"Mwanahalisi toleo namba 249".......Kiongozi huyo wa nchi (Kikwete), mtoa taarifa anasema, ana simu tatu za mkononi ambazo anatembea nazo kila anakopita; jambo linalomfanya kupokea umbea kutoka kwa wasaidizi na maswahiba wake.
Hata Mkapa (rais mstaafu Benjamin Mkapa) alikuwa na simu ya mkononi. Lakini simu ya Mkapa ilikuwa ya kupiga tu. Ilikuwa huwezi kumpata Mkapa kwenye simu yake ya mkononi, hadi yeye akupigie, anaeleza kigogo mmoja wa ikulu ambaye alikuwa karibu na Mkapa.
Anasema, Hata mawaziri wake walikuwa hawawezi kuongea naye kupitia simu yake ya mkononi. Simu ya Mkapa ilikuwa kwa mawasiliano ya watu wasiozidi sita wakiwamo watoto wake wawili na mkewe.
Anasema hadi sasa, Mkapa anamiliki simu ya mkononi, lakini huwezi kumpata hadi yeye akupigie. Ile ni simu ya yeye kukupigia, si wewe kumpigia. Ni tofauti na Kikwete. Huyu bwana amegawa namba yake ya simu kwa watu ambao wengine wanaitumia kumpelekea umbeya, anaeleza.
Anasema simu ya Rais Kikwete inapokea ujumbe wa kila mmoja na kuna wakati yeye hujibu ujumbe aliotumiwa usiku wa manane. Anahoji, Sasa katika mazingira hayo, rais anapata wapi muda wa kupumzika na kusoma nyaraka?
Gazeti hili liliwahi kuchapisha ujumbe wa simu uliodaiwa kutoka kwa Rais Kikwete kwenda kwa aliyekuwa mbunge wa Viti Maalum, Amina Chifupa aliyekuwa ameomba ushauri wa kisiasa kwa rais Kikwete.Amina aliusambaza ujumbe uliotoka kwa rais kwa watu mbalimbali akiwamo Zitto Kabwe na Emmanuel Nchimbi.
Hata Mkapa (rais mstaafu Benjamin Mkapa) alikuwa na simu ya mkononi. Lakini simu ya Mkapa ilikuwa ya kupiga tu. Ilikuwa huwezi kumpata Mkapa kwenye simu yake ya mkononi, hadi yeye akupigie, anaeleza kigogo mmoja wa ikulu ambaye alikuwa karibu na Mkapa.
Anasema, Hata mawaziri wake walikuwa hawawezi kuongea naye kupitia simu yake ya mkononi. Simu ya Mkapa ilikuwa kwa mawasiliano ya watu wasiozidi sita wakiwamo watoto wake wawili na mkewe.
Anasema hadi sasa, Mkapa anamiliki simu ya mkononi, lakini huwezi kumpata hadi yeye akupigie. Ile ni simu ya yeye kukupigia, si wewe kumpigia. Ni tofauti na Kikwete. Huyu bwana amegawa namba yake ya simu kwa watu ambao wengine wanaitumia kumpelekea umbeya, anaeleza.
Anasema simu ya Rais Kikwete inapokea ujumbe wa kila mmoja na kuna wakati yeye hujibu ujumbe aliotumiwa usiku wa manane. Anahoji, Sasa katika mazingira hayo, rais anapata wapi muda wa kupumzika na kusoma nyaraka?
Gazeti hili liliwahi kuchapisha ujumbe wa simu uliodaiwa kutoka kwa Rais Kikwete kwenda kwa aliyekuwa mbunge wa Viti Maalum, Amina Chifupa aliyekuwa ameomba ushauri wa kisiasa kwa rais Kikwete.Amina aliusambaza ujumbe uliotoka kwa rais kwa watu mbalimbali akiwamo Zitto Kabwe na Emmanuel Nchimbi.