Mwanasheria mkuu zanzibar apasua jibu kuhusu muungano muda huu

Pamoja na hilo mkuu, pia haitachukua dk watapigana wao kwa wao (wapemba na waunguja). Unajua shida ya zanzibar, wanasiasa (huku wakiweka mbele maslahi yao) wameishapandikiza chuki kwa wananchi wa wakawaida kuhusu muungano. Wameishawajengea too much expectations ambazo watapata pindi muungano ukivunjika. Ukitaka kuamini kinachokisema hapa ongea na wazanzibar wa kawaida, hata wachache tu, utasikia maisha wanayotegemea pindi zanzibar ikibaki peke yake. Yaani wanasiasa wa zanzibar wanawadanganya kweli wazanzibar!!!!

Mi natamani waachie ka-nchi kao, halafu wapemba sijui nani hao wote walioko bara waondoke, waje bara kwa visa. Halafu kila kitu tuwakatie (umeme, mkaa, mchele n.k), tuone kama hawajawa watumwa wa waarabu.

haijalishi, lakini si wako huru, wacheni kuwanga'nga'nia
 
Kwa sababu sisi Bara ndio tunauhitaji, tunaubembeleza huu Muungano. For the life of me I can never figure out why we need that godawful Island. Tunafanya kila kitu kunyenyekea kubembeleza Muungano, hata tukionekana kituko.

attachment.php


We jiulize, kwa nini Mzanzibari akisimama kuuponda Muungano huwa Bara tunamshambulia? Leo Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, juzi Mama Karume kauponda Muungano, wabara wakamshukia kama maporomoko ya Victoria falls, why? Cha ajabu hata hapa JF kwa mfano, hata wale ambao hawataki Muungano, akisimama kiongozi Mzanzibar kuuponda Muungano tunatokwa mapovu, why? Mimi kwa kweli Mzanzibar akipandisha munkari kuiponda Tanganyika mimi huwa nafurahi, kwa sababu mwisho wa siku lake na langu letu moja: hatutaki Muungano.

Let's be perfectly clear, tunadai kila upande, Tanganyika na Zanzibar, kila moja, separately, iwe ni dola huru yenye mamlaka yake kamili.

Taso,

..lakini wanatakiwa wauponde muungano kwasababu za kweli.

..mara waseme muungano ni dhuluma unasababisha ukimwi,madawa ya kulevya, suruali mdebwedo, popo bawa, na kila aina ya uchafu. baadaye wanaibuka wakidai wanataka mkataba, au wanataka "muungano wa uswisi."

..U can not keep up with these ppl.

..Mansour Yussuf Himid anasema anataka kuvunja muungano wakati huohuo hataki kura ya maoni. sasa huyu siyo mbambaishaji kweli??

..mimi ni Mtanganyika na ninaupinga muungano, lakini siko tayari kutumia chuki na majungu kama wanavyofanya Jussa,Ahmed Rajabu,na Uamsho,ktk kuupinga muungano.
 
Kama muungano utavunjika basi TIC inawahusu, maana wana majumba na mashamba kibao upande wa pili (bara). Itakuwa Kama Mayotte ambayo ni Ufaransa iliyo Afrika.
 
Taso,

..lakini wanatakiwa wauponde muungano kwasababu za kweli.

..mara waseme muungano ni dhuluma unasababisha ukimwi,madawa ya kulevya, suruali mdebwedo, popo bawa, na kila aina ya uchafu. baadaye wanaibuka wakidai wanataka mkataba, au wanataka "muungano wa uswisi."

..U can not keep up with these ppl.

..Mansour Yussuf Himid anasema anataka kuvunja muungano wakati huohuo hataki kura ya maoni. sasa huyu siyo mbambaishaji kweli??

..mimi ni Mtanganyika na ninaupinga muungano, lakini siko tayari kutumia chuki na majungu kama wanavyofanya Jussa,Ahmed Rajabu,na Uamsho,ktk kuupinga muungano.

Kila week story inabadilika, mara kupumua, mara mkataba. Lakini kama kweli hawataki muungano kwanini wasiwaambie wabunge wa Zanzibar wasiende Dodoma? Wapitishwe muswada wa kura ya maoni mambo yaishe.

