Sibonike
JF-Expert Member
- Dec 23, 2010
- 17,276
- 17,983
Taarifa za vyombo vya habari leo ni kwamba Werema hataki katiba mpya. Anazungumzia kuweka viraka wakati wanasheria wenzake wanasema viraka vimefika mwisho.
Ukifuatilia mabadiliko ya katiba yaliyofanyika Kenya utajua kwa nini hataki katiba mpya. Moja ya mambo yalibadilisha na ambayo pia Tanzania tunayataka ni kupunguza madaraka ya Rais. Katiba mpya ya Kenya imeweka utaratibu wa kuwapata watu kama Jaji mkuu, Mkuu wa majeshi, mwanasheria mkuu wa serikali nk. Na inabidi hawa waliopo madarakani waondoke ili utaratibu mpya wa kuwapata utumike. Wao wamefanya hata kwa majaji wa mahakama ya rufaa. Inabidi waombo kazi upya kwa muundo mpya.
Werema anaelewa fika kuwa hilo linakuja Tanzania na huenda ana wasiwasi na sifa zake kuwa mwanasheria mkuu wa serikali. Kwenye utaratibu wa wazi wa kuzingatia sifa wengi wa wateule wa jamaa wasingeliona jua.
Ukifuatilia mabadiliko ya katiba yaliyofanyika Kenya utajua kwa nini hataki katiba mpya. Moja ya mambo yalibadilisha na ambayo pia Tanzania tunayataka ni kupunguza madaraka ya Rais. Katiba mpya ya Kenya imeweka utaratibu wa kuwapata watu kama Jaji mkuu, Mkuu wa majeshi, mwanasheria mkuu wa serikali nk. Na inabidi hawa waliopo madarakani waondoke ili utaratibu mpya wa kuwapata utumike. Wao wamefanya hata kwa majaji wa mahakama ya rufaa. Inabidi waombo kazi upya kwa muundo mpya.
Werema anaelewa fika kuwa hilo linakuja Tanzania na huenda ana wasiwasi na sifa zake kuwa mwanasheria mkuu wa serikali. Kwenye utaratibu wa wazi wa kuzingatia sifa wengi wa wateule wa jamaa wasingeliona jua.