Elections 2010 Mwanahalisi leo lamfukua Salma kuhusu ndege

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
233
[B]Wana_JF:
Toleo la leo la Mwanahalisi ni moto wa kuotea mbali. Limekwenda hadi mvunguni na kuanika uongo uliokubuhu alioutoa Mwenyekiti wa Kampeni za CCM, Abdulrahmani Kinana kuhusu ‘ukodishwaji' wa ndege za serikali kwa matumizi ya kampeni za CCM zilizofanywa na mke wa Rais, Salma Kikwete.

Gazeti hilo limethibitisha ‘risiti' (invoice) zilizotolewa na Kinana mbele ya waandishi wa habari wiki iliyopita ni feki – zilighushiwa na maafisa wa CCM wakishirikiana na baadhi ya wale wa serikali.

Kikubwa katika ‘risiti' hizo ni kasoro kubwa katika namna zilivyojazwa – kwamba zilionyesha fedha hizo zinazokusanywa na kitengo cha Wakala wa Ndege za Serikali (za ukodishaji ndege) zinaingizwa katika Vote Na 062 na Sub Vote 087, wakati katika mipangilio ya mahesabu ya serikali hakuna kabisa vifungu hivyo vya mpangilio vya fedha.

Nikipata soft copy ya stori hii nitawawekeeni hapa
.

[/B]
 
Wana_JF:
Toleo la leo la Mwanahalisi ni moto wa kuotea mbali. Limekwenda hadi mvunguni na kuanika uongo uliokubuhu alioutoa Mwenyekiti wa Kampeni za CCM, Abdulrahmani Kinana kuhusu ‘ukodishwaji' wa ndege za serikali kwa matumizi ya kampeni za CCM zilizofanywa na mke wa Rais, Salma Kikwete.

Gazeti hilo limethibitisha ‘risiti' (invoice) zilizotolewa na Kinana mbele ya waandishi wa habari wiki iliyopita ni feki – zilighushiwa na maafisa wa CCM wakishirikiana na baadhi ya wale wa serikali.

Kikubwa katika ‘risiti' hizo ni kasoro kubwa katika namna zilivyojazwa – kwamba zilionyesha fedha hizo zinazokusanywa na kitengo cha Wakala wa Ndege za Serikali (za ukodishaji ndege) zinaingizwa katika Vote Na 062 na Sub Vote 087, wakati katika mipangilio ya mahesabu ya serikali hakuna kabisa vifungu hivyo vya mpangilio vya fedha.

Nikipata soft copy ya stori hii nitawawekeeni hapa.

I knew it. The said docs came up too swift and were so good to be true!! It's a big SHAME!!!!!
 
Mkuu, umeandika topic nzuri; sawa ila ume-bold na wakati font ni kubwa basi ni shida hata haisomeki vizuri. Sijui kama tatizo ni kwangu au na kwa wengine! Kama vipi rekebisha font ya 'content' ya topic yako!
 
Naomba Nitambulishe Singo yangu itakayozinduliwa mwanzoni mwa mwezi november.

chorus:
Kanyagaaaa!, kanyaga! (Kanyaga)
Kanyagaaaa!, kanyaga! (kanyaga)
Kanyaga FISADI Kanyaga (Kanyaga)
Kanyaga JK kanyaga (kanyaga)
kanyaga Makamba (kanyaga)
 
hata siku zile Kinana alivyokuwa akitetea hiyo hoja tuu alikuwa akiongea kwa kutojiamini huku akijua kweli sicho anachokitetea wana JF mkichunguza sana kinana mtamgundua kabisa anapo ongea mbele ya vyombo vya habari uta mgundua mapema kwa anachokiongelea sana sana anapo jibu tuhuma hubabaika sana na kusita sita na kurudia maneno na zile eeeh jamni eeeh eeeh nyingi na suru humshuka.
 
Mkuu, umeandika topic nzuri; sawa ila ume-bold na wakati font ni kubwa basi ni shida hata haisomeki vizuri. Sijui kama tatizo ni kwangu au na kwa wengine! Kama vipi rekebisha font ya 'content' ya topic yako!

Una tatizo na COMPUTER yako,jaribu kuwasiliana na mafundi wakuongezee Font size ya pc yako.

Zac Malang,umenena ukweli,gazeti si mchezo ninalo hapa.
Mambo ni mazito haya.sijui wataamuaje,yetu macho,Tendwa ajiuzulu kwanza kama mfano kwanza kuonesha nguvu aliyonayo DR WA KWELI.
 