Nakubaliana na wewe kabisa JokaKuu kuhusu kauli za matusi dhidi ya upande mwingine wa muungano. Kama hoja ni kuachana kwanini matusi yote haya?
 
Last edited by a moderator:
Mwanasheria mkuu wa zanzibar asesema ukweli leo kuwa hakuna muungano adai yakuwa muungano upo tu kama kiini macho lakini kiuhalisia muungano haupo hilo kalisema leo katika semina ambayo inaendelea muda huu kwa waheshimiwa wawakilishi wa baraza la mapinduzi zanzibar. Tizameni ZBC ni live muda huu. Baadhi ya waheshimiwa wawakilishi wamekwisha changia ambao ni Raza, Mshimba Vuai Nahodha na Jussa ikihuacha Vuai wengine wanataka kesho watangaze mgogoro wa muunganoBaadhi ya mambo ambayo mwanasheria kazungumzia ni kuhusu ushikishwaji wa upande wa zanzibar katika mambo ya muungano kuwa ni kiini macho, akaunti ya pamoja toka ipitishwe mwaka 1996 hadi leo hakuna account hiyo wala utekelezaji wake, Raisi wa jamuhuru kumteua waziri mkuu bila kushauriana na makamu wa rais, pia kuwateuwa mawaziri bila kushauriana na makamu wa raisi, raisi wa muungano kuwa na kinga ya kutokushtakiwa kwa upande mmoja kwa kuwa mambo ya uhaini sio ya muungano na mengine mengi. Wanajamii Kila mtu kamsifu mwanasheria kwa kusema ukweli jana Mzee Hassani moyo alisema viongozi wa zanzibar miaka ya sasa ni waoga na wako kimaslai zaidi

doors are open, why dont you walk out...? if the path is too narrow, go through the open windows guys!
 
Kila week story inabadilika, mara kupumua, mara mkataba. Lakini kama kweli hawataki muungano kwanini wasiwaambie wabunge wa Zanzibar wasiende Dodoma? Wapitishwe muswada wa kura ya maoni mambo yaishe.

Nakubaliana na wewe kabisa JokaKuu kuhusu kauli za matusi dhidi ya upande mwingine wa muungano. Kama hoja ni kuachana kwanini matusi yote haya?

Iwe ni kwa amani, maelewano, ustaarabu, maridhiano ama kwa chuki, husda, kejeli, dharau na matusi; Muungano uvunjike tu hata leo tupumzike kelele za wazanzibari kila siku kelele za malalamiko tuuuuuuu shit!
Tutengane nao ili tuanze kuwauzia huduma mbalimbali kama umeme, sasahivi wanatumia umeme wetu bure tena hawaguswi na mgao.
 
Last edited by a moderator:
Serikali moja tu ndio Suluhu nchi hii asotaka ajinyonge!
Hii serikali moja ya aina ipi?

Serikali ya shirikisho ? Ambayo itafanya iwepo serikali ya Tanganyika na serikali ya Zanzibar kama serikali za majimbo halafu iwepo serikali ya shirikisho?

Au serikali moja kwa maana ya kuimeza Zanzibar na kuifanya ni sehemu(mkoa, wilaya) ya Tanganyika(Tanzania)? na kufuta dhana ya muungano wa nchi mbili wa baadhi ya mambo?

Rai yangu, turudishe Serikali ya Tanganyika na iendelee kuwepo serikali ya Zanzibar ili tujipe nafasi nzuri ya kupanga na kutafakari kuanzisha serikali ya Shirikisho la Afrika Mashariki.

Ni wazi tutakapofikiria shirikisho la Afrika mashariki hatutapenda serikali zetu zipotee na iwepo mamlaka moja tu, serikali ya Afrika Mashariki.

Tuache unafiki, tuone tatizo na tusijifanye wajanja kwani ujanja mwingi, mbele.......

Muungano wa nchi mbili (unaosemwa ni wa hiari) ambao hauainishi mipaka ya mamlaka ya wadau/wanachama wake kinagaubaga unafikia mahali unagonga ukuta kama huu wetu. Tabia ya wanasiasa wetu kuamini kuwa matumizi ya nguvu kuulinda/ kuulazimisha uwepo muungano inatujengea chuki na itatuletea maafa. Tabia ya wanasiasa wetu kufikiria kuwa kero zitajitatua zenyewe na tabia ya kuendelea kuficha uchafu chini ya zulia imetufikisha hapa tulipo leo.

