Mwanamke akipendeza anamfurahisha nani?

vaa any vazi linalokukeep smart and comfotable dats all...........abt kuchaguliwa uvae nn its ok so long utakuwa umefanya shoping mwenyewe
jikubali mwenyewe kabla watu hawajakukubali
 
kwani mpaka ajiunge humo ndo apate uzoefu dear??

sio lazima lakini ukiingia yaani ukiwemo ina-matter zaidi, si unajua mambo aya theory vs practical? nje ya ndoa watu wanatamani kuingia na wanaamini wanaoboronga si waangalifu, lakini wakiingia baadhi yao hawachukui hata miaka miwili, utasikia............ aka babu we, usi....... eti sweet heart wake kishakuwa babu!!!!!!!!!!!1
 
.........Hakuna cha kupigwa talaka wala nini,inategemea na jinsi alivyonikuta napendelea kuvaa mavazi ya aina gani.
Kwanza mie sikubalini na dhana kwamba mavazi yanaelezea tabia ya mtu.Kama mtu una tabia chafu ni chafu tu...........hata uvae vazi refu linatambaa hadi chini kama tabia yako mbaya ni mbaya tu.

mi ninachokiona kwene misimamao yenu ni kuwa mnaweza hata kuwakwaza waume zenu kwa hiyo misimamao. labda niwakumbushe kuwa romance kwa wapendanano ziko kila mahali sio chumbani pekee, sasa ukitoka na vazi asilopenda, utakuwa umeisha punguza hamu juu yako na ukiendelea hivyo, utadhooofisha mapenzi na huenda yakafa hatimaye....ndio kwenye talaka huko...........
 
nafikiri kwenye ndoa kuna mengi zaidi. hayo uliyotaja ukiingia kwenye ndoa huongezeka intensity. halafu kuna ishu wanasema wajuaji inaitwa kuzoeana na wengine kuchokana. yaani kama kwenye uhusiano kuna kiu, kwenye ndoa hufikia kiasi cha kukinaiana sasa hapo ndo a number of implications zinaanza ................

mmh aisee!..mengi nayasikia na kuona!! Nitaingia tu mana nataka nishuhudie labda inaweza kuwa tofauti kwangu..
Yaani sasa hata maswala ya kuvaa nguo nako unaweza kununiwa hata wiki eeh!!??..
 
anajifurahisha mwenyewe na nafsi yake! kwani si amevaa kwa mapenzi yake mwenyewe!
 
anajifurahisha mwenyewe na nafsi yake! kwani si amevaa kwa mapenzi yake mwenyewe!

Pape, unaongelea mkeo au mpita njia. Mkeo hawezi kujifurahisha mwenyewe tu halafu wewe ubaki kuangalia. Labda kama na wewe unaridhika na anavyotoka au kama umemchukua kuondoa nuksi. Kama umewekeza kila kitu chako basi huwezi kuacha hisa zako zikategeketea na wewe umekenua meno tu! Lazima uhakikishe kuwa matamanio yako kwake angalau yanatimia kwa kiasi kikubwa. Mfano, wewe unapendelea kumwona mkeo ndani ya skini jeans na top la nguvu wakati yeye anakomalia batik na mivazi ya Kinigeria, ujue hapo utaishia kutafuta hizo taste zako nje. Mzigo ni wako na lazima uhakikishe uko salama. The vice versa is also true.

Kila abiria anachunge mzigo wake wa ndani, na hilo siyo kwa mavazi tu! Watch out, someone else might be giving a helping hand!:rolleyes::rolleyes:
 
hawa wanawake huwa wanatuzuia kuvaa vipenzi na vest eti tunaonyesha miili yetu na tutawatamanisha wanawake wengine, ila wao wakivaa poa tu. akitongozwa na wanaume kumi mooja hakosi. mwenza wangu hatavaa nguo za ajabu
 
Pape, unaongelea mkeo au mpita njia. Mkeo hawezi kujifurahisha mwenyewe tu halafu wewe ubaki kuangalia. Labda kama na wewe unaridhika na anavyotoka au kama umemchukua kuondoa nuksi. Kama umewekeza kila kitu chako basi huwezi kuacha hisa zako zikategeketea na wewe umekenua meno tu! Lazima uhakikishe kuwa matamanio yako kwake angalau yanatimia kwa kiasi kikubwa. Mfano, wewe unapendelea kumwona mkeo ndani ya skini jeans na top la nguvu wakati yeye anakomalia batik na mivazi ya Kinigeria, ujue hapo utaishia kutafuta hizo taste zako nje. Mzigo ni wako na lazima uhakikishe uko salama. The vice versa is also true.

Kila abiria anachunge mzigo wake wa ndani, na hilo siyo kwa mavazi tu! Watch out, someone else might be giving a helping hand!:rolleyes::rolleyes:


Apo mkulu DC umegusa penyewe.....kwa nini aninyime ninavopenda kumwona kisha anilaumu kwa kwenda kuangaza macho huko nje! Misimamo isiyokuwa na msingi sio mizuri kabisa kabisa kwenye mahusiano.....
 
Lengo la kwanza la mavazi ni kujisitiri. Malengo mengine yaweza kuwa kujifurahisha binafsi, mwenza au watu wengine baki. Lakini mavazi pia yanaweza kuashiria 'kazi' ya mtu husika na inaweza kwenda zaidi na kuwa matangazo ya biashara. Ni muhimu kujua watu wengi wanamevaluate mtu kwa mtizamo wa nje (including mavazi) kwa karibia asilimia 70%.

Katika ndoa nadhani pamoja na uhuru wa kila mtu kuamua nguo ya kuvaa (na wakati gani avae), lakini pia ni muhimu kuzingatia mawazo/mtizamo wa mwenza wako. Na hili linakuwa muhimu zaidi kama mnatoka pamoja. Mara nyingine, mwenza anaweza kuvaa katika namna ambayo unaona 'itakupa shida' kuji associate nae mbele za watu. Ni katika hili nadhani unaweza ukamshauri (kwa nia safi tu!) mwenza kuvaa nguo ambayo kwa mtizamo wako inaweza kuwa appropriate kwa shughuli husika.

Lakini hivi kupendeza maana yake nini? Can it be something internal and personal (like some are trying to suggest)? Au ni suala la 'watazamaji'?
 
both... myself and my partner...:)

and he should do the same... otherwise i will lose interest on him... cos I have standard and he should keep up with the standard.:)
 
both... myself and my partner...:)

and he should do the same... otherwise i will lose interest on him... cos I have standard and he should keep up with the standard.:)

N,

Wewe ni mdada wa kipekee kabisa. Nimefuatilia toka mwanzao lakini ni wachache sana walikuwa na huo mtazamo. You are selfless! Hope Mungu amekutunuku/atakutunuku kilicho chema!
 
Tunavaa ili tupendeze ila tukishakuw ana wenzi wetu mara nyingi kama mimi huwa napenda mwenzangu aseme nivae nini ili yeye afurahi na huko tutakapokuwa awe na confidence na mkew. mara zote ni respect, hata mie naweza penda kitu fulani akavaa ili nifurahi.

Big up guys, vaeni mridhishane.
 
mi japo umri upo kati na ni mom wa 3, no one will tell me what to wear! yani navaa chochote kinachonifanya niwe comforatble na kujickia nimependeza for that brightens my mood!
Inaelekea huyo jamaa nae ana kawivu kakijinga, mwanamke akivaa nguo aipendayo akapendeza ni jambo la kujivunia kutoka nae, au wanaume hamjisikii raha pale wanaposema mkeo kapendeza, haujioni nawe kidume eti?!!!!
 
, au wanaume hamjisikii raha pale wanaposema mkeo kapendeza, haujioni nawe kidume eti?!!!!

Nadhani hapo ishu ni kupendeza kwa mtizamo wa nani. Unaweza kujidhania umependeza kumbe hamna kitu! Watu wanakung'ong'a tu ukipita! hivyo ni vema kama mdau hapo juu alivyosema ukapata ushauri kutoka kwa mwandani wako!
 
Tunavaa ili tupendeze ila tukishakuw ana wenzi wetu mara nyingi kama mimi huwa napenda mwenzangu aseme nivae nini ili yeye afurahi na huko tutakapokuwa awe na confidence na mkew. mara zote ni respect, hata mie naweza penda kitu fulani akavaa ili nifurahi.

Big up guys, vaeni mridhishane.

Hayo ndiyo mambo. Hakuna sababu ya kuendekeza umimi kwenye mahusiano. Mwenzio akishakupa complement (na wewe ukawa unaamini kuwa siyo za kizushi kwani umependeza kweli) hata wengine wakibeza watakuwa wanajisumbua. Mwenye mali katoa ruksa. Hao wengine wana uamuzi wa kujoin kukupongeza au kuendelea na porojo zao. They are harmless anyway!

mi japo umri upo kati na ni mom wa 3, no one will tell me what to wear! yani navaa chochote kinachonifanya niwe comforatble na kujickia nimependeza for that brightens my mood!
Inaelekea huyo jamaa nae ana kawivu kakijinga, mwanamke akivaa nguo aipendayo akapendeza ni jambo la kujivunia kutoka nae, au wanaume hamjisikii raha pale wanaposema mkeo kapendeza, haujioni nawe kidume eti?!!!!

Huo ndio umimi ninaouongelea. Hope you wont tell your husband what to wear as well. What if someone else (smart and tender than you) takes over?

Akina nani hao unawaongelea (kwenye blue) endapo mimi sijasema au kuridhika? Charity begins at home. Hizo complement za nje inaweza kuwa ni mitego halafu wewe unavimba kichwa. Ni vizuri kuonesha kuwa angalau unamjali mwenzio na hisia zake.
 
Je mwanamke akivaa nguo halafu no-body comments kama amependeza au vipi atajisikiaje? Mwanamke nadhani anavaa akitegemea asifiwe au aambiwe nguo hiyo mhhhh!! Hivyo najumuisha kuwa mwanamke hana uhuru wa kuvaa nguo anayotaka bali anahakikisha sikio lake litakuwa tayari kupokea maoni yoyote juu ya kivazi chake.
 
Mwanamke kupendeza ni pamoja na kumfurahisha mumewe na hata yeye mwenyewe anajifili confortable tatizo ni kuwa unataka upendeze kwa aina ipi je iwe kama matangazo kuwa hata public wakikuona wasikutofautishe na mfanyabiashara? maana swala si kuvaa nguo fupi kuwa ndio utapendeza au kuvaa nguo ndefu kuwa ndio utapendeza maana unaweza kuvaa nguo ndefu lakini isiwe na heshima vile vile au unaweza kuvaa nguo fupi lakini ina hadhi yaani sio kimini ambacho huwezi kutembea wala kuinama.

so inategemea huyo mvaaji hilo lengo lake la kupendeza limeegemea upande gani.
 
Back
Top Bottom