Wadau naomba msaada wenu.
Nipo kikazi huku kusini mwa Tanzania. ni karibia wiki moja sasa, na nitakaa kwa wiki nne.
Mara ya kwanza nilifikia katika gest moja hivi ya kawaida tu. Lakini kuna rafiki yangu ambaye anaishi huku aliniomba sana nikafikie kwake.
Nami bila hiana nikakubali, sasa naishi kwakwe.
Sasa cha ajabu kila nikiamka asubuhi nakuta nimechanjwa mwilini yaani kama nilijikwaruza hivi kwenye michongoma. Mara ya kwanza nikapuuzia.
Jana kabla ya kulala, baada ya sala nikaamua kulala na kitabu cha dini ninayoiamini.
Lakini leo nimeamka asubuhi, hadi usoni sasa nimekuta nina alama za kuchanjwa chanjwa.
Nimemweleza rafiki yangu kasema ni mambo ya kishirikina tu endapo nitayapuuzia basi sitopata madhara yeyote.
Kwa mwenye kuwa familiar na mambo kama haya, nini mwisho wa haya yote yanayonikuta?
Nifanye nini mwenzenu kwani hofu inanizidi sasa.
Wadau naomba msaada wenu.
Nipo kikazi huku kusini mwa Tanzania. ni karibia wiki moja sasa, na nitakaa kwa wiki nne.
Mara ya kwanza nilifikia katika gest moja hivi ya kawaida tu. Lakini kuna rafiki yangu ambaye anaishi huku aliniomba sana nikafikie kwake.
Nami bila hiana nikakubali, sasa naishi kwakwe.
Sasa cha ajabu kila nikiamka asubuhi nakuta nimechanjwa mwilini yaani kama nilijikwaruza hivi kwenye michongoma. Mara ya kwanza nikapuuzia.
Jana kabla ya kulala, baada ya sala nikaamua kulala na kitabu cha dini ninayoiamini.
Lakini leo nimeamka asubuhi, hadi usoni sasa nimekuta nina alama za kuchanjwa chanjwa.
Nimemweleza rafiki yangu kasema ni mambo ya kishirikina tu endapo nitayapuuzia basi sitopata madhara yeyote.
Kwa mwenye kuwa familiar na mambo kama haya, nini mwisho wa haya yote yanayonikuta?
Nifanye nini mwenzenu kwani hofu inanizidi sasa.
UondokeeeeWadau naomba msaada wenu.
Kwa mwenye kuwa familiar na mambo kama haya, nini mwisho wa haya yote yanayonikuta?
Utakufa ukibaki hapo
Nifanye nini mwenzenu kwani hofu inanizidi sasa.
Wapendwa.
Nashukuru kwa mwazo yenu.
Jana jioni baada ya kazi nikarudi nyumbani kwa rafiki yangu nilipofikia. Nikamwambia rafiki yangu pamoja na mkewe (ambaye alikuwa ni mcheshi kwangu kipindi ambacho nipo pale) kuwa kutokana na sababu za kiofisi imenibidi nihame nikafikie kwenye hotel ambayo ofisi imetupangishia pamoja na staffs wengine ambao wamekuja leo kutoka Dar.
Rafiki yangu akawa mnyonge sana akawa ananisihi kama inawezekana niendelee kuwepo pale kwake. Cha kushangaza mkewe kwa sauti ya ukali akamwambia rafiki yangu "Unamlazimisha nini? Mwache aende" Rafki yangu alijiskia aibu lakini kiaina akawa anazuga ili ile sentensi aliyotoa shemeji ionekane kama ni utani tu.
Usiku wakati nipo gest niliyofikia akanitumia sms hii "...sory kwa kauli aliyotoa mama...lakini unahama kwa sababu ya ile issue uliyoniambia?" Nikamkatalia kata kata.
Kimsingi nimelala vizuri sana lakini moyoni najistukia kwani nahisi rafki yangu anaona kama nimewaona wao ni washirikina.
Goma unamaanisha mdudu a.k.a kitimoto?