Naomba Nitambulishe Singo yangu itakayozinduliwa mwanzoni mwa mwezi november.

chorus:
Kanyagaaaa!, kanyaga! (Kanyaga)
Kanyagaaaa!, kanyaga! (kanyaga)
Kanyaga FISADI Kanyaga (Kanyaga)
Kanyaga JK kanyaga (kanyaga)
kanyaga Makamba (kanyaga)

Itarudisha gharama za wewe kupoteza muda wa kufikiria???? nadhani uitoe mapema maana huko november mmmmh ni mbali sana, watanzania si wepesi wa kusahauuu jamani

 
Mkuu, umeandika topic nzuri; sawa ila ume-bold na wakati font ni kubwa basi ni shida hata haisomeki vizuri. Sijui kama tatizo ni kwangu au na kwa wengine! Kama vipi rekebisha font ya 'content' ya topic yako!

Ongelea mada mkubwa, hakuna shida na font, unless kama wewe umehitimu kwenye m asuala hayo!.....................................................................................................................................Zile risiti za Kinana zilistukiwa just from Day One!, maana kama ni Agency ya serikali walitakiwa kutumia risiti za serikali, tofauti na zile za kughushi!...........................Mwisho wa dhuluma ni aibu!...Sasa ikithibitika kuwa wamefanya fodgery, je watakuwa wamekiuka sheria ya gharama za uchaguzi, au Mama Salma yeye hahusiki na suala hilo kwa vile si mgombea?...more news is awaited!
 
Fanya faster mkuu, mie niko mbali sana na ninaisubiri hiyo soft copy kwa shauku kubwa maana mwaka huu mimi na familia yangu kwa ujumla tunasema HATUDANGANYIIIIIIIKII
 
Hamna chochote kitakachofanyika hata kama uongo ni wa wazi kabisa. Kinana alitumwa kutekeleza tu sababu akili yake inavutwa na harufu ya madaraka asijerudishwa Somalia. Kila anapotetea hoja hujaza mate mdomoni akifoka kwa hofu asije akaonekana hakutetea ipasavyo.

Lakini hiyo ndiyo hulka na labda sera ya chama chao, maana angalia bosi wake alivyo ndumila kuwili. Anauma na kupuliza ilimradi anataka apate anachotaka. Alipoenda Monduli kamfagilia kwa sana rafiki yake kipenzi LOwasa akiwaambia watu wasahau yaliyopita wampe kura Lowasa. Alipoenda kwa Mramba akamfagilia kwamba ni mwaminifu kupindukia, watu wake wampe kura tu, lakini akiwaacha hoi wanarombo imekuwaje alisaini hati ya kushitakiwa mwaminifu wake huyo ambako hadi leo anaburuzwa na kesi hiyo. Hatujakaa sawa kaenda Iringa anamfagilia Mwakalebela ati ni kiongozi bora huyo. Na Mwakalebela bila kulaza damu asijekosa ukuu wa wilaya, akaanika meno yooooote 45.5 mdomoni akifurahia kukumbatiwa na kusahau haki yake ya kimsingi aliyonyimwa, ati anavunja makundi.

Watanzania bora kuwachukulia wote hao kama sehemu ya tatizo la ufisadi. aonyeshe hasira zao siku ya kupiga kura na kulinyima kabisa dudu lolote linaloweza kuuma vidole vyetu. Warombo wampe Mramba lakini wamnyime kura Vuvuzela, Kinana anyimwe pia. Wanyalukolo wasidanganyike, wawape wapinzani kura zao. Bwana huyu kila anapopita anatoa ahadi lukuki anasahau kwamba miaka mitano iliyopita alifanya hivyohivyo na akaishia kupanda mapipa kwenda ulaya na marekani akiwaacha wanaosubiri ahadi ulimi nje.
 
tunashukuru kwa singo tamuj
Naomba Nitambulishe Singo yangu itakayozinduliwa mwanzoni mwa mwezi november.

chorus:
Kanyagaaaa!, kanyaga! (Kanyaga)
Kanyagaaaa!, kanyaga! (kanyaga)
Kanyaga FISADI Kanyaga (Kanyaga)
Kanyaga JK kanyaga (kanyaga)
kanyaga Makamba (kanyaga)
 
Hapa sasa mimi nitaona ni upumbavu kama wakala wa ndege za serikali hatasema lolote kuhusiana na hilo, waandishi fuatilieni huko pia waoneshe kitabu cha risiti hizo kama kweli zimetoka kwao. Wallah hawa jamaa mwakani wavae bangili za chuma tu, Mh. Rais Dr W. Slaa ukiwaacha hawa jamaa na trupu yao nzima ya maNgumbaru utakuwa hujawatendea haki watanzania!:mad2::mad2::mad2::mad2::mad2::mad2::mad2::mad2::mad2::mad2::mad2::mad2::mad2:
Hawa watu wanastahili kunyongwa! Nawasifu sana wachina.
 
Mkuu, umeandika topic nzuri; sawa ila ume-bold na wakati font ni kubwa basi ni shida hata haisomeki vizuri. Sijui kama tatizo ni kwangu au na kwa wengine! Kama vipi rekebisha font ya 'content' ya topic yako!

Nimerekebisha Mzee.
 
Mkuu, umeandika topic nzuri; sawa ila ume-bold na wakati font ni kubwa basi ni shida hata haisomeki vizuri. Sijui kama tatizo ni kwangu au na kwa wengine! Kama vipi rekebisha font ya 'content' ya topic yako!

Nimerekebisha Mzee.
 
wasi wasi wangu ni kuwa nakala kwa watu wa mikoani ambako internet nako ni shida
 
Hamna chochote kitakachofanyika hata kama uongo ni wa wazi kabisa. Kinana alitumwa kutekeleza tu sababu akili yake inavutwa na harufu ya madaraka asijerudishwa Somalia. Kila anapotetea hoja hujaza mate mdomoni akifoka kwa hofu asije akaonekana hakutetea ipasavyo.

Lakini hiyo ndiyo hulka na labda sera ya chama chao, maana angalia bosi wake alivyo ndumila kuwili. Anauma na kupuliza ilimradi anataka apate anachotaka. Alipoenda Monduli kamfagilia kwa sana rafiki yake kipenzi LOwasa akiwaambia watu wasahau yaliyopita wampe kura Lowasa. Alipoenda kwa Mramba akamfagilia kwamba ni mwaminifu kupindukia, watu wake wampe kura tu, lakini akiwaacha hoi wanarombo imekuwaje alisaini hati ya kushitakiwa mwaminifu wake huyo ambako hadi leo anaburuzwa na kesi hiyo. Hatujakaa sawa kaenda Iringa anamfagilia Mwakalebela ati ni kiongozi bora huyo. Na Mwakalebela bila kulaza damu asijekosa ukuu wa wilaya, akaanika meno yooooote 45.5 mdomoni akifurahia kukumbatiwa na kusahau haki yake ya kimsingi aliyonyimwa, ati anavunja makundi.

Watanzania bora kuwachukulia wote hao kama sehemu ya tatizo la ufisadi. aonyeshe hasira zao siku ya kupiga kura na kulinyima kabisa dudu lolote linaloweza kuuma vidole vyetu. Warombo wampe Mramba lakini wamnyime kura Vuvuzela, Kinana anyimwe pia. Wanyalukolo wasidanganyike, wawape wapinzani kura zao. Bwana huyu kila anapopita anatoa ahadi lukuki anasahau kwamba miaka mitano iliyopita alifanya hivyohivyo na akaishia kupanda mapipa kwenda ulaya na marekani akiwaacha wanaosubiri ahadi ulimi nje.

...Umenena Vyema. Baada ya maneno kama haya ya kumsafisha Mramba ni wazi kuwa hakuna Hakimu atakayethubutu kumtia hatiani Mramba. Kesi itapigwa kalenda wee, na mwanzoni mwa mwaka kesho itafutwa kwa kukosekana ushahidi. Mark my Words.
 
Mimi nilijua tu from the very beginning Kinana alipoitisha mkutano wa haraka haraka na waandishi wa habari kukanusha tuhuma hizo huku akiwa na hizo fake receipts akizionyesha kwa waandishi. Ulikuwa ni UONGO WA MCHANA KWEUPE!

Hivi kwanini CCM wanatufanya sisi Watanzania kuwa ni wajinga,wapumbavu,tusio na akili na kwamba CCM wanaweza wakakaa na kutunga uongo halafu wanawatangazia dunia nzima kuwa ni ukweli.

We're fed up na CCM. Kinana anatakiwa aachie ngazi na wale maafisa wote wa Serikali walioshirikiana naye wajiuzulu mara moja. Kujiuzulu peke yake haitoshi inabidi wakamatwe na washtakiwe mahakamani kwasababu KUGHUSHI NI KOSA LA JINAI!
Hatuwezi kuvumilia propaganda za kihuni zinazotumiwa na CCM kujaribu kuwalaghai Watanzania na ilhali wanaujua ukweli.

Njia nzuri ya KUWA ADHIBU CCM ni KUWANYIMA KURA siku ya uchaguzi. Shhhhhhnzzz kabsa,Pambaf!!1
 
Muda unakwisha. Msaidieni Dr Slaa hoja nzito za kuiondoa CCM madarakani. Mwanahalisi anauza tu gazeti leo.
 
Back
Top Bottom