Mwenye ubavu anishtaki! - Yona

Yona si ndio zake anadhani kuchimba mkwara ndio watu watamuonea aibu mbona mwenzake alidai ni vijisenti tu na watu wakaruka nae mpaka ameachia ngazi.. na yeye lazima aning'inizwe tu na huyo BWM wake!!! Hapendwi mtu kaka
 
Time will tell hawa jamaaa wamenunua mgodi kwa bei chee tena wanalipwa capacity charge wanatakiwa wanyang'anywe mali ya watanzania halafu waende jela

.........Bandugu,
hii kitu CAPACITY CHARGE!!!..........ina maana gani hasa na ni ya nini
 
Habari zinazoingia mida hii zinasema kuwa aliyekuwa waziri wa Nishati na Madini na mbia mkubwa wa Mgodi wa Kiwira Bw. Daniel Yona amejitokeza na hatimaye kuzungumzia madai kuwa yeye pamoja na Rais wake walijigawia mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira kwa njia za kinyemela.

Imeripotiwa katika mojawapo ya magazeti kuwa Bw. Yona anadai kuwa haki iko upande wake na hajatisikika.

Bw. Yona anasema kuwa aliposikia kuwa kuna mbunge toka Kilimanjaro ameleta hoja ya Kiwira alidhania ni Bw. Ndesamburo wa Chadema. Lakini alipogundua kuwa ni Kimaro wa Vunjo (CCM) Bw. Yona alibakia kusema "Haya bwana".

Hiyo "Haya Bwana" ndiyo kutikisika kwenyewe.
Kwa ushauri wangu nampa Bw Daniel Yona kwamba asijigambe kabisa kwani alichokifanya ni dhuluma kwa wananchi wala si kwa Mbunge wa Vunjo.
 
hivi sheria za nchi zinaruhusu bunge kufungua mashtaka?


Bunge kama taasisi haliwezi kumfungulia mashtaka, lakini uweza kuagiza serikali kuwashtaki wale wote walioonekana na Bunge wanamakosa!

Na hapo serikali ina mamlaka yake, yakukubali moja kwa moja (kuwashtaki) ama kuwashtaki kwa mtindo wa "Richmond"!
 
Yona pole sana kakyangu,ila ujue umefuta historia njema ya wanao, siku zote kizazi chako kitadharaulika na hata kutengwa, fanya maarifa uturudishie hayo mapesa yetu, siku zote watanzania ni wapole ila siku wakicharuka, sijui itakuaje.

Hapa hakuna kitu, mpaka watoto alishawafundisha ufisadi siku nyingi.

Sijui kama yule mtoto wake aliyemchotea bilioni moja toka import support fund za wajapan ameshaziridisha. Kipindi hicho yona alikuwa minister for finance akampa tender mtoto wake kuwa sole supplier of computer appliances ktk ofisi za serikali.

Wajapan waligundua zile hela zimetapanywa hovyo ndipo wakashinikiza aondolewe hazina.

Kuna kipindi huyo mtoto wa yona na wa generali mboma waligombana bar, lakini ukweli ni kwamba kisa cha ugomvi walikuwa wanataka kujua nani zaidi.

Na chenkapa ndiyo alikuwa mwamuzi wa huo ugomvi wa watoto..vyombo vya usalama (police) vilikuwa havina ubavu hapo.

Ile hali ilisikitisha kwa kweli. Ndiyo anayoendeleza huyu fisadi na ameshindwa kabisa kusoma alama za nyakati.
 
.........Bandugu,
hii kitu CAPACITY CHARGE!!!..........ina maana gani hasa na ni ya nini

Capacity charge -- An element in a two-part pricing method used in capacity transactions (energy charge is the other element). The capacity charge, sometimes called Demand Charge, is assessed on the amount of capacity being purchased.

Kwa ninavyoelewa ni kama vile service fee. Kwa hiyo kama unanunua umeme, pia unalipa gharama ya kukuuzia huo umeme. Mwenye kujua zaidi anaweza iweka sawa.
 
Ndiyo! Kama DPP wameshindwa kuwashitaki Yona na Mkapa basi wakereketwa wote ikiwa ni pamjoa na umma nzima ya Watumia Umeme wote wa Tanzania wajadili kutumia class-action suit kuwashitaki Yona pamoja na swahiba wake Mkapa.

Itakuwa ni naive and stupid kusubiri DPP (Director of Public Prosecutions) wawachunguze achilia mbali kuwafungulia mashitaka kwa vile Nicholas Mkapa hivi tayari sasa ni afisa wa DPP.
 
Capacity charge -- An element in a two-part pricing method used in capacity transactions (energy charge is the other element). The capacity charge, sometimes called Demand Charge, is assessed on the amount of capacity being purchased.

Kwa ninavyoelewa ni kama vile service fee. Kwa hiyo kama unanunua umeme, pia unalipa gharama ya kukuuzia huo umeme. Mwenye kujua zaidi anaweza iweka sawa.

Je naweza kusema ni "Overheads" pia?
 
Kwa ninavyoelewa ni kama vile service fee. Kwa hiyo kama unanunua umeme, pia unalipa gharama ya kukuuzia huo umeme. Mwenye kujua zaidi anaweza iweka sawa.


Kila siku hii kampuni inatakiwa iwe inatengeneza umeme, bila kujali kama Tanesco itanunua au la .. so hizo gharama (mashine, mafuta, wafanyakazi) za kuzalisha huo umeme lazima siangaliwe ..

Usisahau hii kampuni haitakiwi kuishiwa umeme (out of stock), yaani haitakiwi Tanesco kuhitaji umeme (wa kununua) halafu hii kampuni ikawaeleza leo hatukuzalisha ...

Na kama unavyofahamu miundombinu ya Tanesco, kila mara uhitaji umeme kwa style ya "emergency" (utasikia line kubwa kutoka Mtera imekatika tunaomba mtuuzie umeme, ohh ...) kwa style hii lazima kampuni iwashe mashine zake saa zote, na wafanyakazi wake wawepo kazini 24hrs!!

hiyo ndio "capacity charges!!"
- Richmond/ Dowans wanamegewa 152Milioni/day
- Kiwira watamegewa 146Milioni/ day

Na hii ulipwa nje ya gharama za manunuzi ya huo umeme uliohitaji!
 
Shkrani sana think BIG,

na hivi wanauzaje huo umeme/energy yao.......i.e whats their rate as to compare na ya kwetu TANESCO.....any idea?
 
Mzuzu,
..... angalia quatation hii:
``Kama yupo mwenye ubavu na nia ya kwenda mahakamani sawa ni haki yake, sitishiki kwa vile pia nina haki zangu. Tutakutana huko,`` alisema.
HIKI NI KIBURI CHA KUTISHA

"Hivi ni Vijisenti tu" , "Mwenye Ubavu anishtaki" Unajua hawa jamaa wanasahau kuwa Hizi Kebehi zao si Nzito tu kwenye masikio ya sisi Walala hoi,bali hata kwa SYSTEM iliyekuwa mwajiri wao.
**Sasa Daniel umeanzisha 'Vita' hii rasmi,na kabla hujampata huyo mbavu mwenziyo wa kusimama naye kwenye vyombo vya sheria nakushauri uendelee kushuhudia jinsi WANAZUONI WA JF watavyo kuchambua kama karanga humu,na si-kwa majungu/mabomu! bali kwa hoja/Facts,si unamwona mwenziyo Bilionea wa Vijisenti......
 
Jamani mbona MKAPA haongei kitu??? waandishi wa habari mnamsuburi huyu jamaa mpaka awaite???? nendeni wenywe mkamuombe mahojiano nae, msumbueni mpaka atamke neno jama, na naahidi siku atakayo fungua mdomo ataongea madudu kama haya "ooo ni magazeti ya udaku tuu, am going to grant their wish am resigning".... "ni vijisenti tu na sitajiuzulu"

Kwa kuwa Mbia mwenzake kaongea tena kwa ubabe wa yeye mweneyewe Mkapa, muda si muda naye ataongea maana maji yanakaribia shingoni. kuna fununu kuwa Mkapa anajiandaa kuongea, tusubiri.
 