Muungano wa Tanganyika na Zanzibar(Tanzania)kama ulivyo sasa ni Muungano wa wanasiasa wajanja tu ambao wanatutengenezea bomu hatari. Wanasiasa hawa wamelea kero za muungano kwa miaka 48 na kutoa kauli za kisanii kuwa kero zitatuliwa,zitashughulikiwa, mwaka baada ya mwaka, huku wakiacha kero hizo kuongezeka.

Muungano huu ni kiini macho cha CCM cha kutaka kuendelea kutawala Tanzania. Hata hivyo kama ni wenye kuona mbele na mbali basi wangeelekeza juhudi zao katika kutatua hizo kero za muungano. Tatizo la CCM linaongezeka kwani kuna CCM ya Zanzibar ambayo ina msimamo wa akina Moyo, Raza nk na kuna CCM bara inayoamini katika kuleta serikali moja, Tatizo pia linaongezeka kutokana na kuwepo na sisa za vyama vingi na kila chama kikiwa na sera ya Muungano tofauti. CCM wamebakiwa na njia moja tu, kutumia mabavu/nguvu kuulinda muungano au wakubaliane na uhalisia wa sasa.Watatue kero za muungano.

Kuna wizara maalum ya Muungano(inashughulikia muungano, matatizo ya Muungano, kero za muungano), kazi yake ni nini? Kero ngapi imetatua? au nini kinakwamisha kutatua kero nyenginezo?

kwa bahati kila kitu hapa Tz ni siri. Kama hii wizara ingekuwa inabainisha kero za Muungano zilizopo baina ya Tanganyika(Bara) na Zanzibar na wananchi kuzielewa na vipi zinatatuliwa ingeepusha hizi jazba ambazo wengi wetu tumo tu, bendera kufata upepo.
Kila mtu anakubali kuwa Muungano una kero nyingi na sasa Muungano wenyewe unakuwa ni kero.

Kwa wale washabiki wa serikali moja,nchi moja,taifa moja ningeshauri wangefikiria hii kitu onecountrytwosystems. Nafikiri Zanzibar watapata kupumua kama wanavyodai huku Tanganyika(Tanzania)tunajiandaa kuunda Shirikisho la kisiasa la Afrika Mashariki. Tunu yetu ya kuwa pamoja na ndugu zetu wa EAC katika nchi moja,serikali moja na taifa moja lenye nguvu itapata muda mzuri wa matayarisho ili tusirudie makosa ya muungano wa Tanzania.
 
Huyu anawachezea tu Wazanzibari; kama angekuwa anaamini hakuna Muungano angekuwa wa kwanza kuzuia viongozi wa Muungano kuja Zanzibar na serikali ya Muungano kutoa misaada kila majanga yanapopatikana. Yeye si ndio mwanasheria mkuu? angetakiwa kuweka zuio kwa viongozi wa Muungano kuja Zanzibar na uwepo wa taasisi za Muungano Zanzibar.

Wa kulaumiwa ni Dr. Shein. Kama Shein angekuwa hamlei na siyo mwoga huyo angetakiwa avuliwe hicho cheo ili akajiunge na wanauamsho wenzie kudai serikali ya Zanzibar. It is simple as that.

Al Uamsho katika mihadhara yao (video clips zilitundikwa hapa jana) wanajiapisha KUMLINDA Dr. Ali Mohammed Shein! Hapo unaweza kuunganisha dots!!!
 
Mimi hii mijitu inayotaka muungano na hawa wapemba huwa inanikera sana!! Sasa hapo huyo mwanasheria kakosea nini?
 
Itakuwa chereko chereko na furaha isiyokifani kufufuliwa kwa taifa langu Tanganyika. Inaweza ikawa ndiyo mwisho wa nchi kuongozwa kiswahiliswahili. Mungu tuwezeshe tufike huko waja wako.
 
Muungano ukivunjika utakuwa umechanguiwa kwa asilimia 100 na udhaifu wa viongozi wa CCM na serikali zake period.
Kama unautaka muungano we sepa zako pemba!! Sisi hatuutaki. Hauna faida yoyote kwa watanganyika.
 
