lutayega
JF-Expert Member
- Feb 29, 2012
- 1,288
- 552
Naandika habari hii nikiwa na masikitiko yaliyochanganyikana na hasira zilizopitiliza.Leo asubuhi baada ya kupata kifungua kinywa, nilanza kujiandaa kufua nguo zangu kama mnavyojua leo siku ya mapumziko, mara akatokea binti mmoja akiwa kabeba mtoto kama wa miaka 2 hivi. Nikamkaribisha na baada ya kusalimiana akaniuliza kamaanaweza kupata kazi yoyote ile, kabla sijamjibu nikaona anaishiwa nguvu akakaa chini ili kuepuka kuanguka. Ikabidi nimuulize kama anatatizo lolote lile la afya, akanijibu kuwa hajala toka janamchana, pia ikanibidi kumuuliza mtoto aliyembeba ni wa nani akanijibu kuwa ni mtoto wakekiukweli sikumwamini mpaka nilipoona anamnyonyesha kwasababu huyu binti kama ana umri mkubwa ni miaka 13. Ilibidi nimpatie chakula ili kupunguza njaana baada ya kula niliamua kumpatia kazi ya kufua nguo nilizokuwa nataka kuzifuaalipokuwa anafua alimuweka mtoto wake chini, mtotot huyo nipomwangalia alikuwa na upeleupelemwili mzima nikamuuliza mtoto wake anaumwa nini akanijibu kuwa mtoto anaumwa kaswende ambayo alizaliwa nayo, ndo akaanza kunisimulia kuwa akiwa ana miaka 9 kuna baba wa miaka kama 50alimwomba wawe na mahusiano ya mapenzi kwa makubaliano kuwa atamnunulia simu na cherehani pia atamwoa, hivyo binti alianza kumpa penzi huyo babu. Walidumu katika mahusiano hayo kwa mda wa miaka 2.Akiwa na miaka 12 alishika mimba na alivyomweleza huyo baba huyobaba aliikataa mimba na kuwambia kuwaakiendelea kumfuatilia au kumwambia mtu atamchinja. Baada ya wazazi wake kugundua kuwa ni mjamzito walimuuliza nani mhusika kwanza aligoma kuwambia lakini baada ya kupigwa na kulazwa juu ya mti kwa muda wa siku mbili aliamua kuwaeleza ukweli nao waliamua kumshitaki mhusika kwa mtendaji wa kijiji. Mhusika baada ya kuona anafuatiliwa alitoroka. Yule binti naye alifukuzwa kwao na mpaka anaponisimulia kisa hiki hana pakuishi na chakula chake ni pale anposaidiwa na wasamalia, pia mtoto wake anaumwa kaswende yeye kwa upande wake hafahamu kama ana kaswende au la.Kinachonitia hasira zaidi ni kwamba huyu baba aliyempa mimba ameshatoka mafichoni na hajachukuliwa hatua yoyotena hatoi huduma yoyote kwa huyu binti na kwa mtoto wake.Kutokana na hilo naomba msaada wa mawazo, wa kimatibabu na wa kisheria kumsaidia huyu binti. Nimemwambia aje jumamosi ijayoili niweze kumsaidia