Mwangaza

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,316
33,112
Naanza yangu qauli
Kwa jina lake Jalali
Alomleta Rasuli
Kuiongoa duniya

2

Reh'ema zake A'zizi
Zishuke kwa Mwokozi
Kipenzi chake Mwenyezi
Na Aali zake jamiya

3

Na S'ahaba zake bora
Wenye nyoyo za imara
Walo kwetu ni ishara
Kama nyota samawiya

4

Tukisha Mola h'imidi
Na kus'alia
H'amadi
Tutaje ya
Maulidi
Ya maisha ya Nabiya

5

Ulimwengu uli kiza
Hauoni muwangaza
Kila jema wapuuza
Maovu wakakamiya

6

Fikira zilichafuka
Na nyoyo zilitibuka
Ya kweli yalifichika
Urongo ukaeneya

7

Ulitoweka muruwa
Wabora
wajishauwa
H'ata Mola azuliwa
Kuzaliwa na Mariya

8

Mapadiri na kuhani
Walijijenga yaqini
Ni nani huyo ni nani
Muweza wa kuzuiya

9

Walijipa utukufu
Reh'ema kuzis'arifu
(Ewe mja mpungufu)
Na dhambi kughufiriya

10

Nako huko A'rabuni
Kufuru yatia
kani
Ndiyo nyumba ya Shet'ani
Ndiko aliko hamiya

11

Kaa'ba yake Karimu
Alojenga Burahimu
Ikajazwa masanamu
Zaidi thalatha miya

12

Na kiza kilipo kaza
Alitengeza Muweza
Kuuleta mwangaza
Kwa kuzaliwa Nabiya

13

Na mwaka tawambiani
Alo zaliwa
Amini
Mia tano sabii'ni
Na moja wa shamsiya

14

Ni mwezi Mfungo Sita
Qarini zilizo pita
Ulimwengu ulipata
Mtume kumpokeya

15

Mwezi huu mtukufu
Alizaliwa Sharifu
Mjiwe mtakatifu
Maka nchi H'ijaziya

16

Kazaliwa Muungwana
Na
mamiye Bi Amina
Na
babiye wetu Bwana
Alisha mtanguliya

17

Akatunzwa na babuye
Na khalafu na a'miye
Na walo mlea yeye
Baraka na Saa'diya

18

Na huyo Mwana Baraka
Ni mama Muafirika
Na Saa'diya
pulika
Ni
H'alima A'rabiya
MAFUNZO
Tunalo jifunza katika mlango huu ni kuwa upotovu ukizidi mno ndio huja uwongofu. Waingereza husema: "The darkest hours are just before dawn". Saa za kiza kabisa ni zile za karibu mno na alfajiri. Ndio Muhammad s.a.w. kazaliwa kwa wakati wake. Nasi tutaraji faraji dhiki zinapo shtadi.
 
Back
Top Bottom