Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Jaji Lewis Makame amestaafu, tumkumbukuke kwa lipi?

Apumzike kwa amani! Lakini mimi naona ni mmoja kati ya watu ambao ametufanya Watz wengi tuache UOGA na kuhakikisha NGUVU YA UMMA inalazimisha yale tuliyoona yanakaribia kupindishwa hayapindishwi. PEEOOOPLES POWEEEER
 
What the sad news! The man executed his duties with great integrity much as Magwanda found him baneful because he walked on the truth and honesty. Folks will revere his devotion towards maintaining and promoting democracy amid pressure from disgruntled opposition liners notably Magwanda.
Great integrity my foot! Ngoja niachie hapo kwa sasa.
 
Wanadamu wengi wanaokuwa kwenye kazi na kuondoka au wanapofariki huwa wanakumbukwa kwa yale mema waliofanya walipokuwa kwenye ile ofisi au duniani. Kwa mtazamo huo yupo mtu aliyekuwa mhimu kwa mustakabali wa Tanzania huyu si mwingine ni Jaji mstaafu aliyekuwakuwaMwenyekiti wa tume ya uchaguzi Lewis Makame ambaye kwa mujibu wa vyombo vya habari amefikia mwisho wa utumishi wake. Sasa tujiulize Watanzania tunaweza kumkumbuka kwa yapii mema au ni alama gani ameiacha ambayo kwayo atakumbukwa kwayo?

mi nitamkumbuka kwa kuiba kura za chadema mwaka 2010
 
Ni mjinga mmoja aliyekuwa anachumia tumbo badala ya kusimamia taaluma yake.acha aje huku uraiani atatia akili.
 
kazi anayo huyu mh jaji...!

i will never miss you hon jaji....
 
Nitamkumbuka kwa kufacilitate wizi wa kura na kuwa mtumwa wa CCM, na mpaka leo hajawahi kurudisha kadi ya CCM.Napendekeza na Rajab Kiravu afuate nyayo za makame maana naye ni uchafu mwingine.
Naunga mkono hoja hata Kiravu nae ha2fai Tuendelee kudai katiba mpya ili itupe tume huru.
 
lewis makameee ooooooukey linnox lewis , ntalikumbuka jina km la mbaba wa mbondia wa u.s.a.
 
Is a gud guy.AMEWEZA KUWAVUMILIA NA KUWABEBA CDM HATA WAKAPATA MAJIMBO MENGI INGAWA WALIKUWA WANATUKANA KAMA INAVYOJIDHIHIRISHA HAPA.
 
Hatuna kumbukumbu za kutosha kuhusu utumishi wake Kama jaji; lakini kama mwenyekiti wa tume ya uchaguzi tutamkumbuka kwa WIZI na UCHAKACHUAJI wa kura pamoja na kuchangia kuviza demokrasia yetu changa.
 
Huyu mzee amedhalilisha fani ya sheria, ni aibu kwa fani nzima. Lakini kitu ambacho wengi humu jf hawakijui, ni kwamba mchakachuaji mkubwa ni mkurugenzi wa Tume Rajabu Kiravu.
 
atakumbukwa kwa kupindisha demokrasia na kuwanyima watz wengi haki yao kuchagua!watz hawakupewa viongozi wale walio wachagua
 
Kama ni kukumbukwa tu sawa- Kwa kuwanyima watanzania haki! kama kwa jema silioni.

Inasikitisha mzee kama yeye kukubali kufanywa kibaraka katika mwisho wake wa utumishi hata kama kuliwahi kuwapo jema katika utumishi wake linafutwa na UCHAKACHUAJI aliousimamia 2010
 
huyu jaji huwenda alichakachua vyetu..sidhani kama ni jaji kweli. Atakumbukwa kwa kusaliti demokrasia na kuwatia watanzania katika hatia ya kuongozwa kinyume na matakwa yao...hafai
 
Bora, maana mizee kama hii ndiyo imetuharibia nchi kwa woga wa kupoteza nafasi zao. Atakumbukwa kwa uchakachuaji 2010 na Watanzania hawatamsamehe maisha yake yote.
 
Back
Top Bottom