Mwanamke usimdanganye mumeo hujazaa!

Huyo jamaa amesusa msiba lakini ajue tatizo la kutokua na mtoto ni la kwake si la mkewe.
Kazi kwake sasa aende akapime kwa daktari
 
rekebisha kichwa cha habari tafadhali....
wanaodanganya na kuficha watoto ni wanaume na wanawake sio wanawake pekee....
 
Muda huu tunapoongelea uhuru wa miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika, kuna mwanamke hapa Chan'ombe Dodoma limemshuka, tena looooooooooooooote! Ameolewa ana miaka 9 ktk ndoa yake ingawa hajabahatika kuzaa ktk ndoa yake hii. Mumewe siku zote hakujua kuwa kabla ya kuoana alishazaa mtoto wa 'ujanani'. Hakumueleza mumewe wakati wa urafiki, uchumba na baada ya ndoa. Juzi huyo mtoto wake wa ujanani alokuwa akiishi na bibi alifariki hapa dodoma, hivyo ilibidi mama na mumewe waje dodoma, huku mume akijua kuwa mtoto aliyefariki alikuwa ni wa kaka wa mkewe. Hakukuwa na jipya lililoendelea zaidi ya hali ya majonzi miongoni mwa wafiwa.

Hali libadilika leo asubuhi wakati wa maandalizi ya kwenda kuzika wakati wa kuaga mwili. Mama alipoenda kwa jeneza, si ndo akaanza kulia kwamba anamuachia upweke kwani yeye ndiye alikuwa mwanawe pekee, ataishije bila kuwa na mtoto. Siku zote alikuwa akijivunia kuwa mzazi sababu ya yeye ingawa alikuwa akisemwa hazai na watu na majirani. Minong'ono ikawa mingi pale msibani baada ya kuona ameng'ang'ania kwa jeneza zaidi ya dk 5 ambapo ililazimu watu waende kumuondoa ili taratibu za mazishi ziende kama ilivyopangwa.

wakati minong'ono ikiendelea ndipo mumewe alipojua na kuthibitish kwamba kumbe mtoto aliyekuwa akimjua kama mpwa wa mkewe, ukweli alikuwa ni mtoto wa mkewe. Jamaa alimaindi sana, na nusura aondoke msibani ila busara ya wazee ilisaidia jamaa abaki msibani na kuendelea na mazishi. Ajabu mara baada ya kurudi mazishini, pamoja na juhudi za wazee na ndugu kumuomba baki ili waliongelee hilo, jamaa alifungasha vitu vyake na kurudi dar, pamoja na juhudi za mkewe kumsihi ili wamalize issue hii kabla ya kurudi zao dar na mumewe. Hakuna nayejua nini kitafuatia baada ya 'aibu' hii kujulikana.

My take: Chondechonde kina dadana wanaume pia, kama mtu kakupenda epuka kumdanganya issue ambazo ziko wazi kama hii au kabila yako. Mambo hayo hayana kificho yatakuja julikana tu. Na ukweli utakapojulikana utakosa pa kuuficha uso wako.

hili tatizo siyo la wanawake tu. sisi watanzania tulio wengi hatuwezi kusema ukweli, iwe wanawake au wanaume. pale tunapoona tunapapenda, wengi wetu tunapoteza uwezo wa kusema ukweli, tukifikiri kuwa tutakataliwa.hatuwezi kuacha kusema uongo kwakuwa hatujajaribu ukweli na kupata faida yake. wengi wetu ni wa ongo ktk nyanja zote.

chukua mfano, uingie ktk matatizo na mtanzania wa leo, say amepotelewa na kitu ktk mazingira wewe ulikuwapo. uwe umeiba au hujaiba, atakapo tangaza kupotelewa lazima ataongeza idadi au thamani ya vilivyo potea, atatia na chumvi ya maneno mengine mengi. matokeo yake hata pale tunapo peleka kesi mahakamani zile chumvi na uongo, zina gundulika na hata kufanya ule ukweli wa msingi kupotezwa na uongo.

