MwanaHALISI: Makala ya leo ya Ndimara ni 'must read'

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
234
Ukombozi waja… kipigo chayoyoma

Na Ndimara Tegambwage

Njia bora ya kuharakisha mabadiliko ya kisiasa nay a kiuchumi nchini Tanzania ni kubughudhi viongozi wa upinzani kila kukicha.

Kamata. Bambika mashitaka. Weka rumande. Peleka mahakamani… Achia kwa dhamana. Kamata. Weka rumande. Fungulia mashitaka…kama jana, kama leo, kama kesho, kila siku.

Wasimamizi wa mradi huu – wakipenyeza amri kwa watekelezaji – wanafikiri kwa njia hii, watafaulu kudhoofisha na hata kuua upinzani dhidi ya serikali chovu ya Chama cha Mapinduzi (CCM).

Polisi hawafurahii kukamata. Polisi wanafurahia kubaki na ajira yao. Kubaki na vimishahara vyao. Ni ya magwanda yao yanayoelekeza urefu wa kamba yao katika kujikimu.

Polisi wakamataji hawana masilahi katika kukamata viongozi wa upinzani. Wanatii amri ya wakubwa zao. Wakubwa wenye uswahiba na wakubwa siasani.

Wanaotumiwa kukamata hawana masilahi katika kufyatua risasi. Katika kulipua mabomu ya machozi. Katika kumimina maji-pilipili machono mwa wananchi. Hawana!

Ndani ya polisi nako kumejaa “Kabwela hana kitanda” – yule wa kwetu wanaita ndala omwa fulano – mtegemea fadhila!

Watawala wanatoa amri. Polisao wanatii amri. Watawala wanatoa amri kujilinda leo. Leo hii. Kufika au kutofika kesho so hoja kwao. Wanataka leo nay a leoleo.

Kwa hiyo kamata! Bambikia mashitaka. Weka rumande. Peleka mahakamani. Achia kwa dhamana. Kamata. Weka ruymande. Fungulia mashitaka… kama jana, kama leo, kama kesho, kila siku.

Chukua mfano wa Mbowe. Freeman wa Chadema. Kijana mdogo tu mwenye mdomo mpana uliojaa ushawishi.

Mbowe, kama Dk Willibrod Slaa na viongozi wengine wa Chadema, akilia wananchi wanaomsikiliza wanalia naye. Akicheka wanacheka naye. Akinuna wananuna naye. Watawala wanaamuru: kamata. Bambika mashitaka.

Chuykua mfano wa Chadema. Chama ambacho kimejidhihirishia kuwa na uwezo mkubwa wa kuwafikia wananchi, kuwaibua kutoka lindi la woga na ujinga.

Chukua mfano wa Chadema. Chama ambacho kimefuta umaarufu wa bandia wa CCM, kukinyang’anya wafuasi, kukibakizia wanafunzi wanaoswagwa na walimu wanaolinda ajira zao kama polisi.

Chukua mfano wa Chadema. Chama ambacho wengi wanasema mgombea wake wa urais alishinda na CCM inakiri nguvu yake ndani ya vikao na kwenye hadhara.

Chukua mfano wa umati wa wananchi unaojitokeza kwenye mikutano ya Chadema; maswali yanayoulizwa na wananchi na ahadi wanazotoa ili kuing’oa CCM

Fuatilkia kashifa lukuki zilizoizonga CCM na serikali yake; kushindwa kwa chama hicho kujibu hoja kuhusu wizi ndani ya benki kuu, kuhusu matumizi hewa; kuhusu mikataba ya kihuni nay a kinyonyaji.

Kazi ya kisiasa iliyofanywa na upinzani, hasa Chadema, CUF na NCCR-Mageuzi, imewezesha wananchi kuelewa kuwa CCM siyo chama cha siasa, ni chama cha ukwapuaji.

Kukua na hata kuimarika kwa vyama vbya upinzani, hasa Chadema hakutokani na ubora na umakini wa viongozi wake peke yake. Kunatokana pia na mazingira ya kutota kwa waliotawala kwa miaka 50.

Chadema wamepata fursa ya kuzunguka nchi na kueleza kuwa mataifa huadhimisha miaka 50 ya uhuru wake kwa kuonyesha utawala bora – kisiasa na kiuchumi.

Lakini katika Tanzania, hasa tunapokaribia kuadhimisha miaka 50, watawala ndio huionyesha walivyo na makucha marefu ya kupora fedha na rasilimali za taifa.

Viongozi wa Chadema wamewafafanulia haya wananchi; na wananchi wameelewa kuwa viongozi wengi wa sasa wanashindana kuiba dhahabu, alimasi, tanzanite, mbao na rasilimali nyingine.

Wamewafafanulia wananchi jinsi viongozi walivyoshiriki ufisadi wa kila aina; wakitoa mifano kadha wa kadha na kuoanisha nay ale wanayoona na kufahamu.

Uongo na kutosema ukweli; kutotekeleza ahadi kubwa na nzito kama kununua meli kwa matumizi katika Ziwa Victoria; kutokamata watuhumiwa wakuu wa ufisadi na tabia ya ndumila kuwili; vyote vimeelezwa kwa wananchi.

Katika mazingira ya kawaida, viongozi wa CCM wanahitaji ujasiri wa mwendawazimu kusimama mbele ya umati kueleza mafanikio, matarajio na kuomba umma kuunga mkono.

Wamewekwa uchi; wao na chama chao. Wamebakia kuanza na kumaliza mikutano yao kwa kusema “sasa tunajivua gamba.” Ndizo hotuba. Ndizo ahadi. Ndizo kinga za aibu.

Huwezi kusikia tena viongozi wa CCM wakitamba na “Ari zaidi, Nguvu zaidi na Kasi zaidi.” Wamezimika. Watani zao hutafsiri ashirio hilo kuwa ni kifupi cha “ANGUKA” na huko ndiko Chadema inahubiri kuwa wanaelekea.

Na ndani ya CCM kwenyewe mifarakano imeota ndevu. Ni piga nikupige. Kila anayefaulu kuchomoa kizinga anamchoma mwenzake.

Katika mazingira haya ndimo tunakuta: kamata mbowe, kamata Slaa. Kamata Zitto. Bambika masitaka. Weka rumande. Peleka mahakamani… Fungulia mashitaka… kama jana, kama leo, kama kesho, kila siku.

Mazingira haya yanaibua chuki. Yanaibua hasira. Yanachochea ujasiri wa kiwango cha juu wa kusema, “Hapana. Hatukubali tena kunyanyaswa.”……………..
………………………

……Habari zaidi katika MwanaHALISi ya leo uk 3.





 
Hivi leo ni jumatano eeeeh!
Dah mfuko umetoboka tayari...
 
Ukombozi waja… kipigo chayoyoma

Na Ndimara Tegambwage

Njia bora ya kuharakisha mabadiliko ya kisiasa nay a kiuchumi nchini Tanzania ni kubughudhi viongozi wa upinzani kila kukicha.

Kamata. Bambika mashitaka. Weka rumande. Peleka mahakamani… Achia kwa dhamana. Kamata. Weka rumande. Fungulia mashitaka…kama jana, kama leo, kama kesho, kila siku.

Wasimamizi wa mradi huu – wakipenyeza amri kwa watekelezaji – wanafikiri kwa njia hii, watafaulu kudhoofisha na hata kuua upinzani dhidi ya serikali chovu ya Chama cha Mapinduzi (CCM).

Polisi hawafurahii kukamata. Polisi wanafurahia kubaki na ajira yao. Kubaki na vimishahara vyao. Ni ya magwanda yao yanayoelekeza urefu wa kamba yao katika kujikimu.

Polisi wakamataji hawana masilahi katika kukamata viongozi wa upinzani. Wanatii amri ya wakubwa zao. Wakubwa wenye uswahiba na wakubwa siasani.

Wanaotumiwa kukamata hawana masilahi katika kufyatua risasi. Katika kulipua mabomu ya machozi. Katika kumimina maji-pilipili machono mwa wananchi. Hawana!

Ndani ya polisi nako kumejaa "Kabwela hana kitanda" – yule wa kwetu wanaita ndala omwa fulano – mtegemea fadhila!

Watawala wanatoa amri. Polisao wanatii amri. Watawala wanatoa amri kujilinda leo. Leo hii. Kufika au kutofika kesho so hoja kwao. Wanataka leo nay a leoleo.

Kwa hiyo kamata! Bambikia mashitaka. Weka rumande. Peleka mahakamani. Achia kwa dhamana. Kamata. Weka ruymande. Fungulia mashitaka… kama jana, kama leo, kama kesho, kila siku.

Chukua mfano wa Mbowe. Freeman wa Chadema. Kijana mdogo tu mwenye mdomo mpana uliojaa ushawishi.

Mbowe, kama Dk Willibrod Slaa na viongozi wengine wa Chadema, akilia wananchi wanaomsikiliza wanalia naye. Akicheka wanacheka naye. Akinuna wananuna naye. Watawala wanaamuru: kamata. Bambika mashitaka.

Chuykua mfano wa Chadema. Chama ambacho kimejidhihirishia kuwa na uwezo mkubwa wa kuwafikia wananchi, kuwaibua kutoka lindi la woga na ujinga.

Chukua mfano wa Chadema. Chama ambacho kimefuta umaarufu wa bandia wa CCM, kukinyang'anya wafuasi, kukibakizia wanafunzi wanaoswagwa na walimu wanaolinda ajira zao kama polisi.

Chukua mfano wa Chadema. Chama ambacho wengi wanasema mgombea wake wa urais alishinda na CCM inakiri nguvu yake ndani ya vikao na kwenye hadhara.

Chukua mfano wa umati wa wananchi unaojitokeza kwenye mikutano ya Chadema; maswali yanayoulizwa na wananchi na ahadi wanazotoa ili kuing'oa CCM

Fuatilkia kashifa lukuki zilizoizonga CCM na serikali yake; kushindwa kwa chama hicho kujibu hoja kuhusu wizi ndani ya benki kuu, kuhusu matumizi hewa; kuhusu mikataba ya kihuni nay a kinyonyaji.

Kazi ya kisiasa iliyofanywa na upinzani, hasa Chadema, CUF na NCCR-Mageuzi, imewezesha wananchi kuelewa kuwa CCM siyo chama cha siasa, ni chama cha ukwapuaji.

Kukua na hata kuimarika kwa vyama vbya upinzani, hasa Chadema hakutokani na ubora na umakini wa viongozi wake peke yake. Kunatokana pia na mazingira ya kutota kwa waliotawala kwa miaka 50.

Chadema wamepata fursa ya kuzunguka nchi na kueleza kuwa mataifa huadhimisha miaka 50 ya uhuru wake kwa kuonyesha utawala bora – kisiasa na kiuchumi.

Lakini katika Tanzania, hasa tunapokaribia kuadhimisha miaka 50, watawala ndio huionyesha walivyo na makucha marefu ya kupora fedha na rasilimali za taifa.

Viongozi wa Chadema wamewafafanulia haya wananchi; na wananchi wameelewa kuwa viongozi wengi wa sasa wanashindana kuiba dhahabu, alimasi, tanzanite, mbao na rasilimali nyingine.

Wamewafafanulia wananchi jinsi viongozi walivyoshiriki ufisadi wa kila aina; wakitoa mifano kadha wa kadha na kuoanisha nay ale wanayoona na kufahamu.

Uongo na kutosema ukweli; kutotekeleza ahadi kubwa na nzito kama kununua meli kwa matumizi katika Ziwa Victoria; kutokamata watuhumiwa wakuu wa ufisadi na tabia ya ndumila kuwili; vyote vimeelezwa kwa wananchi.

Katika mazingira ya kawaida, viongozi wa CCM wanahitaji ujasiri wa mwendawazimu kusimama mbele ya umati kueleza mafanikio, matarajio na kuomba umma kuunga mkono.

Wamewekwa uchi; wao na chama chao. Wamebakia kuanza na kumaliza mikutano yao kwa kusema "sasa tunajivua gamba." Ndizo hotuba. Ndizo ahadi. Ndizo kinga za aibu.

Huwezi kusikia tena viongozi wa CCM wakitamba na "Ari zaidi, Nguvu zaidi na Kasi zaidi." Wamezimika. Watani zao hutafsiri ashirio hilo kuwa ni kifupi cha "ANGUKA" na huko ndiko Chadema inahubiri kuwa wanaelekea.

Na ndani ya CCM kwenyewe mifarakano imeota ndevu. Ni piga nikupige. Kila anayefaulu kuchomoa kizinga anamchoma mwenzake.

Katika mazingira haya ndimo tunakuta: kamata mbowe, kamata Slaa. Kamata Zitto. Bambika masitaka. Weka rumande. Peleka mahakamani… Fungulia mashitaka… kama jana, kama leo, kama kesho, kila siku.

Mazingira haya yanaibua chuki. Yanaibua hasira. Yanachochea ujasiri wa kiwango cha juu wa kusema, "Hapana. Hatukubali tena kunyanyaswa."……………..
………………………

……Habari zaidi katika MwanaHALISi ya leo uk 3.






