Mwanasiasa gani Tanzania mwenye mvuto namna hii?

Wewe kuwa mwangalifu hapo kwenye red! Hiyo PH. D unayoshadidia mbona magumashi tuu? Au unajifanya kipofu!
PH. D inafanywa baada ya vi-certificates tuu?, hamna Bachelor wala Masters uliona wapi? Hicho chuo kilicho mpa hiyo PH. D sidhani kama kinatambuliwa na bodi huru! Labda papa peke yake!
Kwa nini usiombe paper alizoandika, ili ujue PhD inapatikana vipi? Au umwulize rafiki yako mwenye hiyo PhD
 
Umenena ukweli tupu, Dr wa kweli Slaa anamvuto sana kwa sasa na hakuna mwanasiasa mwingine kwa hapa Tanganyika anayeweza fananishwa nae, sifa za Dr Phd ni:
Mpole,
Mnyenyekevu,
mtulivu,
mkweli,
mpenda watu,
anaufahamu mkubwa,
anaona mbali,
anauchungu wa kweli na nchi yake,
hana makundi
hajivuni
haogopi
hapendi mafisadi na wahujumu uchumi wa nchi
na nyingine nyingi zinazofanana na hizo.

sasa watanzania tutaulizwa siku moja niliwaletea kiongozi awezaye kuwatoa katika ndimbwi la matatizo yenu nanyi hamkuona sasa mnataka nini?

nasi tutakuwa hatuna cha kujibu? bali kusutwa na watoto au hata wajukuu wetu.

Dr Phd Slaa ndie kiongozi wa kweli wa Tanzania ya sasa.

tulimuona.tukatumia haki yetu ya msingi kumchagua!masikini sisi wakachakachua kura hakutangazwa kama mshindi!wakatupa mtu asiyeweza kuongoza hata familia yake!kazi kuchekacheka.kutalii na kulipa fadhila
 
Kwa nini usiombe paper alizoandika, ili ujue PhD inapatikana vipi? Au umwulize rafiki yako mwenye hiyo PhD

Wewe hiyo ndiyo official CV yake aliyopeleka bungeni! Hamna paper nyingine alizoandika! labda unataka kumuandikia!
 
Tuangalie hizi picha kisha tujifariji kama mrema vile akikumbukia alivyokuwa anasukumwa kwenye gari, kwa kweli wabongo wasanii, kumnanga mzee wa watu walitaka kumuuwa kwa presha? ndio maana kawa kichaa siku hizi anauawa ma RC.
sahau huyu sio mrema na watanzania wa sasa sio walee wa enzi ya mrema na kuhusu ukichaa nafikiri yule anayelalamika nchi imemshinda ndiye anastahili cheo hicho cha uchizi
 
Mwanasiasa gani Tanzania anayeweza kuvutia umati mkubwa namna hii bila watu hao kuhongwa? Mimi nakumbuka nilikuwa Jamhuri stadium Dodoma mwaka 1989 au 1990 Nyerere akiagwa alipoamua kuachia uenyekiti wa chama na wakati alipohutubia baada ya Madiba kutoka gerezani. Sijaona nyingine tena kama hii.

71598_457101522471_823957471_5395767_2365798_n.jpg

Mimi ilikua Mbeya (MEI MOSI) Mwaka 1995 alikua Marehemu Baaba wa Taifa (Mwal) JK Nyerere Mbeya ilifurika saaana cha kushangaza baadae alikuja Mh. Mkapa watu walijaa but si kama Kwa mwalimu.

VIVA Mwalimu Legacy, Viva CDM, VIVA DR Wa ukweli!
 
sahau huyu sio mrema na watanzania wa sasa sio walee wa enzi ya mrema na kuhusu ukichaa nafikiri yule anayelalamika nchi imemshinda ndiye anastahili cheo hicho cha uchizi

sioni kilicho badilika, yaani kundi lote hilo kaishia kushindana na kina Spunda, na Kuga kwenye kura? vipi viatu mtamchangia?
 
Halafu hawa walemavu wanakuja Maelezo kutoa kauli za kipuuzi eti wanaogopa machafuko. Watulie tu maana hakuna mwenye shida nao. Wana changamoto za kutosha hivyo wasubiri tu neema toka kwa wateule kama CDM

Hujafa hujaumbika ndugu yangu.

Other wise mchango wako uko poa.
 
Wewe kuwa mwangalifu hapo kwenye red! Hiyo PH. D unayoshadidia mbona magumashi tuu? Au unajifanya kipofu!
PH. D inafanywa baada ya vi-certificates tuu?, hamna Bachelor wala Masters uliona wapi? Hicho chuo kilicho mpa hiyo PH. D sidhani kama kinatambuliwa na bodi huru! Labda papa peke yake!

========================================================

EDUCATION
International Eye H. Centre Certificate in Eye Health 1993-1993

TransWorld Tutorial College, London Certificate in Management 1985-1985

St. Thomas Aquinas University Advanced Diploma in Rural Development 1980-1981

St. Urban University, Rome PhD (JCD) Law 1977-1981 [Doctor of Canon Law (Latin: Juris Canonici Doctor or JCD)]

Kipalapala Seminary Certificate in Theology 1974-1977
Kibosho Seminary School Certificate in Philosophy 1972-1973

Itaga Seminary School A-Level Education 1970-1971
Dung'unyi Seminary School O-Level Education 1966-1969

Karatu Primary School Primary Education 1962-1965
Daudi Primary School Primary Education 1961-1961
Kwermusl Primary School (Mbulu) Primary Education 1958-1960

========================================================

heri hata PhD ya kupika lol
lakini siyo ya Kikwete na mwenziye Karume
afadhari hata wangekuwa nayo ile ya kusoma qurani
 
Jesuit hebu tuwekee na education background ya mkwere. Na uwe makini kwenye kupata phd kama ulivyofanya kwa slaa
 
Mjepu ninayemfahamu mimi kama ndo wewe, basi naamini hela ni mwanaharamu, unaweza kukunjwa kidume na ukajisifu. Damn!
 
ni kweli umaarufu huu unatishia usalama wa mafisadi ndio maana matamko kila kukisha .watanzania hawakumchagua kikwete na ccm yake hiyo ni dhahiri

Nan sasa alimchagua Kikwete,achen kutapatapa nyie WATANZANIA HALIS ndo walio mchagua na MH KIKWETE NDO MWENYE MVUTO
 
Jesuit hebu tuwekee na education background ya mkwere. Na uwe makini kwenye kupata phd kama ulivyofanya kwa slaa

Tatizo mkuu, watu humu wanjaribu kuonyesha kwamba PH.D ya Slaa haina doa! ukweli ina magumashi ambayo watu hawako tayari kuyazungumzia! afadhali ya mkwere inajulikana ni ya heshima tuu--hatusikii watu wakisema DR PH.D wa ukweli!
 
Hivi, inapofika wakati wa kupiga kura huu umati najifcha wapi? Au wanaenda tu kumsanifu mzee watu?
 
Hivi, inapofika wakati wa kupiga kura huu umati najifcha wapi? Au wanaenda tu kumsanifu mzee watu?

wengi huwa wanafuata kumuona chizi na kucheka anapokuwa analalamika, kwa kweli hata mimi hunikosi mikutano/matembezi ya CDM.
 
Back
Top Bottom