tazama chumvi za kamanda kova,pccb ktk kesi ya muro

kwetu sote;
tujifunze kusema ukweli, ukweli unafaida kuliko uongo. ukweli unaleta kujiamini, na ukimkamata mtu ukamshawishi kwa kusema ukweli , hata upendo wake unakuwa ni usio na mashaka
 
Mi staki kujua hayo ya zamani.Kama alikuwa na mtoto au anao..sihitaji kujua.
Akinifica so much the better.Mradi ahudumie mwanae kimyakimya bila kunihusisha.
 
ni makabila gani yanaongoza kwa kuficha ukweli? hili ni muhimu kulifahamu ili mtu unapotafuta mchumba ukidondokea kwenye hilo kabila ufanye full check up....nyumbakubwa tufahamishe pls..
Mie nawataja kama wataniua waniue ila ukweli ndio huo..... Wanawake wa kabila la kirangi wengi wana hiyo tabia sana ya kuficha watoto...



Back to topick: ni ulimbukeni wa hali ya juu na naungana na aliyesema kuwa ni kumnyima mtoto haki yake ya msingi...kama mwanaume kakupenda hata ukimwambia umezaa watoto 10 hawezi kukuacha, kwani kuwa na mtoto/watoto ni dhambi kwenye jamii? Tena basi hakuna dhambi mbaya kama mwanamke mzima na akili zako unabeba mimba miezi 9 kisha unazaa kwa uchungu afu eti unakutana na mtoto wa mwanamke mwenzio unamkana mwanao loooh.... Ni aibu kumtelekeza mtoto kijijini kwa bibi na kumlazimisha akuite shangazi/ dada/ mamdogo n.k..
 
kumbe warangi ni kiboko...........duh...inatakiwa kuwa mtafiti kabla hujadondokea humo kwenye mahusiano...
Mie nawataja kama wataniua waniue ila ukweli ndio huo..... Wanawake wa kabila la kirangi wengi wana hiyo tabia sana ya kuficha watoto...



Back to topick: ni ulimbukeni wa hali ya juu na naungana na aliyesema kuwa ni kumnyima mtoto haki yake ya msingi...kama mwanaume kakupenda hata ukimwambia umezaa watoto 10 hawezi kukuacha, kwani kuwa na mtoto/watoto ni dhambi kwenye jamii? Tena basi hakuna dhambi mbaya kama mwanamke mzima na akili zako unabeba mimba miezi 9 kisha unazaa kwa uchungu afu eti unakutana na mtoto wa mwanamke mwenzio unamkana mwanao loooh.... Ni aibu kumtelekeza mtoto kijijini kwa bibi na kumlazimisha akuite shangazi/ dada/ mamdogo n.k..
 
Huyo mwanaume nae hovyoooo......kususa msibani maana yake nini sasa?? Au alidhani yale aloambiwa ndo yatageuka miujiza?? Atleast hata mwanamke hakughasi kwa malezi, kuna mijanaume mingine inasubiri mpaka ikishakuweka ndani ndo unaanza kuletewa orodha ya watoto, mmoja baada ya mwingine utadhani unasajili wacheza mpira bana!!! Sio issue kabisa waungwana, kutakiana lawama tu!

Tena umesema kweli, kuna bro. mmoja nafanya kazi naye ofisi moja alikuwa na mke wakapata wototo wawili, bahati mbaya mke akafariki mtoto wao wa pili akiwa mdogo sana (1.5yrs). Baadaye akaoa mdada mwingine ambaye alimkuta na kabinti kake. Mkaka aliwatambulisha kwa mke wake huyu wale watoto wawili tu wa marehemu, kumbe mshikaji ana msululu wa watoto kabla ya ndoa yake ya kwanza. Sasa ameshaona yule mke yuko fair kwa wototo aliowakuta ameamua kuleta kundini mtoto mmoja baada ya mwingine na ameshaleta watatu mpaka sasa. Mdada anajiuliza sijui christmas hii atapata mtoto mpya ama la . Na zote ni ndume copy right na baba yao mpaka kuwatoa nduki nomaaaaaa. Kwa hiyo ni yetu sote waume kwa wake.
 
rekebisha kichwa cha habari tafadhali....
wanaodanganya na kuficha watoto ni wanaume na wanawake sio wanawake pekee....

