Mwanamke aliyepambana na Majambazi azawadiwa na Polisi

barafu

JF-Expert Member
Apr 28, 2013
6,726
32,818
image.jpeg


MWANAMKE ALIYEPAMBANA NA MAJAMBAZI AZAWADIWA LAKI TANO

Polisi mkoa wa Kipolisi Tarime/Rorya yampa zawadi ya Laki tano Bi Sophia Manguye Mkazi wa kata ya Sirari wilaya ya Tarime mkoani Mara kwa ushujaa wake wa kupambana na Majambazi na kufanikiwa kuwanyang'anya silaha aina ya SMG.
Source:East Africa Tv
 
Unajua kupambana na mtu mwenye silaha na kuweza kumnyanganya si jambo dogo. Zawadi aliyopewa hailingani na thamani ya silaha aliyoipokonya na uhalifu ambao ingelifanya ni bora aongezewe ili kuwapa moyo watu wengine.
 
View attachment 322784

MWANAMKE ALIYEPAMBANA NA MAJAMBAZI AZAWADIWA LAKI TANO

Polisi mkoa wa Kipolisi Tarime/Rorya yampa zawadi ya Laki tano Bi Sophia Manguye Mkazi wa kata ya Sirari wilaya ya Tarime mkoani Mara kwa ushujaa wake wa kupambana na Majambazi na kufanikiwa kuwanyang'anya silaha aina ya SMG.
Source:East Africa Tv
Duh kumbe kweli
 
Hii zawadi ilitakiwa itolewe kimya kimya, halafu na polisi wa kawaida mmoja tu. Hapo wamemhatarishia usalama wake na familia yake. Huko vijijini laki tano ni hela ndefu sana. Kuna watu mpaka wanahama duniani bila kuishika.
 
Unajua kupambana na mtu mwenye silaha na kuweza kumnyanganya si jambo dogo. Zawadi aliyopewa hailingani na thamani ya silaha aliyoipokonya na uhalifu ambao ingelifanya ni bora aongezewe ili kuwapa moyo watu wengine.
Moyo wa kutoana roho, uwiii uwiiii uwiii yelewii eeh
 
Hii zawadi ilitakiwa itolewe kimya kimya, halafu na polisi wa kawaida mmoja tu. Hapo wamemhatarishia usalama wake na familia yake. Huko vijijini laki tano ni hela ndefu sana. Kuna watu mpaka wanahama duniani bila kuishika.
Haha kuna ukweli hapa maana hata hao majambazi na SMG yao walikua wameiba laki na themanini
 
Ni vizuri polisi wamuajiri huyu mama. Hiyo ilikuwa ni sawa na kujitoa muhanga kwa ajili ya usalama wa wengi.
 
Back
Top Bottom