kipanga mlakuku
Member
- Jun 9, 2011
- 92
- 53
Nilipojitokeza hadharani kwa mara ya kwanza kupinga vikali imani iliyokuwa inaenezwa mithili ya moto usaambaao kwenye nyasi kavu kuwa eti Saed Kubenea ni mpambanaji wa kweli. Nilijitokeza kwenye majukwaa kadhaa ikiwa ni pamoja na Mwanahalisi wenyewe kukanusha vikali imani hii ambayo niliamini kuwa ni upuuzi mtupu lakini pia nikaahidi kwa kusema "time will tell"
Ikiwa takribani ni miaka sita sasa ni dhahiri kabisa kuwa kile ambacho nilikibashiri sasa ndicho kinatokea na labda niseme wazi huu ni mwanzo tu kaeni mkao wa kula kwa maana kuna atakayekula kabisa matapishi yake. Wafatiliaji wa gazeti la Mwanahalisi hususani mwandishi Saed Kubenea sasa kwa kujua au kutojua naona wote kwa umoja wao wanaungana na mimi kuwa "bei yake " imefika na sasa amenunuliwa.
Kwa mantiki hii nimekusudia kusema "kweli" yote kuhusu Saed Kubenea, ukweli wenyewe ni huu kwa mchezo aliofanya jana kwenye kichwa cha habari cha nje hakuna ubishi kuwa amepata sifuri mtihani huo. Sababu za kuyasema haya ziko wazi kama ifuatavvyo;
1.Alichofanya Samwel Sitta kumtuhumu kwenye kipindi cha dakika 45 ilikuwa ni kama kuchokoza nyuki
2.Baada ya kutuhumiwa Kubenea akaanza mashambulizi na matusi kedekede dhidi ya Sitta
3.Kwa vile Mungu alishapanga kumuumbua akajikuta mara moja amefanya mchezo wa kitoto kwa kutaka kuuaminisha umma wa Tanzania kuwa hajanunuliwa eti kwa kuibuka na kichwa kikubwa cha habari "Mzimu wa Ricmond wamwandama Lowassa" katika toleo la jana huku akimpachika Jacob Daffi jukumu la kuiandika taarifa hiyo.
MY TAKE;
Kwa vile yeye (Kubenea)amejiumbua mwenyewe tena kwa mbinu rahisi za kujifanya bado yuko ngangari dhidi ya Lowassa, sasa na tuseme enough is enough kwani sasa imetosha, atuache tujitafutie habari wenyewe kuliko kupika habari hizo kwenye vyumba vya "mafisadi" kisha kutaka kutunywesha, sisi kama watu huru na wazalendo tunasema, kwa hili kubenea umepata zero na tunaweka "BIG NO!