Mwanza wamtaka Kikwete ajiuzulu

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
Mwanza wamtaka Kikwete ajiuzulu


na Mwandishi wetu, Mwanza


amka2.gif
CHAMA cha Wafanyakazi wa Taasisi ya Elimu ya Juu, Sayansi, Teknolojia, Habari na Utafiti nchini (RAAWU), mkoani Mwanza kimewataka Rais Jakaya Kikwete na Waziri wa Mambo ya Ndani Shamsi Vuai Nahodha waachie ngazi mara moja kutokana na kashfa ya Dowans na vurugu zilizosababisha maafa na vifo vya raia mkoani Arusha.
Mwingine ambaye ametakiwa kujiuzulu ni Inspekta Jenerali wa Polisi Said Mwema. Wanadai viongozi hao watatu wameshindwa kutimiza vema wajibu wao na maamuzi yao tata yamesababisha maafa ambayo yangeweza kuepukika.
RAAWU pia imewataka Watanzania kutoogopa wanaposimamia na kutetea haki zao za msingi Kikatiba kwani ni dhahiri kwamba serikali ya Rais Jakaya Kikwete imeyumba mno na imekosa mwelekeo wa kiutawala.
Kauli ya RAAWU ilitolewa jana na Katibu wa RAAWU Kanda ya Ziwa, Ramadhan Mwendwa, katika mahojiano maalumu na Tanzania Daima juu ya mustakabali wa nchi.
Alisema Rais Kikwete hawezi kukwepa kashfa ya Dowans ambayo sasa serikali inalazimika kuilipa mabilioni ya shilingi wakati maisha ya wananchi yakiwa duni. Dowans ndiyo ilirithi mikoba yaRichmond ambayo ilibebwa na Baraza la Mawaziri chini ya Rais Kikwete na kupewa mradi wa kufua umeme wa dharura huku wakijua kuwa haikuwa na uwezo huo.
"Sisi RAAWU tunashawishika kuamini kwamba Rais Kikwete ameshiriki moja kwa moja katika mkataba wa Dowans, ndiyo maana ameshindwa kuueleza umma juu ya kampuni hii. Inaonekana hapa kuna mchezo mchafu unafanywa na viongozi wetu... haiwezekani serikali inatangaza kulipa mabilioni ya fedha bila Bunge na Baraza la Mawaziri kuridhia" alisema Mwendwa.
Aidha, Mwendwa alimmwagia sifa nyingi Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, kwa kukataa Dowans kulipwa mabilioni hayo ya fedha, na kusema: "Waziri Sitta anajua ujanja unaochezwa hapa."
Vile vile, alihoji sababu ya serikali kuendelea kuilipa kampuni ya IPTL, huku ikilisukumia mzigo Shirika la Ugavi wa Umeme (TANESCO) lilipe fedha hizo wakati mikataba imesainiwa na serikali.
Alisema IGP Mwema na Waziri Nahodha wameonekana kushindwa kuwatumikia Watanzania, ndiyo maana idara zao zimeanza kutumia nguvu kwa kuua raia wasiokuwa na hatia.
"Polisi haina mamlaka ya kupiga risasi na kuua wananchi wanaoandamana kwa amani, tena hawana silaha wala hawajafanya fujo. Kwa maana hiyo, tunataka Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na IGP Mwema waachie madaraka yao haraka sana" alisema.
 
Mwanza wamtaka Kikwete ajiuzulu


na Mwandishi wetu, Mwanza


amka2.gif
CHAMA cha Wafanyakazi wa Taasisi ya Elimu ya Juu, Sayansi, Teknolojia, Habari na Utafiti nchini (RAAWU), mkoani Mwanza kimewataka Rais Jakaya Kikwete na Waziri wa Mambo ya Ndani Shamsi Vuai Nahodha waachie ngazi mara moja kutokana na kashfa ya Dowans na vurugu zilizosababisha maafa na vifo vya raia mkoani Arusha.
Mwingine ambaye ametakiwa kujiuzulu ni Inspekta Jenerali wa Polisi Said Mwema. Wanadai viongozi hao watatu wameshindwa kutimiza vema wajibu wao na maamuzi yao tata yamesababisha maafa ambayo yangeweza kuepukika.
RAAWU pia imewataka Watanzania kutoogopa wanaposimamia na kutetea haki zao za msingi Kikatiba kwani ni dhahiri kwamba serikali ya Rais Jakaya Kikwete imeyumba mno na imekosa mwelekeo wa kiutawala.
Kauli ya RAAWU ilitolewa jana na Katibu wa RAAWU Kanda ya Ziwa, Ramadhan Mwendwa, katika mahojiano maalumu na Tanzania Daima juu ya mustakabali wa nchi.
Alisema Rais Kikwete hawezi kukwepa kashfa ya Dowans ambayo sasa serikali inalazimika kuilipa mabilioni ya shilingi wakati maisha ya wananchi yakiwa duni. Dowans ndiyo ilirithi mikoba yaRichmond ambayo ilibebwa na Baraza la Mawaziri chini ya Rais Kikwete na kupewa mradi wa kufua umeme wa dharura huku wakijua kuwa haikuwa na uwezo huo.
"Sisi RAAWU tunashawishika kuamini kwamba Rais Kikwete ameshiriki moja kwa moja katika mkataba wa Dowans, ndiyo maana ameshindwa kuueleza umma juu ya kampuni hii. Inaonekana hapa kuna mchezo mchafu unafanywa na viongozi wetu... haiwezekani serikali inatangaza kulipa mabilioni ya fedha bila Bunge na Baraza la Mawaziri kuridhia" alisema Mwendwa.
Aidha, Mwendwa alimmwagia sifa nyingi Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, kwa kukataa Dowans kulipwa mabilioni hayo ya fedha, na kusema: "Waziri Sitta anajua ujanja unaochezwa hapa."
Vile vile, alihoji sababu ya serikali kuendelea kuilipa kampuni ya IPTL, huku ikilisukumia mzigo Shirika la Ugavi wa Umeme (TANESCO) lilipe fedha hizo wakati mikataba imesainiwa na serikali.
Alisema IGP Mwema na Waziri Nahodha wameonekana kushindwa kuwatumikia Watanzania, ndiyo maana idara zao zimeanza kutumia nguvu kwa kuua raia wasiokuwa na hatia.
"Polisi haina mamlaka ya kupiga risasi na kuua wananchi wanaoandamana kwa amani, tena hawana silaha wala hawajafanya fujo. Kwa maana hiyo, tunataka Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na IGP Mwema waachie madaraka yao haraka sana" alisema.



Makamba na tambwe hiza watakuja hapa kumsemea bosi wao sasahivi, kwamba hao RAAWU wametumwa na Chadema.

Mwaka huu tutashuhudia sinema nyingi kweli kweli.
 
CHAMA cha Wafanyakazi wa Taasisi ya Elimu ya Juu, Sayansi, Teknolojia, Habari na Utafiti nchini (RAAWU), mkoani Mwanza kimewataka Rais Jakaya Kikwete na Waziri wa Mambo ya Ndani Shamsi Vuai Nahodha waachie ngazi mara moja kutokana na kashfa ya Dowans na vurugu zilizosababisha maafa na vifo vya raia mkoani Arusha.

Huu ni mwanzo wa vuguvugu la Bunge kupiga kura ya kukosa imani na JK na serikali yake ya kifisadi...................
 
Huu ni mwanzo wa vuguvugu la Bunge kupiga kura ya kukosa imani na JK na serikali yake ya kifisadi...................

100% correct.
Lakini inabidi hoja hii ipewe msukumo zaidi kwani kuna watu wanasema eti JK impeachment ni mission impossible....tayari kuna thread inaongelea hili.

Sijui kwa nini watu hatutaki kufikiria nje ya kisanduku (outside te box)?

Mimi nadhani kuna haja ya ku-mobilize wabunge wapato 20% ya bunge lote (kwa mujibu wa katiba) wawasilishe motion ya impeachment and then we move from there.
 
Mhh Jamani, katika historia ya Taifa hili,sijawahi kuona uongozi uliopo madarakani ukipingwa kila kona ya nchi na watu wa aina zote. Kwa kweli hapa kuna walakini.
 
Mhh Jamani, katika historia ya Taifa hili,sijawahi kuona uongozi uliopo madarakani ukipingwa kila kona ya nchi na watu wa aina zote. Kwa kweli hapa kuna walakini.

Huu ndo wa kwanza. Jiulize mkapa aliingia kwa asilimia ngapi awamu ya kwanza na alitoka na asilimia ngapi awamu ya pili.
Maana yangu hapa watu hawamkumpenda mwanzo ila utendaji wake ulimpa credit ya kutosha hata watu kutamani katiba itenguke mkuu aweke mambo sawa kidogo.

Kiukweli Mkwere kachemka, na nchi imemshjinda sema anang'ang'ania na kutaka kufa kiume.

Hapa hakuna mchawi, atekeleze majukumu yake uone kama kutatokea tatizo. Kama atatekeleza kwa kuwapa watu stahiki zote na kutekeleza wajibu wake kiusawia then tuone kama mawazo haya yatatokea. Yakitokea kweli tutajua uko walakini
 
Na mimi naunga mkono hao watanzania wa mwanza, JK ajiuzuru kwa kutuingiza kwenye matatizo watanzania. Ni maafa kuichagua ccm tena, hayo ndo matokeo yameanzia Downs, Nauli za dala dala na mabasi, mfumko wa bei nk. sijui kwa nini hawajaachapisha noti za 50000 na 100000.
 

Alisema IGP Mwema na Waziri Nahodha wameonekana kushindwa kuwatumikia Watanzania, ndiyo maana idara zao zimeanza kutumia nguvu kwa kuua raia wasiokuwa na hatia.
"Polisi haina mamlaka ya kupiga risasi na kuua wananchi wanaoandamana kwa amani, tena hawana silaha wala hawajafanya fujo. Kwa maana hiyo, tunataka Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na IGP Mwema waachie madaraka yao haraka sana" alisema.


Ni kuwa wanataka kumthibitishia JK kuwa pamoja na vijana wao i mean Jeshi la police kutomchagua JK kwenye Uchaguzi uliopita kwa asilimia kubwa bado wanampenda labda ila huu tunajua ni uhuni wa kutaka kuvunja imani kuwa wanajeshi walimchagua JK, Sie twajua ukweli 75% ya majeshi yote kwa wale waliopiga kura walimchagua Dr. Slaa na liko wazi nasikia Juzi katika maandamano huko Arusha maeneo ya Philips lilipita gari la Jeshi JWTZ na wakanyoosha vidole viwili kwa ishara ya chadema na Police wa kawaida hawa wa IGP mwema hawakufanya lolote na wakapita bila kuguswa

 
sio mwanza tu hata mimi.hope watanzania wote pia wanataka iwe hivyo
 
HUYU MKWERE AJIUZULU!!!!

ametuletea matatizo mengi sana.
udini
dowans
mgao wa umeme
mfumuko wa bei
ufisadi na kuwalinda mafisadi
migomo vyuo vikuu (shemeji )
trl kufa
atcl kufa
huduma mbovu za afya
kushindwa kuajiri walimu
kuua raia kwa amri za kisiasa
 
Na mimi naunga mkono hao watanzania wa mwanza, JK ajiuzuru kwa kutuingiza kwenye matatizo watanzania. Ni maafa kuichagua ccm tena, hayo ndo matokeo yameanzia Downs, Nauli za dala dala na mabasi, mfumko wa bei nk. sijui kwa nini hawajaachapisha noti za 50000 na 100000.

Duh! Mkuu noti za laki moja? Kuna watu watapokea noti mbili tu mwisho wa mwezi. Hatari!!!!
 
wala jk hatasema lolote wapo wengi watajibu ni kweli mkuu. ongeza hapo na salva Rweyemamu
 
kikwete hawezi kujiuzulu hata wangekufa watu mia mbili, ccm ni hatari sana.
 
Back
Top Bottom