Mimi sioni haja ya kuendelea kuwa na hizi mbio za Mwenge.

Hauna faida yoyote zaidi ya kueneza ujinga kwamba nchi ina amani na utulivu, huku watu wanaibiwa kodi na misaada ambavo vinaliwa au kutumiwa vibaya.

Penye mahali popote penye amani na utulivu panatakiwa pawe pameneemeka kiuchumi, kisiasa na kijamii na watu wote wana furaha, ukakika wa milo mitatu kwa siku, elimu, afya.

Mwenge kwa sasa naufananisha na mdundiko, na mkole mambo ambayo yanaleta ushawishi wa ngono, ulevi na watu kuwa wajinga zaidi.

Kuwe kampeni ingine kabisa mbadala ya kuhamasisha wananchi wawe wanawaza maendeleo bila kuwepo vizuizi visivo lazima, urasimu na UFISADI ambao ni watu wachache ndio wanafaidi Tanzania ya leo.

Ni juzijuzi tu ndio tunasikia eti hospitali ya Muhimbili ndio kwa mara ya kwanza yangu uhuru ndio imefanya upasuaji wa moyo! Hii ni aibu.

Mwenge ukiishakimbizwa mwaka huu iwe ni mara ya mwisho na uwekwe jumba la makumbusho, kwani una miaka 47 sasa na umeshikwashikwa sana, inatosha jamani!
 
wanaopinga mwenge huenda hawajafahamu madhumuni ya mwenge. si kweli kuwa kwa vile siku ya Xmas watu wanalewa sana na wanasex sana na wanafanya fujo kwa hio uhalali wa Xmas umeondoka na ifutwe. siamini hivyo pia kwetu sisi waislam ktk siku kuu zetu.


la msingi ni kuzingatia yale madhumuni ya shughuli hizo na kuwajenga hisia za ndani wafuasi wake.

mwenge ni alama ya uhuru wetu, na ni alama ya umoja wetu nia alama ya kuondosha kiza na kuleta mwanga ktk taifa letu na mengi mengine na nnategemea ni mazuri sasa ndio mwalimu wangu MKjj anasema sasa mwenge hauunguzi tena kama ilivyo Xmas au eid cha kufanya ni kuurejeshea nguvu zake za kuunguza iwe mafisadi au maradhi au ujinga na ulete msisimko kwa wananchi na viongozi kuwa tulidai uhuru wa taifa hili ili tuweze kuleta maendeleo yetu sasa jee tumefikia wapi?


siku hizi ndio iwe kipimo cha tulipofikia na kurekebisha mapungufu yake.


mie nnapendekeza huu mwenge uwe modified ili uweze kuonekana vizuri pia uweze kubebwa na kila mtanzania wadogo na wakubwa walemavu na wazima wenye afya na madhaifu.

nnaomba kuwasilisha
 
Ungeweza kumulika kama ungepitishwa maeneo ya ;
1.Masaki.
2. Mikocheni.
3.Mbezi Beach.
4. Kichanga Chui.

Na maeneo yote walipo mafisadi wetu labda ungeweza kumulika na Rais kuweza kuona ila kitendo cha kuupeleka ukamulike huko Mbelekajima, Omurshaka, Nyakibimbili, Dongobeshi,Buzwagi, Nguruka, Nakijiko, Kibanda maiti, mchamaba wima n.k hakuna maana hata kidogo.

Kuna mgombea urais mmoja 2005 alisema akichaguliwa atauweka kwenye jumba la makumbusho ya taifa .

Sioni mantiki na maana ya mwenge kama hata kuuwasha lazima ukawashwe nyumbani kwa kiongozi basi hakuna sababu.

Ama niungane na Mbunge Erasto Tumbo wa UDP mwaka 2002 aliposema kuwa hakuna haja ya kuwa na Mwenge , na serikali ikiona kuna ulazima sana basi ihakikishe kuwa inatengeneza kiwanda cha kuzalisha mienge mingi na kila mwananchi aweze kuupata wa kwake na ndipo akiona hamu ya kuuona mwenge basi awashe wa kwake na kukimbia nao nyumabni kwake na sio vinginenvyo.

Kuna matumani gani wakati taifa liko kwenye msiba ulioletwa na mafisadi?
Kuna matumaini gani wakati bei ya mafuta inawaangamiza wananchi?
Kuna matumaini gani wakati Zanzibar wapo gizani hii wiki ya pili sasa?
Kuna matumaini gani wakati Pemba wanatengwa na hata kutaka kujitenga?
Kuna matuamini gani wakti tuliowapa dhamana ya kutuongoza wanageuka kuwa wezi wakubwa dhidi yetu?

Sioni matumaini.
 
Ungeweza kumulika kama ungepitishwa maeneo ya ;
1.Masaki.
2. Mikocheni.
3.Mbezi Beach.
4. Kichanga Chui.

Na maeneo yote walipo mafisadi wetu labda ungeweza kumulika na Rais kuweza kuona ila kitendo cha kuupeleka ukamulike huko Mbelekajima, Omurshaka, Nyakibimbili, Dongobeshi,Buzwagi, Nguruka, Nakijiko, Kibanda maiti, mchamaba wima n.k hakuna maana hata kidogo.

Kuna mgombea urais mmoja 2005 alisema akichaguliwa atauweka kwenye jumba la makumbusho ya taifa .

Sioni mantiki na maana ya mwenge kama hata kuuwasha lazima ukawashwe nyumbani kwa kiongozi basi hakuna sababu.

Ama niungane na Mbunge Erasto Tumbo wa UDP mwaka 2002 aliposema kuwa hakuna haja ya kuwa na Mwenge , na serikali ikiona kuna ulazima sana basi ihakikishe kuwa inatengeneza kiwanda cha kuzalisha mienge mingi na kila mwananchi aweze kuupata wa kwake na ndipo akiona hamu ya kuuona mwenge basi awashe wa kwake na kukimbia nao nyumabni kwake na sio vinginenvyo.

Kuna matumani gani wakati taifa liko kwenye msiba ulioletwa na mafisadi?
Kuna matumaini gani wakati bei ya mafuta inawaangamiza wananchi?
Kuna matumaini gani wakati Zanzibar wapo gizani hii wiki ya pili sasa?
Kuna matumaini gani wakati Pemba wanatengwa na hata kutaka kujitenga?
Kuna matuamini gani wakti tuliowapa dhamana ya kutuongoza wanageuka kuwa wezi wakubwa dhidi yetu?

Sioni matumaini.
 
wanaopinga mwenge huenda hawajafahamu madhumuni ya mwenge. si kweli kuwa kwa vile siku ya Xmas watu wanalewa sana na wanasex sana na wanafanya fujo kwa hio uhalali wa Xmas umeondoka na ifutwe. siamini hivyo pia kwetu sisi waislam ktk siku kuu zetu.


la msingi ni kuzingatia yale madhumuni ya shughuli hizo na kuwajenga hisia za ndani wafuasi wake.

Good coments sir! Kuna indication kuwa you not nly think with IQ but wth a deep aspects of EI.
 
Let alone lost productivity and time, mnajua adha za michango ya mwenge kwa wananchi masikini? Michango hii inakuja on top of michango ya harusi na mingine mingi tu?

Hivi kabla ya kuanza kuutetea mwenyge huu tunajua unagharimu kiasi gani? Na nchi yetu masikini inaweza ku afford gharama hizi?

This is an extravagant relic of a bygone era and should not be entertained by modern Tanzania.
 
Kuna matumani gani wakati taifa liko kwenye msiba ulioletwa na mafisadi?
Kuna matumaini gani wakati bei ya mafuta inawaangamiza wananchi?
Kuna matumaini gani wakati Zanzibar wapo gizani hii wiki ya pili sasa?
Kuna matumaini gani wakati Pemba wanatengwa na hata kutaka kujitenga?
Kuna matuamini gani wakti tuliowapa dhamana ya kutuongoza wanageuka kuwa wezi wakubwa dhidi yetu?

Sioni matumaini.

I solidly appriciate this post. Niogozeee....

Take away the normal way of looking at thigs...Go above your IQ..use your EI ... you will see more and more and the deeper thngs ..kwenye hiyo Formula inayoitwa..kukimbizwa kwa mwnge wa uhuru.