Natamani ungesoma paragrafu ya mwisho pengine usingeweza kupost
 
Muda huu tunapoongelea uhuru wa miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika, kuna mwanamke hapa Chan'ombe Dodoma limemshuka, tena looooooooooooooote! Ameolewa ana miaka 9 ktk ndoa yake ingawa hajabahatika kuzaa ktk ndoa yake hii. Mumewe siku zote hakujua kuwa kabla ya kuoana alishazaa mtoto wa 'ujanani'. Hakumueleza mumewe wakati wa urafiki, uchumba na baada ya ndoa. Juzi huyo mtoto wake wa ujanani alokuwa akiishi na bibi alifariki hapa dodoma, hivyo ilibidi mama na mumewe waje dodoma, huku mume akijua kuwa mtoto aliyefariki alikuwa ni wa kaka wa mkewe. Hakukuwa na jipya lililoendelea zaidi ya hali ya majonzi miongoni mwa wafiwa.

Hali libadilika leo asubuhi wakati wa maandalizi ya kwenda kuzika wakati wa kuaga mwili. Mama alipoenda kwa jeneza, si ndo akaanza kulia kwamba anamuachia upweke kwani yeye ndiye alikuwa mwanawe pekee, ataishije bila kuwa na mtoto. Siku zote alikuwa akijivunia kuwa mzazi sababu ya yeye ingawa alikuwa akisemwa hazai na watu na majirani. Minong'ono ikawa mingi pale msibani baada ya kuona ameng'ang'ania kwa jeneza zaidi ya dk 5 ambapo ililazimu watu waende kumuondoa ili taratibu za mazishi ziende kama ilivyopangwa.

wakati minong'ono ikiendelea ndipo mumewe alipojua na kuthibitish kwamba kumbe mtoto aliyekuwa akimjua kama mpwa wa mkewe, ukweli alikuwa ni mtoto wa mkewe. Jamaa alimaindi sana, na nusura aondoke msibani ila busara ya wazee ilisaidia jamaa abaki msibani na kuendelea na mazishi. Ajabu mara baada ya kurudi mazishini, pamoja na juhudi za wazee na ndugu kumuomba baki ili waliongelee hilo, jamaa alifungasha vitu vyake na kurudi dar, pamoja na juhudi za mkewe kumsihi ili wamalize issue hii kabla ya kurudi zao dar na mumewe. Hakuna nayejua nini kitafuatia baada ya 'aibu' hii kujulikana.

My take: Chondechonde kina dadana wanaume pia, kama mtu kakupenda epuka kumdanganya issue ambazo ziko wazi kama hii au kabila yako. Mambo hayo hayana kificho yatakuja julikana tu. Na ukweli utakapojulikana utakosa pa kuuficha uso wako.

Nadhani huyu dada alisahau ule usemi usemao "kuwa mkweli leo ili usiadhirike kesho" angekuwa mkweli tangia mwanzo yote hayo yasingetokea sasa wana Jf tujifunze kwa kosa la mwenzetu huyu kuliko kuja kujifunzia kwenye makosa yetu wenyewe
 
Kuna kabila moja so far ndio nimekuja ku conclude wana hiyo tabia saaana. Wakizaa ujanani wanaficha kuanzia mimba mpaka mtoto. Jirani yetu alikuja kujua mtoto wa mkewe siku binti anafunga ndoa; MC akasema mama wa bibi harusi, kasimama mama ambaye sote tulijua ni dada yake na ndo alomlea watu wakabaki midomo wazi. From there ndo tukajua kumbe alikuwa mtoto wake. Mumewe alimind kishenzi ila ndio hivyo walishakaa kwenye ndoa more than 20 years na wana watoto wengine.

Nina rafiki yangu nae watu wanasema chini chini (wamejua from reliable source) ana mtoto alimzaa akiwa form two; nayo ni siri sirini. Na alikuja kuolewa na kuachika bila ku mention kuwa ana mtoto. Sasa ana mtoto mmoja kwa ex hubby wake.

BUT it is not fair kwa hao watoto wanaonyimwa haki ya kuita mama zao "Mama" very selfish behavior indeed!

