aisadie Chadema kuwashinda Tarime, then kuna something hatujui kuhusu CCM.

- Binafsi I respect this kid kwa sababu ya kutoka at the right time na siku zote huongea the right words, na siamini kwamba Chadema walimnunua kama ambavyo huwa tunaambiwa hapa kiongozi wa upinzani anapohamia CCM huwa wamenunuliwa tu na njaa inawasumbua, siamini kuwa that is the case na this kid.

Wanasiasa wote huwa ni ma-oppurtunists.

Mara zote ambazo nimekaa na Mwikwabe kuanzia Kampeni kule Tarime , Mikutano Musoma , Kuapishwa Mbunge wao watu wa Tarime pale Dodoma nimetumia muda sana kumsoma ili kujua jambo lakini the boy ni makini tuache utani .Kama ni mapungufu wote tunayo lakini kwa national issues tumpe nafasi akiboronga pia hatutacha kusema .
 
Mara zote ambazo nimekaa na Mwikwabe kuanzia Kampeni kule Tarime , Mikutano Musoma , Kuapishwa Mbunge wao watu wa Tarime pale Dodoma nimetumia muda sana kumsoma ili kujua jambo lakini the boy ni makini tuache utani .Kama ni mapungufu wote tunayo lakini kwa national issues tumpe nafasi akiboronga pia hatutacha kusema .
Baada ya miaka saba una la kuongeza mkuu?
 
Back
Top Bottom