Kabla ya kuendelea do the same exercise..kwenye hiyo formula inayoitwa kifo cha Balali...If you use your EI ..utaona kuwa Balali yuko hai kisiasa,Balali yuko..hai Kiroho..balali yuko hai..Kiuchumi..and balali...Kimwili... It all depends on how you crack this things..and ..what tools....etc

Very soon huo Mwenge huo..!

Narudia..!

Kama ilivyo kwa Kifo cha Balali..na future yake..!

Hicho kibatari hicho..wil' come with something you never X_peted....just like Balalis death!!!?!!!

And you will know there is more than IQ n this world.

Huwezi kucheza na EI ya Taifa kama la Tanzania kizembe zembe tu na ukafikiri you will be safe..No ..Never!

Ni upuuzi wa kiwango cha juu...kinachowafanya Viongozi wa Tz wasione shina la Nchi inayoitwa Tanzania.

Wapi inatoka...wapi ..ilipo na wapi inakwenda.

If they{VIONGOZI} hard an eye..na kuona kuwa they are done already..
na.. Ezi za Azimio jipya Hazipingiki tena.... Mwenge wa uhuru then wangetambua kuwa...huo mwenge sio kama unvyonekena...Nikama kifo cha Balali...that is just an appearance! dont miX up the appearence and the reality!

Mungu Ibariki TZ
 
Gloria Tesha
Daily News; Thursday,May 29, 2008 @00:05

MBIO za Mwenge wa Uhuru ni moja ya matukio yenye kulinda na kukuza historia ya nchi. Matukio hayo yanalenga kuwaenzi wanaharakati, viongozi na wananchi waliopigana kufa na kupona, kuhakikisha kuwa taifa linakuwa huru kabla na baada ya Uhuru mwaka 1961.

Kwa mara ya kwanza Mwenge wa Uhuru, uliwashwa juu ya kilele cha Mlima Kilimanjaro Desemba 9 mwaka 1961 na Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere. Tangu mwaka huo, serikali ikiongozwa na chama tawala cha Tanganyika African National Union (TANU) iliratibu na kuendeleza Mbio hizo za Mwenge wa Uhuru.

Baada ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, mbio hizo ziliimarishwa zaidi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ziliimarishwa kwa lengo la kukuza umoja na mshikamano miongoni mwa Watanzania bila kujali tofauti za kabila, rangi, itikadi na dini. Hivyo, kwa miaka mingi kazi ya kuendesha Mbio za Mwenge, ilikuwa ikifanywa na TANU.

Hata hivyo, taarifa mbalimbali za historia ya Mwenge wa Uhuru, zilizopatikana kutoka wizara inayoratibu mbio hizo, ambayo ni Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana hasa Idara ya Maendeleo ya Vijana, zinaeleza kuwa mfumo wa kukimbiza Mwenge wa Uhuru ilibidi ubadilishwe mwaka 1993, kutokana na mabadiliko ya kisiasa, yaliyotokea nchini mwaka 1992.

Mwaka huo, nchi iliacha mfumo wa chama kimoja cha siasa na kuingia katika siasa ya vyama vingi. Kutoka mwaka huo, Mbio za Mwenge wa Uhuru zilirejeshwa chini ya utaratibu wa Serikali mwaka 1993.

Sasa ni mwaka wa 15 tangu Serikali ianze kuratibu na kusimamia mbio hizo, lengo likiwa ni kuondoa dhana ya kwamba Mwenge wa uhuru ni wa chama tawala, ambacho kwa sasa ni CCM. CCM ilizaliwa kutokana na muungano wa TANU na ASP ya Zanzibar. Huko nyuma, utaratibu wa mbio za Mwenge wa Uhuru, ulikuwa ukifanywa na Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM).

Mbio za Mwenge wa Uhuru hupita katika nchi, mikoa, wilaya na vitongoji mbalimbali, kwa kufuata falsafa ya Mwenge wa Uhuru, iliyoanzishwa na Mwalimu Nyerere enzi za uhai wake. Humulika palipo na giza na kwa sasa unamulika rushwa na maovu ya watendaji katika ngazi mbalimbali nchini.

Mbio za Mwenge ni kielelezo cha mshikamano Mwenge wa Uhuru umetoa mchango mkubwa katika kudumisha mshikamano wa kitaifa, amani, upendo na umoja miongoni mwa Watanzania.

