khaaa! hii inanibidi niilie msuli kidogo manake ninaona kama kuna maeneo natofautiana sana na mtazamo wako.
Aaaaah gfsonwin, mie sio mhafidhina bana, kama unatofautiana na mimi wewe weka point zako hapa, kamwe sichukizwi na mtu anayetofautiana na mimi, kwani humu tunajifunza wote....... Naomba sana usisite kutoa mtazamo wako bila kujali kama nitafurahi au sitafurahi,....
karibu dada ukumbi ni wako.
kabla sijajaja na mashoka yangu hebu niambie hapa unaongelea wapenzi ambao ndo kwanza ni bf &gf ama ambao wapo kwenye uchumba ama ambao tayari wako ndoani?
Mwanamke: Dalili zitakazomfanya mpenzi mpya akuone wewe ni king'ang'anizi…!
Hizi ni miongoni mwa sababu ambazo wanaume wengi huchomoa mapema kwa wapenzi wao wapya kabla uhusiano haujashika kasi. Kuna wakati wanawake hukosea na kuvuka mipaka mwanzoni tu mwa uhusiano. Anamganda mwanaume haraka sana au anaonesha dalili zote za kujipendekeza kupita kiasi. Lakini jambo ambalo wanawake wengi hawalijui ni kwamba, wanaume wako makini sana kuwakwepa wanawake ving'ang'anizi……..
Hamuwezi kutuona kuwa ving'ang'anizi kwa sababu ung'ang'anizi kwenu ni kitu positive. Tofauti iliyopo ni kwamba kwa wanaume ung'ang'anizi ni kitu negative, lakini kwa wanawake ni kitu positive. Mking'ang'aniwa ndo mnafurahi na kuona mnapendwa. Ikitokea mwanamke akakuona we king'ang'anizi basi labda hakupendi au hana matarajio yoyote na wewe.
Umejuajeee! Mimi hilo la urafiki na mamushka mkwe limenishinda kabisa, kila nikijaribu holaaa! Pamoja nakumaliza hela zangu kumnunulia miwaxx ya west africa bado tunatoana jasho
ha haa thanks mkuu jenenekewao nipeukweli kweli umeitendea haki id yako vyote ulivosema sina cha kuongeza i salute you