Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Muswada wa sheria kuhusu fedha haramu uliendelea huku wabunge wakichangia hoja kwa kusuasua. Mwisho wa michango ndipo bunge lilipokaa kama kamati kupitia vifungu kwa ajili ya marekebisho na kuvipitisha. Hapo ndipo mh Mnyika alipotaka marekebisho katika kanuni ya adhabu ambapo mwanasheria mkuu pamoja na kutounga mkono hoja ya Mnyika lakini tayari bila kushituka ilikuwa imeshaingia kwenye hansad za bunge na kukubaliwa.
Ishu ilishitukiwa na Ole Sendeka na kupeleka ujumbe kwa AG ambaye naye alisimama kumkumbusha mwenyekiti kuwa Ole Sendeka alikuwa na taarifa ya kutoa. Wakati huo kulikuwa na muhudumu wa bunge aliyepeleka ujumbe kwa mwenyekiti kitu ambacho tafsiri yake ilikuwa ni kumwambia mwenyekiti akubali kusikiliza taarifa ya Ole Sendeka ambayo mwanzo aliikataa kwa madai kuwa hoja ilisha pita na kuungwa mkono kwa hiyo hakuna taarifa wala mwongozo tena. Baada ya Ole Sendeka kupewa nafasi hiyo ki mazabemazabe ndipo alipomkumbusha mwenyekiti kuwa hoja ya Mnyika iliyokataliwa na AG imeingia kwenye hansad tayari. Ndipo Mwenyekiti alipoamua kuwa hiyo sasa inafutwa kwenye hansad mara moja kisha na joho lake haraka haraka akaahirisha bunge na kutoka kwenye kiti japo CDM waliomba mwongozo. Hilo ndilo bunge letu lilivyo. Upande wa serikali hauko makini kabisa.
Kwa hili naona sasa watakuwa wanapanga kukutana Chako ni Chako kwa ajili ya kupongezana kwa vyuku na biere. Ngoja nami niende huko nikasake udaku.
Ishu ilishitukiwa na Ole Sendeka na kupeleka ujumbe kwa AG ambaye naye alisimama kumkumbusha mwenyekiti kuwa Ole Sendeka alikuwa na taarifa ya kutoa. Wakati huo kulikuwa na muhudumu wa bunge aliyepeleka ujumbe kwa mwenyekiti kitu ambacho tafsiri yake ilikuwa ni kumwambia mwenyekiti akubali kusikiliza taarifa ya Ole Sendeka ambayo mwanzo aliikataa kwa madai kuwa hoja ilisha pita na kuungwa mkono kwa hiyo hakuna taarifa wala mwongozo tena. Baada ya Ole Sendeka kupewa nafasi hiyo ki mazabemazabe ndipo alipomkumbusha mwenyekiti kuwa hoja ya Mnyika iliyokataliwa na AG imeingia kwenye hansad tayari. Ndipo Mwenyekiti alipoamua kuwa hiyo sasa inafutwa kwenye hansad mara moja kisha na joho lake haraka haraka akaahirisha bunge na kutoka kwenye kiti japo CDM waliomba mwongozo. Hilo ndilo bunge letu lilivyo. Upande wa serikali hauko makini kabisa.
Kwa hili naona sasa watakuwa wanapanga kukutana Chako ni Chako kwa ajili ya kupongezana kwa vyuku na biere. Ngoja nami niende huko nikasake udaku.