Vilevile, mbio za Mwenge huo zimeweza kuleta msukumo wa pekee katika maendeleo ya Watanzania, hasa katika shughuli za kiuchumi, kijamii na kiutamaduni. Serikali imekuwa ikihamasisha wananchi na makundi mbalimbali, kuunganisha nguvu, kwa kuchangia kwa hali na mali ili kufanikisha miradi mbalimbali ya maendeleo.

Mwenge huzindua miradi ya kijamii Mbio za Mwenge wa Uhuru zimekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha dira ya maendeleo inapatikana, kwa kuweka nguvu kwenye mapambano dhidi ya Ukimwi na vita dhidi ya umasikini na ukosefu wa ajira kwa vijana.

Mchango wake unajidhihirisha wazi, kwani mbio hizo zimewezesha kuanzishwa kwa miradi mingi ya kijamii. Kwa mujibu wa taarifa za Wizara hiyo mwaka 1961 hadi mwaka 1998, miradi yenye thamani ya Sh bilioni 15 iliweza kuzinduliwa tofauti.
Na tangu mwaka 1998 hadi sasa, miradi mingine ya zaidi ya Sh bilioni 80 imezinduliwa. Miradi hiyo ni sekta ya afya na ujenzi wa shule, kupitia michango ya wadau, wahisani na wananchi wenyewe. Aidha, mbio hizo zimeelekeza nguvu katika Utandawazi, haki ya mtoto iliyopitishwa katika mikataba mbalimbali ya kimataifa.

Pia, mbio hizo zinahimiza umuhimu wa kudumisha amani na upendo wa kweli, vilivyoiwezesha nchi na wananchi wake kuwa ndugu. Kumekuwapo na ushirikishwaji au usawa kijinsia na uhamasishaji wa Watanzania, juu ya masuala mbalimbali ya maendeleo ya kiuchumi kijamii na kiutamaduni.

Ujumbe wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka jana, ulizingatia dira, programu, malengo, mikakati na masuala muhimu, yanayowakabili Watanzania na jamii ya Kimataifa. Mbio hizo zinaimarisha juhudi za serikali katika kufikiria nini kifanyike na kwa wakati gani kwa maslahi ya Taifa.

Licha ya vita dhidi ya Ukimwi, Mbio za Mwenge wa Uhuru zimeelekeza vita dhidi ya rushwa, kwa kaulimbiu na hotuba za viongozi katika kila mkoa, wilaya, tarafa, kata, vijiji na maeneo unakopita kukemea kwa dhati wote wanaojihusisha katika vitendo vya rushwa na ufisadi.

Mbio za Mwenge wa Uhuru hutoa elimu kuhusu majanga mbalimbali ya kitaifa, ikiwa ni pamoja na namna ya kufahamu sheria za ardhi, rushwa, mazingira na haki za binadamu ili kutoa fursa kwa wananchi kujua haki zao. Hulinda utamaduni Kwa upande wa utamaduni, ngoma za makabila mbalimbali huchezwa Mwenge unakopita.

Ngoma hizo huwa na nyimbo na maneno ya kukumbusha mila na utamaduni, kwa watu wa rika mbalimbali ili kuhakikisha historia haipotei. Pia, huwapo maonyesho ya bidhaa zilizo za kiutamaduni na zinazolenga kufikisha ujumbe wa kaulimbiu ya mwaka husika.

Waraka wa Mbio za Mwenge ulipitishwa mwaka 2000 na Baraza la Mawaziri ili kuruhusu mabadiliko kadhaa. Waraka huo ulipitisha kuwa katika kilele cha Mbio za Mwenge kila mwaka, kuwe na Wiki ya Maonyesho ya kazi za Vijana na wadau wengine.

Waraka huo pia uliongeza idadi ya wakimbiza Mwenge, kutoka wanne hadi sita, huku msisitizo mkubwa ukiwa ni kwa wanawake, angalau wawe wawili. Suala hili limeimarisha harakati za usawa wa kijinsia.

Hakika Mbio za Mwenge wa Uhuru, zimesaidia kulinda uhuru wa nchi, kupiga vita maadui wa jamii na kuhimiza matumizi mazuri ya rasilimali za nchi kwa faida ya vizazi vijavyo. Mungu Ibariki Tanzania, Mungu wabariki Watanzania.
 
Hogwash,

Mbio za Mwenge wa Uhuru hutoa elimu kuhusu majanga mbalimbali ya kitaifa, ikiwa ni pamoja na namna ya kufahamu sheria za ardhi, rushwa, mazingira na haki za binadamu ili kutoa fursa kwa wananchi kujua haki zao

My beef exactly.

We do not need "Mbio za Mwenge" to do that, watendaji lukuki na redundant walioko huko wilayani, kwenye tarafa, kata na vijiji wanafanya nini?

Tatizo ni kwamba Chama na serikali bado vina fikra za "top down" kwamba tutawapelekea mwenge ukawamulike na kuwaelimisha.Tunahitaji lateral involvement and people based initiatives.Ningewaelewa kama wangefocus kuendeleza grassroot organizations, but there is no political glory in that.

This is a rather expensive excuse to splurge in largesse we cannot really afford because we do not have such resources.
 
Mchango wake unajidhihirisha wazi, kwani mbio hizo zimewezesha kuanzishwa kwa miradi mingi ya kijamii. Kwa mujibu wa taarifa za Wizara hiyo mwaka 1961 hadi mwaka 1998, miradi yenye thamani ya Sh bilioni 15 iliweza kuzinduliwa tofauti.
Na tangu mwaka 1998 hadi sasa, miradi mingine ya zaidi ya Sh bilioni 80 imezinduliwa. Miradi hiyo ni sekta ya afya na ujenzi wa shule, kupitia michango ya wadau, wahisani na wananchi wenyewe. Aidha, mbio hizo zimeelekeza nguvu katika Utandawazi, haki ya mtoto iliyopitishwa katika mikataba mbalimbali ya kimataifa.



Mwanakijiji,

Kwahiyo hii wizara inataka kutueleza kwamba huu mwenge ulipokuwa unakimbizwa, then ndio miradi ya hizo bilioni zilizotajwa hapo juu ndio ikaanzishwa just kwa kitendo cha mwenge kupitia maeneo hayo? Are we wadanganyika enough kuambiwa huu utumbo? Je, haya maneno kweli yana-deserve kutolewa na wizara husika ama yaliongelewa wakati watu wanapata "gahawa"?

Unajua, hawa jamaa wanafikiria wadanganyika wote ni kama wale wana vijiji wa kwa Lowassa, Chenge na Mkapa. Wanafikiria ni rahisi kupotosha ukweli halafu at the end wananchi watawapigia makofi kama walivyofanya watu wa kijijini kwa akina Mkapa, Lowassa & Chenge. We are good enough to criticize their #@%$!7*+. Haya maneno wangeyasema miaka 30 iliyopita tungewapigia makofi, ila sio leo katika karne hii ya 21. Huu ni ujinga!!!!!
 
Mwengeee.. mwenge - mbio mbio
Mwenge tunauikimbiza - mbio mbio
Kuwachoma mafisadi - mbio mbio
Mpaka waachie nchi - mbio mbio!!
mwenge mwenge!! mbio mbio~
mwenge tunaukimbiza - mbio mbio
Uhuru wetu twalinda - mbio mbio!!!
Hatuwazirii nchi - mbio mbio!!

Mwanakijiji,

Huu mwenge wa Uhuru ndio ilikuwa ni alama ambayo ilikuwa ikituunganisha Watanzania na kujihisi kama ni true Tanzanian!

hiyo Quote hapo juu imenikumbusha nilipokuwa Shule ya Msingi kuanzia kuchangia mbio za Mwenge wa Uhuru kisha kukusanyika shule tofauti za mkoa katika kituo kimoja na kushiriki katika michezo mbali mbali kuonyesha ushirikiano na Umoja wetu kabla ya kuupokea mwenge wa Uhuru. Hakika ilikuwa ni siku kubwa kwetu tulipokuwa tunangoja Mwenge wa Uhuru kufika mkoani. Ni mara moja kwa Mwaka na hakika nuru yake ilikuwa inamulika maisha yetu kwa mwaka mzima tukingoja tena mbio za Mwenge kwa kujiandaa na Nyimbo, Mashairi na Ngonjera.

Kwa Tanzania ya sasa Mwenge wa Uhuru uwe wa Kitaifa na ukimbizwe na sisi, watu wenye Uchungu na nchi yao. Mwenge wa Uhuru uwashwe katika mioyo yetu, tuwe na mioyo ya kianamapinduzi. Na Uchungu na Nchi yetu.

Kwa nini Siku hizi Mwenge umekuwa ukikimbizwa na Watanzania wa kipato cha chini na wenye hali duni tu?

Kwa nini tusiutumie Mwenge Wa Uhuru kama Kiunganishi cha Utaifa Wetu?

Kwa nini Mwenge wa Uhuru usitumike kuwafichua Viongozi mafisadi ambao walipewa dhamana ya Kmuongoza na sisi wenyewe?

Kwa nini usifichue wala Rushwa?

Kwa nini usipambane na Umasikini uliolighubika taifa letu?

Kwa nini Mwenge wa Uhuru unatumika kuonyehsa madaraja ya Uchumi kati yetu Watanzania?

Tanzania inaeleka wapi?

na Mwisho kwa nini Mwenge wa Uhuru tumeugeuza kuwa wa Chama Kimoja?
 
Mwenge huu ambao umeanza kukimbizwa tena, uwashe ndani ya mioyo yetu moyo wa kizalendo na mawazo ya kimapinduzi na tusikubali yale matamanio ya kuwa na Taifa la kisasa, lenye haki na nafasi sawa kwa wote, na ambalo ni nyumba ya matumaini kwa wana na mabinti zake hayazimwi kwa hofu, na kamwe yasiache kufifia na kupoteza joto lake!

Hii ni mojawapo ya vitu ambavy are uniquely Tanzanian na nimojawapo ya tamaduni ambazo zinapaswa kuendelezwa na kuboreshwa ili mwenge huu ambao wanajeshi wetu wanauvaa kwenye ngao zao, ambao uko kwenye nembo za Taifa letu, na ukiwa katika alama kadha wa kadha za taasisi zetu uzidi kuwa kweli mwenge wa matumaini na unaoangaza katika mioyo ya Watanzania!

Binafsi ningependa kutuma salamu za mwenge kwa watanzania wote popote pale walipo, kuwa moto wa mabadiliko ya kifikra na moto wa mapenzi ya nchi yetu uzidi kutuunguza na kutumilika kiasi kwamba kama tulikuwa gizani tuanze kuondoka wenyewe kabla hatujachomwa! Katika siku hii ya kwanza ya mbio za mwenge, Watanzania wote tusimame kama mtu mmoja na kuhakikisha kuwa Taifa letu letu halizimwi, na mwanga wa mawazo yetu haufunikwi tena! Tuzidi kuamka na kuangaza kama jua la alfajiri na kama mbalamwezi ingazayo usiku wa manane tuendelee kumilika hata kule kwenye giza bila ya sisi wenyewe kugeuka giza!!

Habari zaidi na Picha tembelea KLH News where we bring the news.. first!

Mzee this is great!!!

Kwa mshangao mkubwa usiotegemewa... very soon patatokea Mjadala usioeleweka umetoka wapi hasa...kuhusu huu Mwenge na maana yake. and its practicle application in our Era.

Kwa kuwa watu wengi (hasa viongozi wetu) wanafikiria na kuona si zadi ya umbai wa nja ya pua zao..watashangaa, kama mzaha vile ....hawatategemea kitakachofumuka ..beyond that figurative thing..Then it will bring what waz nt once though is possible..!

Take time and contemplate..before you jump into any conclusion...Tusinfanye kazi na kuchukua maamuzi ya msingi kwa kutumia mazoea tu...

Kaa tulia fikicha fikra na ufahamu....!

Ona mtu kama EL et al..walitegemea mazoea na mitizamo mgando..kamwe hawakufikiri wangekuwa walipo sasa..Tujifunze kusoma nyakati and "never go counter..IT" We need to be very dynamic..kufuzu hilo.

Hiyo alama ya Mwenge usiitizame kwa "makengeza" ya uzoefu... Ni fumbo lenye very practicle application hasa Leo na hali ya nchi ilivyo.

