**Mwanza City Gallery**

"nene na humoragah, natenamhayo, nalelya nembe ja kukaranga duhu elelo!!! :) :) :D "


Bagoshaaa, basumba batale na baanike, banamhala na baniisale, mamihayo matale gete genago, mashikolo mageni gete gete, nembe jenijo jisoga higulya, kwita ndonu nonu kohaya mibula nolo manumbu gete gete...
 
MZA, ndio mji ninaotegemea kutumia uhai wangu wa mwisho nikisha staafu.
 
Aisee unaweza kuweka na picha za wilaya ya Magu. Ahsante sana kwa hizi picha.
 
Buswelu, hivyo ndo viwanja vya gofu jk alivyoshauri alipokuwa mapumzikoni mwanza, viko fukwe za luchelele, pia kuna resort ya night support ni us$800ppn tu unaweza tembelea siku moja, kama sikosei tiger wood na wenzie watakuwa hapo mwakani.

Hapo alipopumzika mdosi nafikiri ni kamanga ferry hiyo ni public beach kama ilivyo koko beach, ila ukitupa ovyo chupa la dasani mgambo wa jiji anakomaa nawewe.

Haya nimatunda ya mh.ole njolaay na mh.Kabwe.

Thanks eddy...lakini almost picha zote unaziona hapo za beach ni Maganga beach iliyoko Nyegezi...not yet kufunguliwa...kwa sasa....ila unaweza kwenda kupunga upepo na kupiga picha...kama wataka kukaa ukp waenda na vinywaji vyako....the lest ni NSSF Tower,PPF na sio NSSF hotel...kama mmoja wa wachangiaji walivyo sema.Let meet in mwanza by 20 august 2008 i will be there.

Stay online.
 
Kha umenikumbusha home sana, hasa mitaa ya nyakato sokoni, national. gedeli primary school mpaka Buswelu secondary nilikopandishia vidato vyangu vinne. Nasikia siku hizi imekuwa shule ya serikali.
Nitafurahi kama nitapata picha hizo.
Jiji limekuwa kweli na linapendeza.
Aaahh mwanza inogile kwa kweli.
 
Kha umenikumbusha home sana, hasa mitaa ya nyakato sokoni, national. gedeli primary school mpaka Buswelu secondary nilikopandishia vidato vyangu vinne. Nasikia siku hizi imekuwa shule ya serikali.
Nitafurahi kama nitapata picha hizo.
Jiji limekuwa kweli na linapendeza.
Aaahh mwanza inogile kwa kweli.

Mimi nina picha za buswelu secondary,zebwela,mpaka makao makuu yanako jegwa ya wilaya ya elemela...confort kwa sasa dara dara zinafika uko...na kuna nyumba watu wamejenga asikwambie mtu wangu.

tatizo sijuji namna ya kuweka picha hapa JF...ningeweza nigesha weka zamani.

Stay online
 
Jamani wakuu mwenye za Arusha (Geneva Of Africa) atuwekee.By,the way tunashukuru sana kwa mkuu aliyeweka hizi photo
 
Bagoshaaa, basumba batale na baanike, banamhala na baniisale, mamihayo matale gete genago, mashikolo mageni gete gete, nembe jenijo jisoga higulya, kwita ndonu nonu kohaya mibula nolo manumbu gete gete...

bhe bhe kinehe
kwani akanzera kakoja nela ,kitangiri na kona ya Bwiru nako kale salama ? gete gete?
 
...mie ningetaka aniwekee picha ya makoroboi, mlango mmoja, kwa mbita, picha ya kwa "ayubu mishkaki wala" pale mitaa ya liberty, sokoni, stendi ya basi, nyamagana, kwa 'geji' pale unapokula pantoni kwenda kamanga, mwaloni kule kilumba na picha moja ya mkara msukuma toroli.


makoroboi ilifutwa siku nyingi miaka 1998 na kilumba mwaloni nayo walejenga soko nzuri kabisa ,mwaloni ya wakati ule haipo tena,sehemu nyingi ulizotaja zilifutwa siku nyingi labda kamanga nadhani ndio ipo ila nayo walikua na mpango wa kuihamisha kwa sasa sijui.
 
mwanza...!mwanza..! si mnakumbuka song la FID Q....yah mwanza for real is great!!

ni mji ambao unapaswa upangwe kimakini sana...nisinge penda kusikia bomoa bomoa inapita kwa sababu ya uzembe wa kufatilia mpango mji so jamaa wawe makini!!!

people wanaojazana dar waanze kufikiria kwenda kwenye miji kama hii na kujenga nchi!!

mji wa sato na sangara.....ngome....utajiri wa dhahabu na almasi.....ooh mwanza!
 
