Laptop01
JF-Expert Member
- Nov 29, 2009
- 1,365
- 796
Mnamo mwaka 1992, rasmi Taifa letu liliingia katika Mfumo wa Vyama vingi vya Siasa. Inaelezwa kwamba Mfumo huu haukuwa chaguo la Wananchi waliowengi (80% ya idadi ya watanzania waliohojiwa miaka hiyo).
Hata hivyo, Mwl. Nyerere akaona siyo kweli kwamba waliowengi ndiyo wako sawa wakati wote; akaamuru nchi ifuate mtazamo wa wananchi wachache waliotaka vyama vingi (20% ya idadi ya watanzania waliohojiwa miaka hiyo). Mtazamo mpana ilikuwa ni katika umuhimu wa vyama vingi vya siasa nchini katika kuchochea uwazi, ufanisi na uwajibikaji wa serikali iliyopo madarakani.
Kwa mtazamo wangu binafsi naona kama CUF inaenda kinyume na mtazamo huo mpana aliokuwa nao Mwl. Nyerere. Mtazamo wa vyama vingi vya siasa kusaidia kuleta maendeleo ya wananchi na nchi kwa ujumla kwa kuchochea uwazi, uwajibikaji na ufanisi wa Serikali iliyoko madarakani. CUF mmejisahau kabisa, mnatia aibu, mnaaibisha mmetupilia mbali dhana ya kuchochea maendeleo kwa kudai uwazi, uwajibikaji na ufanisi wa serikali iliyoko madarakani. CUF mnapambana na SERIKALI KIVULI YA CHADEMA. Great shame!
Siyo vibaya kuleta siasa za kukosoana, kuelimishana, kujengana na kurekebishana pale mnapoona mwenzenu fulani (here to mean chama fulani cha siasa miongoni mwenu) kinaenenda kwa namna ambayo haifai kwa ustawi wa taifa na watu wake. MKOSOENI na KOSOANENI kwa kuwa Tanzania ambayo kila chama cha siasa kinaililia kuiongoza ni yetu sote. Lakini katika hili, CUF hamko hivyo! Shame on you! Kazi yenu imekuwa ni kupambana na Serikali kivuli ya CHADEMA huku mkisahau kuleta uchochezi katika huduma bora za maji safi na salama mjini na vijijini, huduma za viwango vya juu ya elimu na mafunzo ya ufundi, kushuka kwa mfumuko wa bei na MFUMUKO WA UFISADI nchini.
CUF mmekuwa mkiimba nyimbo zinazotyuniwa na CHADEMA kwa lengo la kukandamizana nyie wenyewe mlio vyama vya upinzani. Mfano wa nyimbo hizo ni wimbo wa Operation Sangara Mkauitikia, Wimbo wa M4C mmeuitikia, nasikia mmeanzakuitikia hata kwa wananchi kujishika kichwani ati kulaani wanaowatumia vijana katika siasa. very shame and severe lack of innovativeness.
Ni maoni tu.
Hata hivyo, Mwl. Nyerere akaona siyo kweli kwamba waliowengi ndiyo wako sawa wakati wote; akaamuru nchi ifuate mtazamo wa wananchi wachache waliotaka vyama vingi (20% ya idadi ya watanzania waliohojiwa miaka hiyo). Mtazamo mpana ilikuwa ni katika umuhimu wa vyama vingi vya siasa nchini katika kuchochea uwazi, ufanisi na uwajibikaji wa serikali iliyopo madarakani.
Kwa mtazamo wangu binafsi naona kama CUF inaenda kinyume na mtazamo huo mpana aliokuwa nao Mwl. Nyerere. Mtazamo wa vyama vingi vya siasa kusaidia kuleta maendeleo ya wananchi na nchi kwa ujumla kwa kuchochea uwazi, uwajibikaji na ufanisi wa Serikali iliyoko madarakani. CUF mmejisahau kabisa, mnatia aibu, mnaaibisha mmetupilia mbali dhana ya kuchochea maendeleo kwa kudai uwazi, uwajibikaji na ufanisi wa serikali iliyoko madarakani. CUF mnapambana na SERIKALI KIVULI YA CHADEMA. Great shame!
Siyo vibaya kuleta siasa za kukosoana, kuelimishana, kujengana na kurekebishana pale mnapoona mwenzenu fulani (here to mean chama fulani cha siasa miongoni mwenu) kinaenenda kwa namna ambayo haifai kwa ustawi wa taifa na watu wake. MKOSOENI na KOSOANENI kwa kuwa Tanzania ambayo kila chama cha siasa kinaililia kuiongoza ni yetu sote. Lakini katika hili, CUF hamko hivyo! Shame on you! Kazi yenu imekuwa ni kupambana na Serikali kivuli ya CHADEMA huku mkisahau kuleta uchochezi katika huduma bora za maji safi na salama mjini na vijijini, huduma za viwango vya juu ya elimu na mafunzo ya ufundi, kushuka kwa mfumuko wa bei na MFUMUKO WA UFISADI nchini.
CUF mmekuwa mkiimba nyimbo zinazotyuniwa na CHADEMA kwa lengo la kukandamizana nyie wenyewe mlio vyama vya upinzani. Mfano wa nyimbo hizo ni wimbo wa Operation Sangara Mkauitikia, Wimbo wa M4C mmeuitikia, nasikia mmeanzakuitikia hata kwa wananchi kujishika kichwani ati kulaani wanaowatumia vijana katika siasa. very shame and severe lack of innovativeness.
Ni maoni tu.