Hizo red nimezipenda sana.
 
Kuendelea kutumia polisi kuzima kauli,hakuwezi kubadili mwelekeo wa wananchi au hata wa polisi wenyewe;ule wakutaka mabadiliko
 
Ukombozi waja… kipigo chayoyoma

Na Ndimara Tegambwage

Njia bora ya kuharakisha mabadiliko ya kisiasa nay a kiuchumi nchini Tanzania ni kubughudhi viongozi wa upinzani kila kukicha.

Kamata. Bambika mashitaka. Weka rumande. Peleka mahakamani… Achia kwa dhamana. Kamata. Weka rumande. Fungulia mashitaka…kama jana, kama leo, kama kesho, kila siku.

Wasimamizi wa mradi huu – wakipenyeza amri kwa watekelezaji – wanafikiri kwa njia hii, watafaulu kudhoofisha na hata kuua upinzani dhidi ya serikali chovu ya Chama cha Mapinduzi (CCM).

Polisi hawafurahii kukamata. Polisi wanafurahia kubaki na ajira yao. Kubaki na vimishahara vyao. Ni ya magwanda yao yanayoelekeza urefu wa kamba yao katika kujikimu.

Polisi wakamataji hawana masilahi katika kukamata viongozi wa upinzani. Wanatii amri ya wakubwa zao. Wakubwa wenye uswahiba na wakubwa siasani.

Wanaotumiwa kukamata hawana masilahi katika kufyatua risasi. Katika kulipua mabomu ya machozi. Katika kumimina maji-pilipili machono mwa wananchi. Hawana!

Ndani ya polisi nako kumejaa "Kabwela hana kitanda" – yule wa kwetu wanaita ndala omwa fulano – mtegemea fadhila!

Watawala wanatoa amri. Polisao wanatii amri. Watawala wanatoa amri kujilinda leo. Leo hii. Kufika au kutofika kesho so hoja kwao. Wanataka leo nay a leoleo.

Kwa hiyo kamata! Bambikia mashitaka. Weka rumande. Peleka mahakamani. Achia kwa dhamana. Kamata. Weka ruymande. Fungulia mashitaka… kama jana, kama leo, kama kesho, kila siku.

Chukua mfano wa Mbowe. Freeman wa Chadema. Kijana mdogo tu mwenye mdomo mpana uliojaa ushawishi.

Mbowe, kama Dk Willibrod Slaa na viongozi wengine wa Chadema, akilia wananchi wanaomsikiliza wanalia naye. Akicheka wanacheka naye. Akinuna wananuna naye. Watawala wanaamuru: kamata. Bambika mashitaka.

Chuykua mfano wa Chadema. Chama ambacho kimejidhihirishia kuwa na uwezo mkubwa wa kuwafikia wananchi, kuwaibua kutoka lindi la woga na ujinga.

Chukua mfano wa Chadema. Chama ambacho kimefuta umaarufu wa bandia wa CCM, kukinyang'anya wafuasi, kukibakizia wanafunzi wanaoswagwa na walimu wanaolinda ajira zao kama polisi.

Chukua mfano wa Chadema. Chama ambacho wengi wanasema mgombea wake wa urais alishinda na CCM inakiri nguvu yake ndani ya vikao na kwenye hadhara.

Chukua mfano wa umati wa wananchi unaojitokeza kwenye mikutano ya Chadema; maswali yanayoulizwa na wananchi na ahadi wanazotoa ili kuing'oa CCM

Fuatilkia kashifa lukuki zilizoizonga CCM na serikali yake; kushindwa kwa chama hicho kujibu hoja kuhusu wizi ndani ya benki kuu, kuhusu matumizi hewa; kuhusu mikataba ya kihuni nay a kinyonyaji.

Kazi ya kisiasa iliyofanywa na upinzani, hasa Chadema, CUF na NCCR-Mageuzi, imewezesha wananchi kuelewa kuwa CCM siyo chama cha siasa, ni chama cha ukwapuaji.

Kukua na hata kuimarika kwa vyama vbya upinzani, hasa Chadema hakutokani na ubora na umakini wa viongozi wake peke yake. Kunatokana pia na mazingira ya kutota kwa waliotawala kwa miaka 50.

Chadema wamepata fursa ya kuzunguka nchi na kueleza kuwa mataifa huadhimisha miaka 50 ya uhuru wake kwa kuonyesha utawala bora – kisiasa na kiuchumi.

Lakini katika Tanzania, hasa tunapokaribia kuadhimisha miaka 50, watawala ndio huionyesha walivyo na makucha marefu ya kupora fedha na rasilimali za taifa.

Viongozi wa Chadema wamewafafanulia haya wananchi; na wananchi wameelewa kuwa viongozi wengi wa sasa wanashindana kuiba dhahabu, alimasi, tanzanite, mbao na rasilimali nyingine.

Wamewafafanulia wananchi jinsi viongozi walivyoshiriki ufisadi wa kila aina; wakitoa mifano kadha wa kadha na kuoanisha nay ale wanayoona na kufahamu.

Uongo na kutosema ukweli; kutotekeleza ahadi kubwa na nzito kama kununua meli kwa matumizi katika Ziwa Victoria; kutokamata watuhumiwa wakuu wa ufisadi na tabia ya ndumila kuwili; vyote vimeelezwa kwa wananchi.

Katika mazingira ya kawaida, viongozi wa CCM wanahitaji ujasiri wa mwendawazimu kusimama mbele ya umati kueleza mafanikio, matarajio na kuomba umma kuunga mkono.

Wamewekwa uchi; wao na chama chao. Wamebakia kuanza na kumaliza mikutano yao kwa kusema "sasa tunajivua gamba." Ndizo hotuba. Ndizo ahadi. Ndizo kinga za aibu.

Huwezi kusikia tena viongozi wa CCM wakitamba na "Ari zaidi, Nguvu zaidi na Kasi zaidi." Wamezimika. Watani zao hutafsiri ashirio hilo kuwa ni kifupi cha "ANGUKA" na huko ndiko Chadema inahubiri kuwa wanaelekea.

Na ndani ya CCM kwenyewe mifarakano imeota ndevu. Ni piga nikupige. Kila anayefaulu kuchomoa kizinga anamchoma mwenzake.

Katika mazingira haya ndimo tunakuta: kamata mbowe, kamata Slaa. Kamata Zitto. Bambika masitaka. Weka rumande. Peleka mahakamani… Fungulia mashitaka… kama jana, kama leo, kama kesho, kila siku.

Mazingira haya yanaibua chuki. Yanaibua hasira. Yanachochea ujasiri wa kiwango cha juu wa kusema, "Hapana. Hatukubali tena kunyanyaswa."……………..
………………………

……Habari zaidi katika MwanaHALISi ya leo uk 3.







Hapo penye highlight: ni kwqeli siku hizi hatusikii kabisa hiyo kauli mbiu. Nasikiavyo aliibuni yule Mihungo Rweyemamu, mwandishi aliyefukuzwa Mwananchi kwa kukosa maadili na kukimbilia kulamba viatu vya RA.

Kauli mbiu hiyo inawasuta CCM kwelikweli
 
Leo ni jumatano. Angalia tena kalenda yako. Isipokuwa kama unaishi Hawaii.

Jasusi wee kichaa kweli, nimeangalia hii line nimecheka sana kwa sababu ni joke iliyo na ukweli ndani yake. Richukuwe hiro ri-THANKS.
 
Sidhan wenzangu waliopiga kura ccm na hali hii ya maisha wanajisikiajeeeee
 
Kudos Ndimara! Kweli umeonyesha CCM ni finito -- inapumulia mashine, kama vile vile alivyotamka Tendwa hivi karibuni kuhusu hali ilivyokuwa wakati wa uchaguzi. Madudu yote haya wanayofanya CCM kwa kutrumia mapolisi wake ni kutapatapa. Na kama vile mtu anayetaka kuzama majini, huwa ni hatari sana anaweza kufanya lolote kujiokoa.

Please CCM -- tokomea peke yako uwaache Watz kwa salama.
 
hahahah, hichi kipande kweli kabisa bwana..ccm hawana jipya,sio kisera wala utendaji

"Wamewekwa uchi; wao na chama chao. Wamebakia kuanza na kumaliza mikutano yao kwa kusema "sasa tunajivua gamba." Ndizo hotuba. Ndizo ahadi. Ndizo kinga za aibu."
 
Ukombozi waja… kipigo chayoyoma

Na Ndimara Tegambwage

Njia bora ya kuharakisha mabadiliko ya kisiasa nay a kiuchumi nchini Tanzania ni kubughudhi viongozi wa upinzani kila kukicha.

Kamata. Bambika mashitaka. Weka rumande. Peleka mahakamani… Achia kwa dhamana. Kamata. Weka rumande. Fungulia mashitaka…kama jana, kama leo, kama kesho, kila siku.