Nonda said:
Au serikali moja kwa maana ya kuimeza Zanzibar na kuifanya ni sehemu(mkoa, wilaya) ya Tanganyika(Tanzania)? na kufuta dhana ya muungano wa nchi mbili wa baadhi ya mambo?

Nonda,

..suala la Zanzibar "kumezwa" linatumika tu for political convinience.

..mimi napendekeza serikali moja, nchi moja, dola moja.

..tena ikiwezekana wa-Zanzibari wote wahamie huku Tanganyika na visiwa vya unguja na pemba vibakie vitupu.

..mind you, mwaka 1964 Znz ilikuwa na watu 300,000. leo hii wa-Znz walioko ktk jiji la Dsm wanakadiriwa kuwa 350,000.

..malalamiko ya wa-Znz hayawezi kuisha kwa kuundwa kwa serikali 3, muungano wa mkataba[whatever that means], au muungano wa uswis[we dont have cantons in tg & znz]. kumbuka kwamba haya malalamiko yote ni ya WANASIASA wa ZNZ. wananchi wa Znz wanaoishi Tanganyika wanaishi bila bugudha yoyote ile, wanashiriki kila jambo bila kubaguliwa.

NB:

..tatizo lingine la wa-Znz ni UBAGUZI. kwanini wanazuia wa-Tanganyika kushiriki ktk mitandao kama www.zanzinet.org na www.mzalendo.net?? mbona walikuwepo tanzanet, na leo wapo hapa Jamii forums.
 
Shabash ----- Mwanasheria hakula maneno. Amesema ukweli na ukweli ndio huo. Sasa hawa wanajeshi wenu waliopo huku kwetu waondosheni warudi kwao. Sisi si watu wa fujo wala hatuna haja ya majeshi. Kaeni kwenu tukae kwetu ila mukumbuke kuwa hata hiyo daresalaam ni yetu , tukiitaka tutaichukua. Kwenu ni dododma na Nyerere anajua hilo ndio maana akaupeleka mji mkuu huko. Nyerere anaona mbali. Alikuwa anajuwa wazanzibari watadai chao. sasa tunadai chetu. Hatuutaki muungano. Zanzibar Oyeeeeeee Uhuru oyeeeee. hhahahahahahahahahahahah
Mwisho wa muungano ndio huu tunauona na hamuna hoja ya kimsingi ya kuendeleza muungano.
 
Iwe ni kwa amani, maelewano, ustaarabu, maridhiano ama kwa chuki, husda, kejeli, dharau na matusi; Muungano uvunjike tu hata leo tupumzike kelele za wazanzibari kila siku kelele za malalamiko tuuuuuuu shit!
Tutengane nao ili tuanze kuwauzia huduma mbalimbali kama umeme, sasahivi wanatumia umeme wetu bure tena hawaguswi na mgao.

hizo ni akili za kibara mda wote zinafikiria ugali na maharage kama mahabusu...hivi nyie wenye umeme muwe munagaiyana kwa makisio then muwape bure ambao hamtaki hata kuwaona katika macho yenu! u must be some kind of psych.. kwa taarifa yako hamumpi mtu umeme wa bure kwa mapenzi gani mlokuwa nayo. majahili wakubwa
 
It seems they know what they want and now they are letting it flow freely....................tatizo la Watanganyika ni kuwa hamtaki kuunganisha dots au kuukubali ukweli...............muungano is no more

Absolutely true!!!!!!!!!!!!!!!!! watanganyika hawaamini kwa sababu ya uoga wao
 
Itakuwa chereko chereko na furaha isiyokifani kufufuliwa kwa taifa langu Tanganyika. Inaweza ikawa ndiyo mwisho wa nchi kuongozwa kiswahiliswahili. Mungu tuwezeshe tufike huko waja wako.

Kitendo cha kuungana na zanzibar ndicho kinaipa nguvu CCM tunataka uvunjike mwaka huu kwa kuupigia kura kabla hatujaendelea na mchakato wa katiba ili tupate nafasi ya kutengenza katiba ya TANGANYIKA
 
There are currently 35 users browsing this thread. (3 members and 32 guests)

Duh! huu uzi unasomwa na "guests" kibao! Nadhani ni wale wanaotetea muungano bila kuwa na hoja, sasa wanapima joto.
Sie wengine wala hatuna mengi, tunaitaka Tanganyika tu!
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom