Kaka yangu Mwigulu,
Awali ya yote nikupe pole kwa kupoteza Jimbo la Arumeru Mashariki kwa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
Kaka, Utakumbuka tangu mchakato wa Kura za Maoni, kulikuwepo tetesi ndani ya CCM kwamba wewe, Nape na wanachama wengine hamkuwa mnamuunga mkono Sioi.Ulikaririwa (haikuthibitishwa0 katika vikao vya ndani kwamba ulikuwa unampiga zengwe la wazi Sioi na hata ulijichomeka katika mchakato wa kura za maoni(ulikanusha hapa JF).
Kaka, baadaye ndugu Sioi alipata kura zinazomtosha na kumshinda William Sarakikya.Kundi lako kimkakati likaonekana kuwa na nguvu kwani katika halli isiyotarajiwa na wengi, mkapitisha zoezi la kurudia kura baina ya Sarakikya na Sumari ambapo Sumari aliikuka mshindi na kuthibitishwa na vikao vya juu kuwa mgombea wa Ubunge Arumeru Mashariki kwa kupitia CCM.
Kaka, CCM wakafanya kosa kubwa ambalo ndiyo msingi wa post yangu hii:
1.Walikuamini, wakakufanya uwe kampeni Meneja; ikiwa na maana wewe ndo msimamizi mkuu wa kampeni, muongoza mikakati na mtu muhimu sana katika kampeni.Ikumbukwe kwamba, miezi michache nyuma uliongoza kampeni kule Igunga na ukafanikisha ushindi.
2.Kosa la pili ulilolifanya ni kumhusisha Rais mstaafu BWM akatika ufunguzi (na ufungaji) wa kampeni.Ulichokosea ni kutokukubaliana na ukweli kwamba BWM ahana mvuto kwa wananchi wa Tanzania na vile vile, hakukuwa umemuandaa na kukubaliana naye nini cha kufanya.Kosa kubwa hasa ni kufungua kampeni zenu baada ya CHADEMA kufungua za kwao; badala ya kuelezea sera zetu na mnawafanyia nini wananchi(walau miaka michahe baada ya mtangulizi - RIP - kutokufanya chochote), mkafanya mkutano ule kuwa ni sehemu ya mipashao na mijembe.Mkapa akafikia kumsema Vicent Nyerere kwamba si wa ukoo wa Nyerere!Yaliyofuatia baadaye ni historia, lakini yalipoteza credibility ya chama chako.
3.Kaka, kosa jingine ulilolifanya, ukiwa kama mkuu wa kampeni, uliruhusu uhuni na udhalilishaji mkubwa.Kwamba kitendo cha wewe kuwa jukwaani, ukamruhusu Bwana Lusinde kutoa lugha nzito za kejeli na matusi, huku wadada na wamama wakishangilia, haikuwa ya kiungwana.Wewe ndiyo ulimleta Lusinde na wewe ndiyo ulimruhusu kupanda jukwaani.Wewe ndo ulimtuma atoe yale matusi mazito?Kwa nini haukumkataza?Watu wengi wana audio na video ya maneno yale na wala haukusikika kokote ukikemea.
4.Kaka, kosa jingine ulilolifanya ni kuruhusu baadhi ya wabunge na makada waandamizi ambao inasadikiwa wako katika kundi hasimu,kupanda jukwaani na kumwombea kura Sioi kwa mbwembwe nyingi wakati inajulikana ni anti Sioi.Swali la msingi: kulikuwa na mantiki kwa Sendeka na Nnauye kupanda jukwani na kumwombea kura Sioi?
5. Kaka, hili pia linahusishwa na ile hali ya nyie kutokuwa wakweli na waaminifu mbele ya jamii.Kwamba, inazungumzwa kuwa Maji Marefu(Ngonyani), alienda kwenye kambi ya CHADEMA na kutaka kuongea na Mh. Nassari.Lakini haijulikani kulitokea nini, ila kesho yake magazetini(Tanzania Daima na Mwananchi), wakaonekana wakiwa wamekumbatiana huku wakicheka katika hali ya matani kabisa.
Hamad, Ngonyani akasema alitishiwa kuuawa na wafuasi wa CHADEMA kwa maelekezo ya Nassari na zile picha zilitungwa tu na Mwananchi na Tanzania Daima.
Hali hiyo ikazua tafrani na mambo kadha wa kadha.Na wachambuzi na wapembuzi wa mambo ya habari na wana intelijensia, wakabisha kwamba ile ilikuwa ni picha ya kirafiki na Ngonyani anaogopa tu kupuuzwa na Makada wenzao.
Kaka, sababu ni nyingi zinazoniaminisha kwamba ukiwa Mkuu wa kampeni, haukutimiza wajibu wako ipasavyo.Na ndiyo maana nashawishika kusema kwamba kuna dalili za wewe kuwahujumu CCM Arumeru.
Hongera sana Mh. Joshua Nassari(MB).
TULIANZA NA MUNGU, TUMEMALIZIA NA MUNGU!
Awali ya yote nikupe pole kwa kupoteza Jimbo la Arumeru Mashariki kwa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
Kaka, Utakumbuka tangu mchakato wa Kura za Maoni, kulikuwepo tetesi ndani ya CCM kwamba wewe, Nape na wanachama wengine hamkuwa mnamuunga mkono Sioi.Ulikaririwa (haikuthibitishwa0 katika vikao vya ndani kwamba ulikuwa unampiga zengwe la wazi Sioi na hata ulijichomeka katika mchakato wa kura za maoni(ulikanusha hapa JF).
Kaka, baadaye ndugu Sioi alipata kura zinazomtosha na kumshinda William Sarakikya.Kundi lako kimkakati likaonekana kuwa na nguvu kwani katika halli isiyotarajiwa na wengi, mkapitisha zoezi la kurudia kura baina ya Sarakikya na Sumari ambapo Sumari aliikuka mshindi na kuthibitishwa na vikao vya juu kuwa mgombea wa Ubunge Arumeru Mashariki kwa kupitia CCM.
Kaka, CCM wakafanya kosa kubwa ambalo ndiyo msingi wa post yangu hii:
1.Walikuamini, wakakufanya uwe kampeni Meneja; ikiwa na maana wewe ndo msimamizi mkuu wa kampeni, muongoza mikakati na mtu muhimu sana katika kampeni.Ikumbukwe kwamba, miezi michache nyuma uliongoza kampeni kule Igunga na ukafanikisha ushindi.
2.Kosa la pili ulilolifanya ni kumhusisha Rais mstaafu BWM akatika ufunguzi (na ufungaji) wa kampeni.Ulichokosea ni kutokukubaliana na ukweli kwamba BWM ahana mvuto kwa wananchi wa Tanzania na vile vile, hakukuwa umemuandaa na kukubaliana naye nini cha kufanya.Kosa kubwa hasa ni kufungua kampeni zenu baada ya CHADEMA kufungua za kwao; badala ya kuelezea sera zetu na mnawafanyia nini wananchi(walau miaka michahe baada ya mtangulizi - RIP - kutokufanya chochote), mkafanya mkutano ule kuwa ni sehemu ya mipashao na mijembe.Mkapa akafikia kumsema Vicent Nyerere kwamba si wa ukoo wa Nyerere!Yaliyofuatia baadaye ni historia, lakini yalipoteza credibility ya chama chako.
3.Kaka, kosa jingine ulilolifanya, ukiwa kama mkuu wa kampeni, uliruhusu uhuni na udhalilishaji mkubwa.Kwamba kitendo cha wewe kuwa jukwaani, ukamruhusu Bwana Lusinde kutoa lugha nzito za kejeli na matusi, huku wadada na wamama wakishangilia, haikuwa ya kiungwana.Wewe ndiyo ulimleta Lusinde na wewe ndiyo ulimruhusu kupanda jukwaani.Wewe ndo ulimtuma atoe yale matusi mazito?Kwa nini haukumkataza?Watu wengi wana audio na video ya maneno yale na wala haukusikika kokote ukikemea.
4.Kaka, kosa jingine ulilolifanya ni kuruhusu baadhi ya wabunge na makada waandamizi ambao inasadikiwa wako katika kundi hasimu,kupanda jukwaani na kumwombea kura Sioi kwa mbwembwe nyingi wakati inajulikana ni anti Sioi.Swali la msingi: kulikuwa na mantiki kwa Sendeka na Nnauye kupanda jukwani na kumwombea kura Sioi?
5. Kaka, hili pia linahusishwa na ile hali ya nyie kutokuwa wakweli na waaminifu mbele ya jamii.Kwamba, inazungumzwa kuwa Maji Marefu(Ngonyani), alienda kwenye kambi ya CHADEMA na kutaka kuongea na Mh. Nassari.Lakini haijulikani kulitokea nini, ila kesho yake magazetini(Tanzania Daima na Mwananchi), wakaonekana wakiwa wamekumbatiana huku wakicheka katika hali ya matani kabisa.
Hamad, Ngonyani akasema alitishiwa kuuawa na wafuasi wa CHADEMA kwa maelekezo ya Nassari na zile picha zilitungwa tu na Mwananchi na Tanzania Daima.
Hali hiyo ikazua tafrani na mambo kadha wa kadha.Na wachambuzi na wapembuzi wa mambo ya habari na wana intelijensia, wakabisha kwamba ile ilikuwa ni picha ya kirafiki na Ngonyani anaogopa tu kupuuzwa na Makada wenzao.
Kaka, sababu ni nyingi zinazoniaminisha kwamba ukiwa Mkuu wa kampeni, haukutimiza wajibu wako ipasavyo.Na ndiyo maana nashawishika kusema kwamba kuna dalili za wewe kuwahujumu CCM Arumeru.
Hongera sana Mh. Joshua Nassari(MB).
TULIANZA NA MUNGU, TUMEMALIZIA NA MUNGU!