Wasimamizi wa mradi huu – wakipenyeza amri kwa watekelezaji – wanafikiri kwa njia hii, watafaulu kudhoofisha na hata kuua upinzani dhidi ya serikali chovu ya Chama cha Mapinduzi (CCM).

Polisi hawafurahii kukamata. Polisi wanafurahia kubaki na ajira yao. Kubaki na vimishahara vyao. Ni ya magwanda yao yanayoelekeza urefu wa kamba yao katika kujikimu.

Polisi wakamataji hawana masilahi katika kukamata viongozi wa upinzani. Wanatii amri ya wakubwa zao. Wakubwa wenye uswahiba na wakubwa siasani.

Wanaotumiwa kukamata hawana masilahi katika kufyatua risasi. Katika kulipua mabomu ya machozi. Katika kumimina maji-pilipili machono mwa wananchi. Hawana!

Ndani ya polisi nako kumejaa "Kabwela hana kitanda" – yule wa kwetu wanaita ndala omwa fulano – mtegemea fadhila!

Watawala wanatoa amri. Polisao wanatii amri. Watawala wanatoa amri kujilinda leo. Leo hii. Kufika au kutofika kesho so hoja kwao. Wanataka leo nay a leoleo.

Kwa hiyo kamata! Bambikia mashitaka. Weka rumande. Peleka mahakamani. Achia kwa dhamana. Kamata. Weka ruymande. Fungulia mashitaka… kama jana, kama leo, kama kesho, kila siku.

Chukua mfano wa Mbowe. Freeman wa Chadema. Kijana mdogo tu mwenye mdomo mpana uliojaa ushawishi.

Mbowe, kama Dk Willibrod Slaa na viongozi wengine wa Chadema, akilia wananchi wanaomsikiliza wanalia naye. Akicheka wanacheka naye. Akinuna wananuna naye. Watawala wanaamuru: kamata. Bambika mashitaka.

Chuykua mfano wa Chadema. Chama ambacho kimejidhihirishia kuwa na uwezo mkubwa wa kuwafikia wananchi, kuwaibua kutoka lindi la woga na ujinga.

Chukua mfano wa Chadema. Chama ambacho kimefuta umaarufu wa bandia wa CCM, kukinyang'anya wafuasi, kukibakizia wanafunzi wanaoswagwa na walimu wanaolinda ajira zao kama polisi.

Chukua mfano wa Chadema. Chama ambacho wengi wanasema mgombea wake wa urais alishinda na CCM inakiri nguvu yake ndani ya vikao na kwenye hadhara.

Chukua mfano wa umati wa wananchi unaojitokeza kwenye mikutano ya Chadema; maswali yanayoulizwa na wananchi na ahadi wanazotoa ili kuing'oa CCM

Fuatilkia kashifa lukuki zilizoizonga CCM na serikali yake; kushindwa kwa chama hicho kujibu hoja kuhusu wizi ndani ya benki kuu, kuhusu matumizi hewa; kuhusu mikataba ya kihuni nay a kinyonyaji.

Kazi ya kisiasa iliyofanywa na upinzani, hasa Chadema, CUF na NCCR-Mageuzi, imewezesha wananchi kuelewa kuwa CCM siyo chama cha siasa, ni chama cha ukwapuaji.

Kukua na hata kuimarika kwa vyama vbya upinzani, hasa Chadema hakutokani na ubora na umakini wa viongozi wake peke yake. Kunatokana pia na mazingira ya kutota kwa waliotawala kwa miaka 50.

Chadema wamepata fursa ya kuzunguka nchi na kueleza kuwa mataifa huadhimisha miaka 50 ya uhuru wake kwa kuonyesha utawala bora – kisiasa na kiuchumi.

Lakini katika Tanzania, hasa tunapokaribia kuadhimisha miaka 50, watawala ndio huionyesha walivyo na makucha marefu ya kupora fedha na rasilimali za taifa.

Viongozi wa Chadema wamewafafanulia haya wananchi; na wananchi wameelewa kuwa viongozi wengi wa sasa wanashindana kuiba dhahabu, alimasi, tanzanite, mbao na rasilimali nyingine.

Wamewafafanulia wananchi jinsi viongozi walivyoshiriki ufisadi wa kila aina; wakitoa mifano kadha wa kadha na kuoanisha nay ale wanayoona na kufahamu.

Uongo na kutosema ukweli; kutotekeleza ahadi kubwa na nzito kama kununua meli kwa matumizi katika Ziwa Victoria; kutokamata watuhumiwa wakuu wa ufisadi na tabia ya ndumila kuwili; vyote vimeelezwa kwa wananchi.

Katika mazingira ya kawaida, viongozi wa CCM wanahitaji ujasiri wa mwendawazimu kusimama mbele ya umati kueleza mafanikio, matarajio na kuomba umma kuunga mkono.

Wamewekwa uchi; wao na chama chao. Wamebakia kuanza na kumaliza mikutano yao kwa kusema "sasa tunajivua gamba." Ndizo hotuba. Ndizo ahadi. Ndizo kinga za aibu.

Huwezi kusikia tena viongozi wa CCM wakitamba na "Ari zaidi, Nguvu zaidi na Kasi zaidi." Wamezimika. Watani zao hutafsiri ashirio hilo kuwa ni kifupi cha "ANGUKA" na huko ndiko Chadema inahubiri kuwa wanaelekea.

Na ndani ya CCM kwenyewe mifarakano imeota ndevu. Ni piga nikupige. Kila anayefaulu kuchomoa kizinga anamchoma mwenzake.

Katika mazingira haya ndimo tunakuta: kamata mbowe, kamata Slaa. Kamata Zitto. Bambika masitaka. Weka rumande. Peleka mahakamani… Fungulia mashitaka… kama jana, kama leo, kama kesho, kila siku.

Mazingira haya yanaibua chuki. Yanaibua hasira. Yanachochea ujasiri wa kiwango cha juu wa kusema, "Hapana. Hatukubali tena kunyanyaswa."……………..
………………………

……Habari zaidi katika MwanaHALISi ya leo uk 3.







Hivi CCM kuna mtu mwenye akili timamu wa kusoma alama za nyakati zilizopo na kutoa tafsiri sahii kwa chama chao? hakika hayupo kwa maana hiyo lazima wa kabiliwe na mauti.......................
 
Safari bado ni ndefu ya kulisogeza taifa hili karibu na mataifa yaliojijengea heshima kwa wananchi wake, kwa mtaji huu wa CCM hatufiki.tumedumaa.
 
Ukombozi waja… kipigo chayoyoma

Na Ndimara Tegambwage

Njia bora ya kuharakisha mabadiliko ya kisiasa nay a kiuchumi nchini Tanzania ni kubughudhi viongozi wa upinzani kila kukicha.

Kamata. Bambika mashitaka. Weka rumande. Peleka mahakamani… Achia kwa dhamana. Kamata. Weka rumande. Fungulia mashitaka…kama jana, kama leo, kama kesho, kila siku.

Wasimamizi wa mradi huu – wakipenyeza amri kwa watekelezaji – wanafikiri kwa njia hii, watafaulu kudhoofisha na hata kuua upinzani dhidi ya serikali chovu ya Chama cha Mapinduzi (CCM).

Polisi hawafurahii kukamata. Polisi wanafurahia kubaki na ajira yao. Kubaki na vimishahara vyao. Ni ya magwanda yao yanayoelekeza urefu wa kamba yao katika kujikimu.

Polisi wakamataji hawana masilahi katika kukamata viongozi wa upinzani. Wanatii amri ya wakubwa zao. Wakubwa wenye uswahiba na wakubwa siasani.

Wanaotumiwa kukamata hawana masilahi katika kufyatua risasi. Katika kulipua mabomu ya machozi. Katika kumimina maji-pilipili machono mwa wananchi. Hawana!

Ndani ya polisi nako kumejaa “Kabwela hana kitanda” – yule wa kwetu wanaita ndala omwa fulano – mtegemea fadhila!

Watawala wanatoa amri. Polisao wanatii amri. Watawala wanatoa amri kujilinda leo. Leo hii. Kufika au kutofika kesho so hoja kwao. Wanataka leo nay a leoleo.

Kwa hiyo kamata! Bambikia mashitaka. Weka rumande. Peleka mahakamani. Achia kwa dhamana. Kamata. Weka ruymande. Fungulia mashitaka… kama jana, kama leo, kama kesho, kila siku.

Chukua mfano wa Mbowe. Freeman wa Chadema. Kijana mdogo tu mwenye mdomo mpana uliojaa ushawishi.

Mbowe, kama Dk Willibrod Slaa na viongozi wengine wa Chadema, akilia wananchi wanaomsikiliza wanalia naye. Akicheka wanacheka naye. Akinuna wananuna naye. Watawala wanaamuru: kamata. Bambika mashitaka.

