ZeMarcopolo
Platinum Member
- May 11, 2008
- 14,017
- 7,220
Nimefurahi kuona umekosa jambo la maana zaidi ya kujaribu kupinga mikakati ya kimaendeleo na maana kwa watanzania wote. Ni kweli Serengeti freight tuliandaa harambee ya kusaidia waliopatwa na mafuriko Dar tukisaidiana na Jestina George. hii ilikuwa ni kutokana na uzalendo tulionao na upendo wetu kwa watanzania wenzetu. Ukumbuke kuwa watu wote waliokuwepo pale waliona nini kilichochangwa na picha zilipigwa(HAKUNA MTU ALIYECHANGISHWA HELA SHAHIDI ALIKUWA NAIBU BALOZI KWANI ALIKUWEPO MUDA WOTE WA HARAMBEE). Mzigo tuliusafirisha bure bila kumtoza mtu nauli. Kutokana na kuwa mchango uliotolewa ulikuwa mdogo sana kama uonavyo kwenye picha. ilibidi tuusafirishe kwenye kontena la kampuni yangu binafsi na ulipofika Dar es salaam tumeulipia ushuru bila kuomba msamaha wa kodi. Sawa mzigo umechelewa na sababu za kuchelewa ni kama ifuatavyo
MICHANGO ILIYOTOLEWA ILIKUWA NI MIDOGO SANA HAIKUWEZA KUFIKA HATA ROBO YA KONTENA DOGO
WATU WACHACHE SANA WALIJITOKEZA KUTOA MCHANGO
KONTENA LILOPAKIWA MZIGO LIMECHELEWESHWA NA CUSTOMS SASA NI MWEZI WA TATU TOKA LIFIKE TUMEISHALIPIA KILA KITU LAKINI BADO TUNASUMBULIWA NA UTARATIBU MBOVU WA BANDARINI AMBAO KILA MTU ANAUFAHAMU.
Mimi nimechangisha kwa moyo wangu.
Nimesafirisha bure
Nimelipia ushuru kwa pesa yangu
Wewe unayepiga kelele humu jee ulichangia nini ? na kwenye ile picha ulikuwepo. uzuri ni kuwa ninawafahamu wote waliotoa kwa sababu sio wengi anyway.
Tumeishpata release ya kontena na inshalah, wakati wowote mtapata picha za mzigo akikabidhiwa mkuu wa mkoa.
DONATED BY TANZANIANS IN UK FOR THE FLOOD VICTIMS
Kwa wale wanaojua ku track nenda SAFMARINE website Container number ni PONU0312771
Nita attach bill of lading later ili uone vizuri
Hii thread imemtoa nyoka ¨pangoni. hahahahahahahaha
naona mkuu umeiweka ile ID yako pembeni na kujisajiri kwa jina lako leoleo kujibu hoja. Safi sana...