Kuhusu pombe sinywi nilishaacha zamani sana.
yawezekana si ushirikiana au ni ushirikina coz uchawi hata bible inasema upo,cha msingi ni kuamini kuwa hakuna mchawi anayemshinda mungu,ukiamini hivyo wala huitaji kuhofia na kuwaza sana juu ya hayo.sali sana kwa imani nothing will harm you!
Ndibalema mpendwa,pole kwa yote lkn una Mungu aliye mkuu kuliko vyote mtumaini yeye pekee.Mtiririko aliokupa Msanii ni mzuri sana kuufuata wakati wa prayer,nami nakuomba baada ya no 1(TOBA),basi no 2:iwe shukrani,kumshukuru Mungu kwa yote yaliyofanyika kwako na hata kwa wengine kwa cku hiyo eg ulinzi,baraka,etc.Baada ya hapo endelea na mtiririko mzima according to Msanii.HESABU 23:23 inasema kuwa "Hakika hapana uchawi juu ya Yakobo wala hapana uganga juu ya Israel"sasa while praying hapo kny Yakobo weka jina lako na kny Israel waweza eka kazi yako or family.Vile vile nakupa neno kutoka Psalm 4:8 "Katika amani nitajilaza na kupata usingizi mara maana wewe,Bwana peke yako ndiwe unijaliaye kukaa salama".Ndibalema pole sana ndugu yangu.
Ondoa hofu maana umeiweka hapa hii hoja na ni jukumu letu kusaidiana.
Awali kabisa nakushairi usihame hapo unapoishi. ila fanya yafuatayo.
Unapoingia kulala fanya sala (sikupi maneno ya kukariri ila vigezo vya sala) kwa mtiririko ufuatao.
- tumia dakika mbili mpaka tano ukimwomba msamaha Mungu kwa yale yote uliyoyafanya kinyume na mapenzi yake.
- tumia dakika tano hadi saba au zaidi kuwaombea ndugu zako walale salama, na usisahau viongozi wa nchi walindwe mwombee ulinzi na huyo mwenyeji wako.
- tumia dakika tano hadi kumi kuomba Mungu akupe ulinzi wewe utakapopanda kitandani, kataa ndoto za kishetani, kataa kutumiwa kichawi lakini kikubwa zaidi mweleze Mungu kwamba unapokuwa unakitumia chumba hicho unavunja mikataba yoyote iliyowahi kufanywa ndani ya chumba hicho na nyumba hiyo, Vunja mikataba yote ya kishetani ya kichawi hata ya kihalifu.
- Mweleze Mungu kuwa unapolala atume malaika walinzi wakulinde na walinde boma.
nakwambia ukiomba kwa kuamini hakika ahsubuhi kesho utatuletea new story hapa.
Kuhusu kuchanjwa just do it ktk maombi kuvunja mkataba na chain yoote iliyoungwa ili kukuconect. Kataa kwa Jina la Yesu nawe utakuwa salama, zaidi ya hapo tegemea maumivu.
NB. Utakaposema uhame, huko uendako wanakungoja hakuna pa kujificha mbele ya shetani zaidi ya kumkimbilia Mungu kupitia Yesu kristo
Wadau naomba msaada wenu.
Nipo kikazi huku kusini mwa Tanzania. ni karibia wiki moja sasa, na nitakaa kwa wiki nne.
Mara ya kwanza nilifikia katika gest moja hivi ya kawaida tu. Lakini kuna rafiki yangu ambaye anaishi huku aliniomba sana nikafikie kwake.
Nami bila hiana nikakubali, sasa naishi kwakwe.
Sasa cha ajabu kila nikiamka asubuhi nakuta nimechanjwa mwilini yaani kama nilijikwaruza hivi kwenye michongoma. Mara ya kwanza nikapuuzia.
Jana kabla ya kulala, baada ya sala nikaamua kulala na kitabu cha dini ninayoiamini.
Lakini leo nimeamka asubuhi, hadi usoni sasa nimekuta nina alama za kuchanjwa chanjwa.
Nimemweleza rafiki yangu kasema ni mambo ya kishirikina tu endapo nitayapuuzia basi sitopata madhara yeyote.
Kwa mwenye kuwa familiar na mambo kama haya, nini mwisho wa haya yote yanayonikuta?
Nifanye nini mwenzenu kwani hofu inanizidi sasa.