Chuykua mfano wa Chadema. Chama ambacho kimejidhihirishia kuwa na uwezo mkubwa wa kuwafikia wananchi, kuwaibua kutoka lindi la woga na ujinga.

Chukua mfano wa Chadema. Chama ambacho kimefuta umaarufu wa bandia wa CCM, kukinyang’anya wafuasi, kukibakizia wanafunzi wanaoswagwa na walimu wanaolinda ajira zao kama polisi.

Chukua mfano wa Chadema. Chama ambacho wengi wanasema mgombea wake wa urais alishinda na CCM inakiri nguvu yake ndani ya vikao na kwenye hadhara.

Chukua mfano wa umati wa wananchi unaojitokeza kwenye mikutano ya Chadema; maswali yanayoulizwa na wananchi na ahadi wanazotoa ili kuing’oa CCM

Fuatilkia kashifa lukuki zilizoizonga CCM na serikali yake; kushindwa kwa chama hicho kujibu hoja kuhusu wizi ndani ya benki kuu, kuhusu matumizi hewa; kuhusu mikataba ya kihuni nay a kinyonyaji.

Kazi ya kisiasa iliyofanywa na upinzani, hasa Chadema, CUF na NCCR-Mageuzi, imewezesha wananchi kuelewa kuwa CCM siyo chama cha siasa, ni chama cha ukwapuaji.

Kukua na hata kuimarika kwa vyama vbya upinzani, hasa Chadema hakutokani na ubora na umakini wa viongozi wake peke yake. Kunatokana pia na mazingira ya kutota kwa waliotawala kwa miaka 50.

Chadema wamepata fursa ya kuzunguka nchi na kueleza kuwa mataifa huadhimisha miaka 50 ya uhuru wake kwa kuonyesha utawala bora – kisiasa na kiuchumi.

Lakini katika Tanzania, hasa tunapokaribia kuadhimisha miaka 50, watawala ndio huionyesha walivyo na makucha marefu ya kupora fedha na rasilimali za taifa.

Viongozi wa Chadema wamewafafanulia haya wananchi; na wananchi wameelewa kuwa viongozi wengi wa sasa wanashindana kuiba dhahabu, alimasi, tanzanite, mbao na rasilimali nyingine.

Wamewafafanulia wananchi jinsi viongozi walivyoshiriki ufisadi wa kila aina; wakitoa mifano kadha wa kadha na kuoanisha nay ale wanayoona na kufahamu.

Uongo na kutosema ukweli; kutotekeleza ahadi kubwa na nzito kama kununua meli kwa matumizi katika Ziwa Victoria; kutokamata watuhumiwa wakuu wa ufisadi na tabia ya ndumila kuwili; vyote vimeelezwa kwa wananchi.

Katika mazingira ya kawaida, viongozi wa CCM wanahitaji ujasiri wa mwendawazimu kusimama mbele ya umati kueleza mafanikio, matarajio na kuomba umma kuunga mkono.

Wamewekwa uchi; wao na chama chao. Wamebakia kuanza na kumaliza mikutano yao kwa kusema “sasa tunajivua gamba.” Ndizo hotuba. Ndizo ahadi. Ndizo kinga za aibu.

Huwezi kusikia tena viongozi wa CCM wakitamba na “Ari zaidi, Nguvu zaidi na Kasi zaidi.” Wamezimika. Watani zao hutafsiri ashirio hilo kuwa ni kifupi cha “ANGUKA” na huko ndiko Chadema inahubiri kuwa wanaelekea.

Na ndani ya CCM kwenyewe mifarakano imeota ndevu. Ni piga nikupige. Kila anayefaulu kuchomoa kizinga anamchoma mwenzake.

Katika mazingira haya ndimo tunakuta: kamata mbowe, kamata Slaa. Kamata Zitto. Bambika masitaka. Weka rumande. Peleka mahakamani… Fungulia mashitaka… kama jana, kama leo, kama kesho, kila siku.

Mazingira haya yanaibua chuki. Yanaibua hasira. Yanachochea ujasiri wa kiwango cha juu wa kusema, “Hapana. Hatukubali tena kunyanyaswa.”……………..
………………………

……Habari zaidi katika MwanaHALISi ya leo uk 3.






Ndimara kashusha mistari ya ukweli.
 
Kufaidi zaidi ni kulipata mwanahalisi lote la leo kama lilivyo na sio vipande
 
Back
Top Bottom