Tuwekane wazi ni kabila gani hilo?
 
Mie nawataja kama wataniua waniue ila ukweli ndio huo..... Wanawake wa kabila la kirangi wengi wana hiyo tabia sana ya kuficha watoto...



Back to topick: ni ulimbukeni wa hali ya juu na naungana na aliyesema kuwa ni kumnyima mtoto haki yake ya msingi...kama mwanaume kakupenda hata ukimwambia umezaa watoto 10 hawezi kukuacha, kwani kuwa na mtoto/watoto ni dhambi kwenye jamii? Tena basi hakuna dhambi mbaya kama mwanamke mzima na akili zako unabeba mimba miezi 9 kisha unazaa kwa uchungu afu eti unakutana na mtoto wa mwanamke mwenzio unamkana mwanao loooh.... Ni aibu kumtelekeza mtoto kijijini kwa bibi na kumlazimisha akuite shangazi/ dada/ mamdogo n.k..

Mimi simoooooooooooo! mwenyewe niliileta thread bila kutaja kabila hapa. Tena una bahati wahusika wamekaa kimyaaaaaaa, ingekuwa wale jamaa wa midizini, ndo ungejua leo nini kilisabababisha tumbusi akose manyoya shingoni. Narudia mie simoo, na naomba thread hi isichafuliwe kwa kutajana kabila jamani, wenyewe hawapendiiiiiiiiiiiiiiiiiiii, ooooooooooh!
 
Hivi mtu anakudanganya kuwa alikua na mtoto unakuja kugundua unakasirika vibaya,tatizo linakua hasa wapi?Uongo uliolishwa au ni mtoto uliekua hata humlei?Au ni mazoea?
 
Hivi mtu anakudanganya kuwa alikua na mtoto unakuja kugundua unakasirika vibaya,tatizo linakua hasa wapi?Uongo uliolishwa au ni mtoto uliekua hata humlei?Au ni mazoea?
Uongo ndio tatizo. . . wengi hawajali kulea/ matumizi wanajali kutokuambiwa ukweli.
 
Hakuna mtu anayempenda mtu muongo,leave aside awe ndo mwenza wako wa maisha. Maana utajiuliza mengi sana mfano ni mangapi mengine aloficha.

Hivi mtu anakudanganya kuwa alikua na mtoto unakuja kugundua unakasirika vibaya,tatizo linakua hasa wapi?Uongo uliolishwa au ni mtoto uliekua hata humlei?Au ni mazoea?
 
Afu mi naona watoto waliokuwa kind of rejected na wazazi wao huwa wanakuwa na tabia tofauti kidogo.
1. defensive nature, hujamguza lakini atakavyokuja na ushahidi kwamba hakufanya yeye kosa ni mkubwa kweli
2. Kutojiamini, mkiwa naye anahisi mnamchukia hata kama hakuna haja ya kuhisi hivyo
3. trust, haamini mtu hata mmoja ile ya kiukweli siku zote yko kimachale machale tu haamini mtu hata mmoja
4. Love, hata unconditional affection kwa mtu hata. Anampenda mtu foa a reason labda anapata kitu fulani toka kwake na aina hizo. Lakini kumpenda mtu freely ngumu sana kwao
5. Kisasi, du bahati mbaya umeingia kwenye kumi na nane yake kisasi chao huwa ni kikali kweli. Wanaishi by jino kwa jino rule.

Basi mie huwa napata shida kuwa nao katika mtiririko wa kila siku wa maisha maana wako siwezi hata elezea hadi ukae nae ndo labda mtanielewa hapa.
 
Wana JF mimi nipo tofauti na hili swala la kuhusisha makabila ya watu na hii tabia ya kuficha watoto wa ujanani. MSIMAMO WANGU NI HUU TABIA HII IPO KARIBU KILA KABILA NA INATOKANA NA MAKUZI YA FAMILIA HUSIKA NA SI KABILA

Mchango wangu kwa topic hii ni Wazazi na walezi wawafundishe watoto wawe wa kike au wa kiume KUWA WAKWELI na kwa kuwa wakweli ndipo jamii itaondokana na tabia mbalimbali zisizofaa km hii
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom