Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Habari wajameni.
Nina dadangu kaolewa na wana watoto 2, mumewe yuko kamili tu, I mean viungo vyake havina tatizo. Shule kasoma, sio sana lakini kutokusoma sio sababu ya haya afanyayo.
Kila siku yeye hana hela anampatia mkewe 10,000 kwa mwezi na kila siku anataka chakula. sister kipato chake kidogo sana, lakini yeye ndo anahudumia familia including huyo mume wake. Ajabu jamaa pombe hanywi wala sigara havuti ila kila siku hana hela na 10,000 kwa mwezi anatoa. Kila siku asubuhi anatokaga, hasemi wapi anaenda, ila jioni hurudi home na akiombwa hela yeote, iwe ya umeme, maji yeye hana. Sister mpole sana ila anaumia mno na kukoromeana nae hawezi. Last week \ mtoto wao kagundulika ana pumu, jamaa anadai hana hela, ivi ni kweli?
Kaniomba ushauri, nami naomba niwashirikishe humu jamvini mnishaurije?