Hivi huyu Yona amekubali kuwa anamiliki Tanpower resourses wakati anaongea haya? Je ameshaanza kuzalisha umeme tayari? Kama bado anasubiri nini?
 
Habari zinazoingia mida hii zinasema kuwa aliyekuwa waziri wa Nishati na Madini na mbia mkubwa wa Mgodi wa Kiwira Bw. Daniel Yona amejitokeza na hatimaye kuzungumzia madai kuwa yeye pamoja na Rais wake walijigawia mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira kwa njia za kinyemela.

Imeripotiwa katika mojawapo ya magazeti kuwa Bw. Yona anadai kuwa haki iko upande wake na hajatisikika.

Bw. Yona anasema kuwa aliposikia kuwa kuna mbunge toka Kilimanjaro ameleta hoja ya Kiwira alidhania ni Bw. Ndesamburo wa Chadema. Lakini alipogundua kuwa ni Kimaro wa Vunjo (CCM) Bw. Yona alibakia kusema "Haya bwana".

Ukisikia mtu anaonyesha kidole cha kati kwa watanzania ndio hivi. Yaani hapa Yona anarudia statement ya Mramba kuwa hata watanzania wakila nyasi yeye bado atafanya anachopenda!
 
Unajua Mkapa aliwafundisha kiburi watendaji wengi sana, na waliamini wao hawawezi kuguswa. Mfano hai, pata picha ya Mramba wa Mwinyi na Mramba wa Mkapa (wanachi watakula majani, lakini ndege lazima inunuliwe)!! Mwingine EL wa Mwinyi na EL wa Mkapa, na hadi alivyofikia kutapikia kwa JK. Wengineo waliofundishwa kiburi na Mkapa:
- Yona
- Mahita
- Chenge
 
Huyu Yona bado hajaelewa wimbi la mabadiliko ya kifikra linaoendelea sasa nchini. Hakuna atakayenda mahakamani, bali tutawanyang'anya Kiwira.

Hajui ni jinsi gani amewatibua wabunge, subirini kikao cha bajeti kuna mpango tunasuka ambao utakuwa somo kwa watawala mafisadi. Na hilo la yeye kuona ni mbunge wa CCM aendelee kushangaa tu maana hayuko mmoja na wengi wamejipanga foleni sasa wakipinga kutumia Ibara 15:1

subirini habari za leo kutoka Bungeni....
 
Cha kusikitisha zaidi, leo asubuhi waziri mkuu ameulizwa na Hamad Rashid ni kwa nini serikali inashindwa kumchukulia hatua Mkapa kwa kukiuka maadili akiwa ikulu. Jibu ikawa serikali inaangalia kama kuna kuna ushahidi wa kosa la jinai au ni tatizo linaloweza kumalizwa kisisasa. Inawezekana Yona anakuwa na kiburi kwa kuwa anajua hilo litashughulikiwa kisiasa.
 
Kwa hesabu ya harakaharaka Tanesco itakuwa taabani kama na kiwira nayo italipwa hiyo pesa. Nimejaribu kufnya hesabu hapa chini

kwa siku kwa mwezi (30 days) kwa mwaka
Richmond 152,000,000 4,560,000,000 55,480,000,000
Kiwira 146,000,000 4,380,000,000 53,290,000,000
Total 298,000,000 8,940,000,000 108,770,000,000

Kwa kifupi Tanesco alipe 298mln kila siku, 8.94billion kwa mwezi na 108.77 billion kwa mwaka.
units; TSH
 
Mkuu..., Yona anajaribu kuleta masikhara kwenye kazi nae 40 zake zimefikia tusubiri kumfanyia hitma yake tu asifanye wa-tz kama majendaeka kuamshwa mpaka wamwagiwe maji...Watu wako macho ati. Na mungu atamlaani na wenzake. Tutawanasa tu hao...
 
Back
Top Bottom