I tell you this; it can be used POSITIVELY to activate MASS CONSCIOUSNESS TOWARD THE GOOD OF MANKIND/THE NATION..beyod any bodys imaginations! Good psychologist/EI technicians knows very clearly about this... Na imeshawahi kufanyika mahali pengine.

Warusi etc wanajua sana habari hii...but always they do it in NEGATIVE way...But Mwenge umebeba Character positve to our nation... na viongozi wengi watake wasitake ..the thing is in their subconsciouse mind, ipo kwenye nembo ya taifa, kwnye kila kofia ya mwanajeshi wa nchi hii, kwnye alama mbalimbali za kijamii,minara lukuki..it can be made to work.

Swali.. who knew all this.., na akapachika kila mahali jambo hili?

Kwa kuchukua muda na kuu_discuss ... Hasa nyakati kama hizi..Ina_Activate a very special CHANGES ndani yaufahamu wa kila muhusika....na haitakoma tena this time!!

You need only to coment about it..Kwenda kulia, katikati au kushoto inatosha..na kinachotakiwa kufanyaka .. kitafanyika..!

That IS ALL IN THE WORD OF EI...No Escaping.

Mungu ibariki Tazania.
 
Naungana na wale wote wanaosema Mwenge ufutwe. Ni ulaji wa kodi zetu bila msingi wowote. MWENGE UFUTWE!
 
labda nijiulize usahihi wa mwenge wa uhuru. je malengo yametimia?? kama yametimia nini kinfuata, kama bado ni wapi parekebishwe??
halafu kwa nini background colours za sherehe za uwashwaji wa mwenge ni za ccm?? je ni tukio la kichama au kitaifa??

nawhurumia viongozi wetu wenye fikra mgando na sio wabunifu
 
well,well well! Hivi wakuu Mwenge huo wa uhuru unatusaidia nini? Kama ulishawashwa kwa mara ya kwanza na miaka yote hiyo kwanini usipelekwe makumbusho?

Taifa linapata hasara bure,hilo suala ni mojawapo wa unnecesary expenses amabazo government inaingia tu.Hapo pia kumekua na channel za mafisadi.

Tujiulize swali,Ni nchi ngapi duniani hazina kitu kama mwenge wa uhuru na bado kuna amani tu? Hebu tujaribu kucancel bajeti za kiuendawazimu kama hizi tuwachukue watoto wa mitaani tuwaweke camp na tuwape elimu.
 
Tangu nilipokuliwa bado mtoto nilikuwa nasikia stori za mwenge kukimbizwa.Jana jioni nikiwa naangalia taarifa ya habari nikaona tena mambo ya mwenge.Mara kibao nimewahi kuona misururu mikubwa ya magari na watu wengi sana katika hekoheko za Mwenge.
Ninaloomba kwenu wakuu nieleweshwe ni nani analipia hizi gharama za kukimbiza mwenge,umuhimu wake,nani alianzisha,imeanza mwaka gani,na kama ina specific time period ya kuisha!
Nawasilisha Hoja!
 
Mkuu Kevo,ukweli ni kwamba mwenge hauna maana yoyote,ni kutuingiza katika gharama zisizo kuwa na ulazima kwani yale ambayo mwenge unayafanya yanaweza kufanyika bila ya mwenge.Ninavyofaham mimi,pesa ya kukimbizia mwenge uchangwa na wafanyakazi wa serikali kwa kukwata katika mishahara yao,hii ni kote bara na zanzibar.Sina uhakika kama utaratibu huu umeshabadirika,lakini zanzibar bado utaratibu huo upo.Wenyewe mchango huu umepewa sura ya kujitolea lakini kujitolea kwenyewe kumekaa kimtego mtego
 
Kevo kula tano....utakuwa wanavijiji wanalazimishwa kuchangia...Wenye mifugo kuku, Mchele wao, basi wanalazimishwa...

Kwa wale wenye wake, Watoto wa Kike, ndo vile tena....watamegwa tu na the so called wakuu wa misafara...imefikia wakati Ibada hizi za Motto ziachwe

Huu Mwenge haukuwa na mpango hapo Awali, Sasa na hapo baadae..UFUTWE!!!
 
Back
Top Bottom