Mzee wa Ufipa katika ubora wake. Yeye kila kitu kinachofanywa na Serikali na chama tawala anakipinga. Huyu jamaa ataugua vidonda vya tumbo soon maana siku hizi anaandika kwa jazba na mihemko
Acha kudanganya vidonda vya tumbo vinasasabishwa na helicobacter pylori.Utawashika maskio wajinga wenzio.
 
Mzee tupa tupa unamkana mungu mwenge.Huoni chama pendwa kitakufa.
 
DHANA mwenge zamani ilitumika kuwaunganisha watu katika melengo ya kimaendeleo sasa dhana hiyo imepitwa na wakati. iwekwe katika kumbukumbu za taifa. Itumike dhana nyingine kuwaunganisha watu
 
Mzee VUTA-NKUVUTE duh umenikuna majuzi nimetishiwa na Mwenyekiti wa Kijiji nisipochangia Mwenge nimejiondoa mwenyewe kwenye kijiji chake nasema Kijiji chake si chetu hapana chake nikamwangalia kuanzia utosini hadi miguu iliyojaa sagamba nikampasha hadi hakapashika kwamba mchango wa Mwenge sitoi hata ndururu lau kama ni mchango wa madarasa,ujenzi wa barabara,ujenzi wa msikiti au kanisa nitatoa kwa moyo mweupeee.

Mbio za Mwenge ni ibada nikishiriki kwa mujibu wa Imani yangu maana yake niko nje ya kundi maana yake nimesaliti Imani yangu maana yake nimejiingiza katika Imani nyingine ambayo yaweza kupunguza uwezo wangu wa kufikiri na kuamua mambo.
Una akili sana.lile niliibada lakishetani.usishiriki kwa namna yoyote ile.
 
uwepo sana tena sana, lakini usikatishe mjini, upite kijiji kwa kijiji pembeni pembeni na kuzindua miradi iliyoko vijijini tu. mjini usipite kabisa na iwe marufuku bin makufuru kukatiza mji wa aina yoyote mkubwa kwa mdogo.
 
Sitaki. Nasema tena sitaki. Kama mmenichoka chamani mseme. Haiwezekani wakuu wangu wa kichama waniombe kuongeza nguvu kwenye mbio za ninachokipinga:Mwenge wa Uhuru.

Mwenge naupinga. Mwenge siupendi. Mwenge umenichemsha na kunichosha. Mwenye sitaki kuuona wala kuusikia. Mwenge umepitwa na wakati. Mwenge unatumalizia fedha kama taifa. Mwenge ni mzigo kwa taifa. Mwenge upumzishwe. Mwenge uwekwe makumbusho. Mwenge una hasara kuliko faida.

Nasema tena,sitakwenda wala kushiriki kwenye mbio za Mwenge. Sasa watanzania wamesusia mbio za Mwenge. Wanalazimishwa tu kuchangia,kusafisha na kushiriki. Si kama mwanzo. Mwenge huu si ule wakati tupo shule. Huu hauna kipaumbele kama ule. Tafadhali,nisihusishwe nao!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Una point. Kama ni kumbukumbu labda uwashwe siku ile 9/12 na kuzungushwa kiwanja husika na kupachikwa kwenye kilima bandia? Au ndio hutaki kabisa hata mawazo mbadala Mkuu?
 
Na hii misheria ya mitandao hii soon utasikia mzee tupatupa yupo mahakamani kwa "kukashifu" Mwenge!
 
Hivi wanajamvi ikulu imeshindwaje kuufutilia mbali mwenge wa Uhuru ukawekwa makumbusho kuna siri gani kuusu huo mwenge ??

Toka nimeanza kufatilia mbio za mwenge sijawai ona faida yake zaidi ya hasara kibao tunazopata kama nchi ndo maana nasisitiza mwenge ni janga la taifa

Unasafirisha watu wengi kwa wakati mmoja magari zaidi ya 100 nchi nzima
Alafu watu wanafika sehemu eti wanaweka jiwe la msingi kwenye darasa la milion 7 harafu wanalala eneo lile lile kwa garama za ajabu kweli

wako na wasanii wa Kuimba!
wako na madakitari wa kuwatibu !!
Wanakula!
Wanakunywa!

Yaani unazindua mladi wa million 7 alafu unatumia million 30 within the day
Alafu kama nchi mnakuja kusema mpo silius ?
Nyerere aliruhusu mwenge kipindi kile watu walikuwa awajaanza kujua matumizi kama sasa na matumizi ya wakati ule yalikuwa chini kwasababu ya kutokuwepo kwa inflation kama ilivyo sasa !!

ni haibu kwa nchi inayobana matumizi kuruhusu mwenge uendelee kukumbizwa nchi nzima kila mwaka!!

Niaibu kuzindua mladi wa million 7 wa jengo la dalasa arafu ukala pale pale
Kwa million 30!!!**********"*

Kama taifa tumepotea sana kwa kufanya mambo bila kushirikisha wananchi
'"Mwenge ni janga la taifa kila mtu anatakiwa kuupinga kwa nguvu na uwezi wake!!

"”"""Yaani unazuia umiseta arafu unaluusu mwenge""!!!
 
Hivi wanajamvi ikulu imeshindwaje kuufutilia mbali mwenge wa Uhuru ukawekwa makumbusho kuna siri gani kuusu huo mwenge ??

Toka nimeanza kufatilia mbio za mwenge sijawai ona faida yake zaidi ya hasara kibao tunazopata kama nchi ndo maana nasisitiza mwenge ni janga la taifa

Unasafirisha watu wengi kwa wakati mmoja magari zaidi ya 100 nchi nzima
Alafu watu wanafika sehemu eti wanaweka jiwe la msingi kwenye darasa la milion 7 harafu wanalala eneo lile lile kwa garama za ajabu kweli

wako na wasanii wa Kuimba!
wako na madakitari wa kuwatibu !!
Wanakula!
Wanakunywa!

Yaani unazindua mladi wa million 7 alafu unatumia million 30 within the day
Alafu kama nchi mnakuja kusema mpo silius ?
Nyerere aliruhusu mwenge kipindi kile watu walikuwa awajaanza kujua matumizi kama sasa na matumizi ya wakati ule yalikuwa chini kwasababu ya kutokuwepo kwa inflation kama ilivyo sasa !!

ni haibu kwa nchi inayobana matumizi kuruhusu mwenge uendelee kukumbizwa nchi nzima kila mwaka!!

Niaibu kuzindua mladi wa million 7 wa jengo la dalasa arafu ukala pale pale
Kwa million 30!!!**********"*

Kama taifa tumepotea sana kwa kufanya mambo bila kushirikisha wananchi
'"Mwenge ni janga la taifa kila mtu anatakiwa kuupinga kwa nguvu na uwezi wake!!

"”"""Yaani unazuia umiseta arafu unaluusu mwenge""!!!
1470741248310.jpg
 
Uhuru umeshapatikana mkoloni ameondoka,(kiaina)sasa ni za zamu ya mafisadi wakoloni weusi, makaburu weusi, huu mwenge uwamulike hawa mamluki.
 
Leo naona kiongizi wa mbio za mwenge akichoma moto zana za uvuvi haramu ktk ziwa Victoria.Hivi hili nalo lilisubiria mpaka mwenge ufike kweli?
 
Back
Top Bottom