Ndugu zangu wana JF mwenzenu niko kwenye hali mbaya, ni miezi michache imepita nilipata mpenzi ambaye nilijikuta kumpenda baaada ya kuvutana sana , maana yeye alipokuja kwangu nilimueleza jinsi nilivyoumizwa huko nyuma na kwamba kwa kweli siamini kama ananipenda, pamoja na vipingamizi vingi nilivyompa akanihakikishia kabisa kuwa yeye hakika ananipenda kwa pendo la kweli. Basi nikajikuta naingia kwenye mapenzi, hivi juzi akasafiri kuja huko nyumbani maana tuko ugenini tunasoma, tangia afike nyumbani hakuna mawasiliano yoyote nilyopata nimejaribu kuandika email maana sina namba ya simu hajibu. Na sina jinsi nyingine ya kumtafuta maana huko nyumbani simfaham hata rafiki yake. Je ndo nimeachwa?? au mpenzi wangu amepata shida gani sielewi nahisi kuchanganyikiwa tu.