Kongosho
JF-Expert Member
- Mar 21, 2011
- 35,999
- 24,163
Nimeamua kuileta hii mada makusudi kwenye jukwaa la MMU sababu japo inahusu ujasiriamali, pia inahusu pia mahusiano ya jinsia hizi mbili yanavyofanikisha au kukwamisha ufanisi kwa mwanamke wa kitanzania.
Baadhi ya mambo/visababishi vinavyofanya mjasiriamali kwa kike asifanikiwe (challenges) ni pamoja na:-
1) Ufinyu wa network za kibiashara: Si rahisi kwa mwanamke kujichanganya na watu waliofanikiwa kibiashara ambao wengi ni wanamme bila jamii kunyanyua kope. Mfano, mkute Kongosho na Reginald Mengi wakiwa Kempinski lazima unyanyue kope, kapata kipya?
2. Kukosa surport ya makusudi toka kwa mwanaume: Anapoomba mwongozo au ushauri au msaada wowote mwanamme anataka ajilipe kwanza ndo amsaidie
3. Mwanamke amelelewa kushika nafasi za usaidizi dhidi ya mwanaume wakati mjasiriamali anatakiwa awe kiongozi wa biashara yake na aoneshe njia au uelekeo.
4. Akina mama wana majukumu mengi ya kifamilia kama kuzaa na kulea familia inawaachia muda mchache wa kujituma katika ujasiriamali
5. Uchaguzi wa biashara: Kwa kuwa asilimia kubwa ya akina mama wana ufinyu wa mitaji, uzoefu, elimu wanajikuta wamejiingiza kwenye biashara ndogo ndogo zisizo na nafasi kubwa ya kukua mfano genge, saloon za kike?
6. Baadhi ya sheria na tamaduni zinawanyima nafasi, mfano kutorithi mali. Inawanyima upatikanaji wa dhamana za mikopo
7. Nafasi ya mwenza kama ameolewa.
Baadhi ya wanaume hawapendi wake zao wawazidi kipato, wengine hawawaamini wake zao kama wanaweza chochote, wengine wakiona wake zao wamefanikiwa wanakata huduma za familia.
Kwa kusema hayo hapo juu, mwanamke anayejiandaa kuingia kwenye ujasiriamali awe ameyatafakari kabla ya kuanza biashara asije akapata hasara au biashara kufa kabisa.
Kwa wanamme na jamii nzima kwa ujumla, je mtasaidiaje hiki kizazi cha kike kisonge mbele?
Ongezeeni sababu zingine ili tuzichambue kwa faida zaidi.
Baadhi ya mambo/visababishi vinavyofanya mjasiriamali kwa kike asifanikiwe (challenges) ni pamoja na:-
1) Ufinyu wa network za kibiashara: Si rahisi kwa mwanamke kujichanganya na watu waliofanikiwa kibiashara ambao wengi ni wanamme bila jamii kunyanyua kope. Mfano, mkute Kongosho na Reginald Mengi wakiwa Kempinski lazima unyanyue kope, kapata kipya?
2. Kukosa surport ya makusudi toka kwa mwanaume: Anapoomba mwongozo au ushauri au msaada wowote mwanamme anataka ajilipe kwanza ndo amsaidie
3. Mwanamke amelelewa kushika nafasi za usaidizi dhidi ya mwanaume wakati mjasiriamali anatakiwa awe kiongozi wa biashara yake na aoneshe njia au uelekeo.
4. Akina mama wana majukumu mengi ya kifamilia kama kuzaa na kulea familia inawaachia muda mchache wa kujituma katika ujasiriamali
5. Uchaguzi wa biashara: Kwa kuwa asilimia kubwa ya akina mama wana ufinyu wa mitaji, uzoefu, elimu wanajikuta wamejiingiza kwenye biashara ndogo ndogo zisizo na nafasi kubwa ya kukua mfano genge, saloon za kike?
6. Baadhi ya sheria na tamaduni zinawanyima nafasi, mfano kutorithi mali. Inawanyima upatikanaji wa dhamana za mikopo
7. Nafasi ya mwenza kama ameolewa.
Baadhi ya wanaume hawapendi wake zao wawazidi kipato, wengine hawawaamini wake zao kama wanaweza chochote, wengine wakiona wake zao wamefanikiwa wanakata huduma za familia.
Kwa kusema hayo hapo juu, mwanamke anayejiandaa kuingia kwenye ujasiriamali awe ameyatafakari kabla ya kuanza biashara asije akapata hasara au biashara kufa kabisa.
Kwa wanamme na jamii nzima kwa ujumla, je mtasaidiaje hiki kizazi cha kike kisonge mbele?
Ongezeeni sababu zingine ili tuzichambue kwa faida zaidi.