asha ngedere
Member
- Nov 6, 2009
- 92
- 11
Wadau,
Habari za uhakika nilizozipata hivi punde zinasema kwamba, kiwanda cha uchapaji cha Mwananchi leo kimegoma kuchapisha gazeti la DIRA YA MTANZANIA.
Ofisa mmoja anaiyetwa Semu Kabugumila ambaye anahusika na masuala ya kiwanda amewagomea wamiliki wa gazeti hilo na kusema hatalichapa ingawa wakubwa wake hawana tatizo...mazungumzo yamefanyika lakini jamaa nasikia ameshikilia uzi, sababu anazozitaja ni kwamba kwanini awali lilikuwa linamilikiwa na Msama promotion na sasa linamilikiwa na dira media group. idara ya habari maelezo haina nongwa, ila jamaa nasikia haambiliki kabisa.
baadhi ya watu wanahisi kwamba huenda kwa sababu mwananchi (magazeti) ilikuwa ikimilikiwa awali na rostam aziz, balozi ruhinda na bm, na kwa vile gazeti hilo kwa siku za karibuni limefululiza kuandika habari zinazohusiana na rostam et al, basi kuna mkono wa rostam katika kuzuia kuchapishwa kwa gazeti hilo kupitia kwa huyo anayeitwa kabugumila.
lakini cha kushangaza ni kwamba, pamoja na pande hizo mbili kuingia mkataba wa maandishi, huyo kabugumila amekuwa akitoa taarifa za kutolichapa gazeti kwa kutumia simu ya kiganjani tu bila maandishi.
hii ndiyo taarifa ambayo wadau tunaweza kuijadili, kwani naona kama inatia hofu sana na kutishia uhuru wa habari nchini, kama ilivyotokea siku zile hujuma kwa gazeti la RAIA MWEMA.
Mjadala unakaribishwa.
Habari za uhakika nilizozipata hivi punde zinasema kwamba, kiwanda cha uchapaji cha Mwananchi leo kimegoma kuchapisha gazeti la DIRA YA MTANZANIA.
Ofisa mmoja anaiyetwa Semu Kabugumila ambaye anahusika na masuala ya kiwanda amewagomea wamiliki wa gazeti hilo na kusema hatalichapa ingawa wakubwa wake hawana tatizo...mazungumzo yamefanyika lakini jamaa nasikia ameshikilia uzi, sababu anazozitaja ni kwamba kwanini awali lilikuwa linamilikiwa na Msama promotion na sasa linamilikiwa na dira media group. idara ya habari maelezo haina nongwa, ila jamaa nasikia haambiliki kabisa.
baadhi ya watu wanahisi kwamba huenda kwa sababu mwananchi (magazeti) ilikuwa ikimilikiwa awali na rostam aziz, balozi ruhinda na bm, na kwa vile gazeti hilo kwa siku za karibuni limefululiza kuandika habari zinazohusiana na rostam et al, basi kuna mkono wa rostam katika kuzuia kuchapishwa kwa gazeti hilo kupitia kwa huyo anayeitwa kabugumila.
lakini cha kushangaza ni kwamba, pamoja na pande hizo mbili kuingia mkataba wa maandishi, huyo kabugumila amekuwa akitoa taarifa za kutolichapa gazeti kwa kutumia simu ya kiganjani tu bila maandishi.
hii ndiyo taarifa ambayo wadau tunaweza kuijadili, kwani naona kama inatia hofu sana na kutishia uhuru wa habari nchini, kama ilivyotokea siku zile hujuma kwa gazeti la RAIA MWEMA.
Mjadala unakaribishwa.