Congrats mkuu Kibunango........ Kuna kitu kimoja ambacho sipendi kitokee Mwanza kama ilivyotkea Dar. Within two years Mza kutakuwa na foleni za kufa mtu. Sijui authorities wanalishughulikiaje hili. Kingine ni Mza kupreserve maeneo makubwa ya wazi kama kule Igoma ukiingia ndani kidogo. Pia hiyo industrial area chini ya Igogo na Igogo yenyewe zinatakiwa ziwe future extensions za City of Mza reson ni kwamba majengo mengi around pale ni serikali na TRC hivyo kuhamisha mbinde yake haitakuwa kubwa sana. Ishu nyingine ni trafic lights hili ofcourse ni tatizo la kitaifa. Nakumbuka kuna mshikaji mmoja muOZ alinibishia na kutaka hata kubet pale nilipomwambia najua idadi yote ya traficc lights Tanzania na locatons zilipo.

Otherwise Mwanza stand to be a great city and therefore a place to live.........

kaumbea kidogo mkuu kibunango: Hivi kwanini mza vijana wote wanaohudhuria kwenye starehe wanajuana to an extent ukinyuti kawekend kamoja watu wanajua umesafiri
 
kaumbea kidogo mkuu kibunango: Hivi kwanini mza vijana wote wanaohudhuria kwenye starehe wanajuana to an extent ukinyuti kawekend kamoja watu wanajua umesafiri
Hii ni kweli, nahisi ni kutokana na kushibana kwa vijana wengi jijini humo!
 
Binafsi ningependa yafuatayo:-

1. Mwanza ingekuwa imepewa hadhi ya makao makuu ya EAC, tungeweza kumeza/uiua miji ya Kisumu na Entebbe kwa Urahisi kwa manufaa ya Mwanza, kichumi etc... na kwa kweli Mwanza ndio centre ye nchi zote za EAC... na Mwanza airport ingekuwa airpot kubwa ya Kimataifa kuliko zote EAC.

2. Baada ya Dodoma kuwa makao makuu ya Bunge... na Makao makuu ya kusita sita ya Serikali kuu... na Makao makuu halisi ya Local Government... ingekuwa busara Mwanza kuwa makao makuu ya Judiciary... (Mahakama Kuu)....

Naomba kutoa hoja.
 
Woh! hiyo picha ya kwanza ni hotel ya nssf, hapa nssf nimewavulia kofia! zamani hapa lilikuwa josho la mbwa, kuna watu waliandamana hadi kwa RC wakipinga kuondolewa kwa josho hilo eti mbwa wao watapata ukurutu.

picha ya tatu ni shopers plaza ya ppf, hili jengo lina car park ya gorofa tano ukitaka kudrive hadi juu sawa au vipi unalipandisha kwa lift maalumu. nyuma yake kuna ka libraly koko, nadhani katafutiwe sehemu nyingine tulivu.

funiko itakuwa hiyo hotel ya moil inayotegemewa kujengwa pale uwanja wa nyamagana. Hotel hii itakuwa na hadhi ya nyota tano na vyumba 300. viwanja vya long tenis, busket ball, budminton, squash na gim. kwa ujumla indoor games zote zitakuwepo. Sio Movenpik kama wewe sio mlevi utaboreka zaidi ya vinywaji hakuna cha ziada.

Hiyo picha ya pili niwafanyakazi wa budege sijui hii kampuni ni ya kinjeketile, angekuwa mwingine angekwisha fukuzwa siku nyingi.

mwanza airport itakuwa international airport sio muda mrefu, ndo itakuwa mwisho wa ATC kwenda mwanza kwani abiria wengi niwafanyabiashara wanaokwenda zao Dubai na hongkong.
Mkuu hio hotel ya Moil iliishia wapi?
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom