Mwanaume Hana Moods

Samahani kwa kuchakachua sredi.........

Naomba kukuuliza DA na MJ1

Hiyo mood mnayozungumzia hapa iko kwenye kikojoleo cha mme wake Dena au kwenye wallet?
Hahahahah nilijua tu unakoelekea ! Hapa naomba nimwchie mwenye ngoma akujibu maana nilivyoivalia njuga utadhani yangu kumbe yangu ilishasahaulika hata mirindimo yake hahahah
Aksante babu kwa kunizima kisebu sebu changu.

We Dena haya mjibu Babu mkubwa hapa.
 
Dah nimeshajaribu hayo mambo lakini wapi tena nikutumia watoto ndo balaa anawaambia ndo mama yenu kawatuma sio..........

dena kila jambo lina chanzo na kama tatizo lipo basi linaweza kutatulika tu .. je mkate wa bwana si anakupatia (haki ya msingi) au nayo kasitisha?? kama anawaingiza watoto basi suala hilo bado liko kwenye mikono yako katika maamuzi ..
 
dena kila jambo lina chanzo na kama tatizo lipo basi linaweza kutatulika tu .. je mkate wa bwana si anakupatia (haki ya msingi) au nayo kasitisha?? kama anawaingiza watoto basi suala hilo bado liko kwenye mikono yako katika maamuzi ..

Ndo maana nikaja hapa si unaona ushauri naoupata sasa sante sana bana
 
Hahahahah nilijua tu unakoelekea ! Hapa naomba nimwchie mwenye ngoma akujibu maana nilivyoivalia njuga utadhani yangu kumbe yangu ilishasahaulika hata mirindimo yake hahahah
Aksante babu kwa kunizima kisebu sebu changu.

We Dena haya mjibu Babu mkubwa hapa.

Nimeshamjibu DHL wamekufikishia mzigo wakoooo????
 
Hahahahah nilijua tu unakoelekea ! Hapa naomba nimwchie mwenye ngoma akujibu maana nilivyoivalia njuga utadhani yangu kumbe yangu ilishasahaulika hata mirindimo yake hahahah
Aksante babu kwa kunizima kisebu sebu changu.

We Dena haya mjibu Babu mkubwa hapa.
Dena ukuye ujibu hapa........

Mood ya mume yako ilopotea ni ipi?

Mood ya kwenye kimwaga mikojo chake
Au
Mood ya kimwaga noti chake?
 
Dear umesahau kuwa simba akizidiwa anakula majani my dear????

3 weeks na hakuna dalili ya kujirudi? mie hata sielewi, au kuna k2 ulimfanyi kikamkwaza/mlikuwa na malumbano/au manaume kaamka 2 asubuhi kakuna(gubu) etc..kuna k2 umechangia kwenye huu mnuno au amejiamua (katibuka kwningie kaja kumalizia kwako)...coz hata sielewi naona mchenga sasa, naongelea k2 cjui undani wake, pa1 na yote mchuno wa 3 weeks? tena mwanaume...ote ndao!
 
Mama wa Kwanza we acha tuuuu ni muda kama wiki tatu hivi

Week tatu ni nyingi sana .......Mama tafuta muafaka ili ujue tatizo ...Vunja ukimya na omba kuongea nae ila aseme nini kinamsumbua .
Inaumiza sana mtu kukaa kimya bila kutoa sababu inayomsumbua ..matokeo yake mtu unakuwa na labda labda kibao...
Da napata picha iliwahi kunitokea sisemeshwi week ya kwanza na mie nikakaa kimya kabisa wala kugutuka week ya pili......
Matokeo yake nikaambiwa nina kiburi ..jamaa akaanza mwenyewe akipita nilipokaa analalamika ndoa kama ndo hivi lol mie kimya..
Mwisho wa siku niliona haya sio maisha tukaongea yakaisha.....
 
Hahahaha hommie unaharibu bana
Kwa mfano unataka kunambia nlikuwa nataka kumpeleka Dena kwenye angle ipi na kwenye gesti ipi?
ODM ngoja tusichakachue siridi ya mpendwa Dena, ila gsti ni ile yenye magodoro ya Comfy!
 
Edson acha tu mambo haya nitakwambia tukionana


NGOJA NIJARIBU KUSAIDIA KABLA HATUJAKUTANA

mwanaume kununa kunatokana na sababu nyingi ambazo zinaweza kukuumiza sana hasa ukizingatia kuwa jambo lenyewe linazungumzika....lakini kama mwenzi wako hataki kushaurika au hata akishaurika anabadilika kwa mda kisha akikwazika anarudi kule kule hii itakuletea shida sana baadae maana taratibu utaanza kudevelop tabia zenye muonekani hasi kwake maana madhara yake yatakuwa yameingia sana na kukusumbua akilini....mojawapo ya matatiozo ni yale ya kisaikolojia kama yafuatayo:

1 Insomnia.....kwa kuwa mwenzi wako ni mtu wa kununa na habadiriki kitabisa itakusababishia wewe kuwa unakosa usiku usingizi...kichwani yatakuja maswali meeeengi bila majibu yanakuja na kutoka hadi inafikia alfajiri saa kumi au kumi na moja ndo unapata usingizi lakini kabla hujalala vizuri kumekuccha na itabidi uende job na hatime ufanisi wa kazi hushuka..hali hii taratibu itakufanya kama ikiendelea kwa mda mrefu itafika mahali utamchukia mwenzi wako na kumuona kama mtu aliyekupotezea mda na anakutesa bila chuki..


2 Bulimia...hali hii ni pale msongo wa mawazo unapokuwa mkubwa katika kutafuta suluhisho la matatizo yanayakukabili inafikia mda unakosa hamu ya kula kabisa...hata ukila mda si mrefu utasikia njaa na mbaya zaidi mnapokuwa na mwenzi wako halafu hamjasuluhisha matatizo halafu mnakula pamoja hakika inaumiza na unaweza kukwepa usikae nae wala kula nae au ukamtegea kula....

3.Stockholm syndrome...hii ni ile hali ya kumchukia mtu lakini huna jinsi ila unaendela kuwa nae...hutawajibika ipasavyo kwa mume wako/mwenzi wako hata ukiwajibika ni kwa shingo upande sana maana hakuna mawasilaino thabiti kati enu ..yaani ni sawa na wewe hapo dena utekwe nyara then mtekaji akujengee mazingira ya kumwanini na kumuona ni mtu asiyena matatizo na watu wakikuuliza..dena vipi mtekaji wako anaweza kukuachia uwe huru? wewe unaweza kusema ni mtu mzuri na hatuna shida tunaishi vizuri.wakati ndani kunawaka mateso hii ndio stokholm syndrome

4.anorexia ...kwa kuwa kwa mda mrfu umetafuta suluhu ya matatizo ya mwezi wako bila mafanikio na huishi kwa raha na amani basi mwili wako utaanza kubadili na hata kupata magonjwa presha, kisukari, madonda ya tumbo nk ...na wakati mweingine usijue chanzo chake ni nini kumbe ni hayo matatizo...na mwisho mtu hufa kifo cha huruma (eutanesia death)


dena dada yangu mwili mmoja hauji kwa kusimama mbele ya shehe au padre na akitamka kuwa ninyi ni mwili mmoja ule mwili huwa hauji mble ya watumishi wa mungu..ili kuufikia mwili mmoja ni process ndefu sana inaanza kabla ya uchumba na inakamilika baada ya miaka mingi huko mbele mkiwa ndani ya ndoa.....dena jaribu na endelea kuutafuta mwili mmoja dada...

katika hii shida iliyokukumba nakushauri kaa na huyo mwenza wako muulize kwa utaratibu natafuta suluhu ya kudumu kabisa ili tatizo hili liishe....maana asili ya matatizo haya kama yasipopatiwa tiba mapema huchukua mda mrefu kuisha lakini hata yakiisha huwa yanaacha maovu na wakti mwingine kuvunjia kwa uhusiano.....mengine umesema tukikutana tutaongea laki kumbuka mambo matatu yanayovunja uhusiano ni :

a: mawasiliano

b: pesa

c: mapenzi

hilo kwanza ndilo linalokusumbueni wewe na mwenza wako
 
mpeleke akafanyiwe maombi atakuwa mpya kama zamani,atakuwa na mapepo bila yeye mwenyewe kujijuwa,maana moods huwa zinaisha sasa zake zp zisizoisha jaman,
 
dena nadhani kuna jambo ambalo linaweza kuwa linamsumbua au kumsuta hivyo anashindwa kujiamini na kuongea na wewe.. mara wanaume kuna maaamuzi wanaweza kuyafanya nje ya mipango yake na mkewe na akajikuta amepata hasara au ameharibu sasa anakosa ujasiri wa kukuelewesha hivyo anakuwa na hasira na tabia za ajabu ajabu kama ukaidi na kiburi.

cha kufanya, kuna mambo au vitu ambavyo huwa vinamfanya awe na furaha jaribu kumfanyia kama chakula au movie au vipindi kwenye TV.. naamini kwa muda ulioishi nae utakuwa unamwelewa ni wakati gani ana furaha , huzuni, mawazo, nk .. hivyo nenda nae taratibu maana anaweza akakugeuzia wewe kibao kama ndo tatizo

dena jambo jingine inawezekana kuna jambo ambalo unamkera au linafanyika hapo nyumbani na anashindwa aanzeje kulisema labda linaweza kukukera au likaleta kutokuelewana zaidi hivyo anajenga chuki juu yako.. cha kufanya kama nawe unaogopa kukaa nae na kuongea tumia watoto au unaweza kupanga out moja kwa ajili ya mazungumzo nje ya nyumbani .. but usimweleze yeye anakukosea nini ila jaribu kumwelezea malengo na maisha ya mbele au kuwa na plan fulani ambayo ataona ni ya maendeleo kwake

samahanini wandugu hapo juu hivi mtu wa kufanyiwa yote hayo ana umri gani? chini ya miaka 25 au?


na wewe unaendeleaga 2 kumbembeleza na ku2ma watoto?
Ajabu lol
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom