MgungaMiba
JF-Expert Member
- Aug 28, 2011
- 999
- 815
Mratibu wa Kampeni wa CCM, Bw Mwigulu, leo mjini Usa River alipokuwa akimnadi mgombea ubunge wake Bw Sioi Sumari, alizungumzia masuala ya ushoga na masharti tuliyopewa na Waziri Mkuu wa Uingereza Bw Cammeron. Cha kujiuliza ni kuwa masuala hayo yanahusiana vipi na uchaguzi huu? Nini kilimsukuma kuongelea masuala hayo kipindi hiki?