Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Aldo Kaduma, amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu mkazi Mkoa wa Iringa, akituhumiwa kujifanya Afisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru). Kada huyo anadaiwa kuomba rushwa ya Sh. 400,000 kutoka kwa Padri wa Kanisa Katoliki Parokia ya Ihemi, Iringa Vijijini.
Kaduma, Mwenyekiti wa CCM Mtaa wa Kiodombi, Iringa Vijijini, anadaiwa kupokea rushwa ya Sh. 150,000 kati ya Sh. 400,000 alizoomba kupatiwa, akijifanya Ofisa wa Takukuru ili asifichue na kushughulikia taarifa za kuwepo kwa tukio la mwanafunzi wa kike wa darasa la tano katika Shule ya Msingi Ihemi kutoroshwa na kuwekwa kinyumba na mfanyakazi wa padri huyo. Inadaiwa kuwa mtuhumiwa huyo alimtishia Padri Pio Callegarri, raia wa Italia kwamba iwapo asingempa dau hilo, angehakikisha anafukuzwa nchini ndani ya saa 24.
Mwendesha Mashitaka wa Takukuru Mkoa wa Iringa, Imani Nitume, akisaidiana na Restituta Kessy, walidai kuwa mtuhumiwa huyo aliwatishia pia walimu wawili wa Shule ya Msingi Ihemi, baba mzazi wa mwanafunzi na kijana anayedaiwa kumuweka kinyumba mwanafunzi huyo wa miaka (17) kwamba wangefungwa miaka 30 kila mmoja iwapo asingepewa fedha hiyo. Ilidaiwa kwamba waliotishiwa kufungwa miaka 30 kwa kumuoza mwanafunzi huyo kinyume cha sheria kama wasingempa rushwa hiyo ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ihemi, Chungueni Kiyao (32) na Mwalimu Mkuu Msaidizi, Edga Mkwama (30). Wengine ni baba mzazi wa mwanafunzi huyo Vallence Mnyenyelwa (44), Msaidizi wa Padri, Anthony Maginga (37) na Tony Kapinga (35) kijana anayedaiwa ndiye aliyemuweka kinyumba mwanafunzi huyo kama mkewe.
CHANZO: NIPASHE
Kaduma, Mwenyekiti wa CCM Mtaa wa Kiodombi, Iringa Vijijini, anadaiwa kupokea rushwa ya Sh. 150,000 kati ya Sh. 400,000 alizoomba kupatiwa, akijifanya Ofisa wa Takukuru ili asifichue na kushughulikia taarifa za kuwepo kwa tukio la mwanafunzi wa kike wa darasa la tano katika Shule ya Msingi Ihemi kutoroshwa na kuwekwa kinyumba na mfanyakazi wa padri huyo. Inadaiwa kuwa mtuhumiwa huyo alimtishia Padri Pio Callegarri, raia wa Italia kwamba iwapo asingempa dau hilo, angehakikisha anafukuzwa nchini ndani ya saa 24.
Mwendesha Mashitaka wa Takukuru Mkoa wa Iringa, Imani Nitume, akisaidiana na Restituta Kessy, walidai kuwa mtuhumiwa huyo aliwatishia pia walimu wawili wa Shule ya Msingi Ihemi, baba mzazi wa mwanafunzi na kijana anayedaiwa kumuweka kinyumba mwanafunzi huyo wa miaka (17) kwamba wangefungwa miaka 30 kila mmoja iwapo asingepewa fedha hiyo. Ilidaiwa kwamba waliotishiwa kufungwa miaka 30 kwa kumuoza mwanafunzi huyo kinyume cha sheria kama wasingempa rushwa hiyo ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ihemi, Chungueni Kiyao (32) na Mwalimu Mkuu Msaidizi, Edga Mkwama (30). Wengine ni baba mzazi wa mwanafunzi huyo Vallence Mnyenyelwa (44), Msaidizi wa Padri, Anthony Maginga (37) na Tony Kapinga (35) kijana anayedaiwa ndiye aliyemuweka kinyumba mwanafunzi huyo kama mkewe.
CHANZO: NIPASHE