Lunyungu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2006
- 8,873
- 1,894
Na Ashauri Waziri Masha achunguzwe EPA
Kada machachari wa CCM aliyehamia Chadema hivi karibuni, Mwita Mwikabe, amevishauri vyombo vya dola kuanza kumchunguza Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha endapo alihusika na wizi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).
Amesema kwa kuwa Masha alikuwa mmoja wa Wakurugenzi kwenye kampuni ya Deep Green iliyochota Sh. bilioni 10 kwenye akaunti ya EPA, lazima ahojiwe na ikibainika alihusika afikishwe mahakamani kuungana na wenzake 20.
Akizungumza na Nipashe jana, Mwikabe alisema Masha ameanza kutoa vitisho vya wanaoandika habari za ufisadi.
``Kabla ya kuanza kutishia watu wanaopiga vita ufisadi, lazima tujue uhusuika wake Deep Green, kampuni iliyoko kwenye kundi la mafisadi...Masha anaanza kujihami ili mambo yake yasianikwe kwa kutishia watu,`` alisema Mwikabe ambaye hivi karibuni alikuwa Katibu wa UVCCM Mkoa wa Tanga.
Aidha, alisema watu wote waliohusika katika wizi wa fedha za umma, wamekuwa maadui wakubwa wa vyombo vya habari kutokana na kufichua uovu wao.
Wakati huo huo, Mwikabe alimshangaa Katibu Mkuu wa CCM Yusuf Makamba kwa kudai kuwa mjadala wa EPA umefungwa.
Alisema Makamba hastahili kutoa kauli kama hiyo kwani chama chake ndicho kinatuhumiwa kwa makosa yaliyotokea na kuisababishia serikali hasara ya mabilioni.
Alisema mtuhumiwa hawezi kuwa hakimu kwenye kesi yake mwenyewe.
``Walengwa kama Kagoda Agriculture Ltd hawajakamatwa halafu unasema mjadala umefungwa? yeye ni nani mpaka afunge mjadala,`` alisema Mwikabe.
Hivi karibuni, Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Reginald Mengi, amemtuhumu Waziri mmoja wa Serikali ya Awamu ya nne kuwa ameagiza abambikiwe kodi bandia ya kiasi kikubwa atakachoshindwa kulipa ili hatimaye afilisiwe.
Alisema Waziri huyo ameahidi kunyamanzisha kabisa kutokana na kupigia kelele ufisadi.
Mengi alisema Waziri huyo amekuwa akijigamba kuwa atanyamanzisha kwa kuhakikisha anafilisiwa kama alivyofilisiwa tajiri mmoja huko Urusi.
Mengi alisema Waziri huyo anadai kuwa vyombo vyake vya habari vimekuwa mstari wa mbele kupiga vita ufisadi, jambo ambalo kwa maoni yake siyo zuri na linawanyanyasa baadhi ya watu.
``Nilitarajia Waziri huyo msomi sana angefahamu jinsi vyombo vya habari vinavyofanyakazi...anayeamua nini kiandikwe na nini kisiandikwe ni mhariri wa gazeti ambaye taaluma yake ni uandishi wa habari na si mmiliki,``.alisema.
Alisema ingawa tayari amemsamehe Waziri huyo lakini anapaswa kujua kuwa asiyekemea maovu katika jamii anakuwa sehemu ya maovu hayo.
Alisema Waziri huyo na wale ambao wamekuwa wakimtumia ujumbe wa vitisho lazima wakumbuke kuwa hata wakifanikiwa kunyamanzisha yeye (Mengi), moto wa kupiga vita ufisadi uliokwishawashwa katika akili za watanzania hauwezi kuzimika kamwe.
SOURCE: Nipashe
Kada machachari wa CCM aliyehamia Chadema hivi karibuni, Mwita Mwikabe, amevishauri vyombo vya dola kuanza kumchunguza Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha endapo alihusika na wizi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).
Amesema kwa kuwa Masha alikuwa mmoja wa Wakurugenzi kwenye kampuni ya Deep Green iliyochota Sh. bilioni 10 kwenye akaunti ya EPA, lazima ahojiwe na ikibainika alihusika afikishwe mahakamani kuungana na wenzake 20.
Akizungumza na Nipashe jana, Mwikabe alisema Masha ameanza kutoa vitisho vya wanaoandika habari za ufisadi.
``Kabla ya kuanza kutishia watu wanaopiga vita ufisadi, lazima tujue uhusuika wake Deep Green, kampuni iliyoko kwenye kundi la mafisadi...Masha anaanza kujihami ili mambo yake yasianikwe kwa kutishia watu,`` alisema Mwikabe ambaye hivi karibuni alikuwa Katibu wa UVCCM Mkoa wa Tanga.
Aidha, alisema watu wote waliohusika katika wizi wa fedha za umma, wamekuwa maadui wakubwa wa vyombo vya habari kutokana na kufichua uovu wao.
Wakati huo huo, Mwikabe alimshangaa Katibu Mkuu wa CCM Yusuf Makamba kwa kudai kuwa mjadala wa EPA umefungwa.
Alisema Makamba hastahili kutoa kauli kama hiyo kwani chama chake ndicho kinatuhumiwa kwa makosa yaliyotokea na kuisababishia serikali hasara ya mabilioni.
Alisema mtuhumiwa hawezi kuwa hakimu kwenye kesi yake mwenyewe.
``Walengwa kama Kagoda Agriculture Ltd hawajakamatwa halafu unasema mjadala umefungwa? yeye ni nani mpaka afunge mjadala,`` alisema Mwikabe.
Hivi karibuni, Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Reginald Mengi, amemtuhumu Waziri mmoja wa Serikali ya Awamu ya nne kuwa ameagiza abambikiwe kodi bandia ya kiasi kikubwa atakachoshindwa kulipa ili hatimaye afilisiwe.
Alisema Waziri huyo ameahidi kunyamanzisha kabisa kutokana na kupigia kelele ufisadi.
Mengi alisema Waziri huyo amekuwa akijigamba kuwa atanyamanzisha kwa kuhakikisha anafilisiwa kama alivyofilisiwa tajiri mmoja huko Urusi.
Mengi alisema Waziri huyo anadai kuwa vyombo vyake vya habari vimekuwa mstari wa mbele kupiga vita ufisadi, jambo ambalo kwa maoni yake siyo zuri na linawanyanyasa baadhi ya watu.
``Nilitarajia Waziri huyo msomi sana angefahamu jinsi vyombo vya habari vinavyofanyakazi...anayeamua nini kiandikwe na nini kisiandikwe ni mhariri wa gazeti ambaye taaluma yake ni uandishi wa habari na si mmiliki,``.alisema.
Alisema ingawa tayari amemsamehe Waziri huyo lakini anapaswa kujua kuwa asiyekemea maovu katika jamii anakuwa sehemu ya maovu hayo.
Alisema Waziri huyo na wale ambao wamekuwa wakimtumia ujumbe wa vitisho lazima wakumbuke kuwa hata wakifanikiwa kunyamanzisha yeye (Mengi), moto wa kupiga vita ufisadi uliokwishawashwa katika akili za watanzania hauwezi kuzimika kamwe.
SOURCE: Nipashe