Ngongo
JF-Expert Member
- Sep 20, 2008
- 18,894
- 31,103
Gazeti la MwanaHalisi toleo Na,172 tarehe 20 - 26 January,2010 kichwa cha habari "Mramba aingiza Meghji matatani" inapaswa kupuuzwa kwasababu haina ukweli wowote.
Mwandishi wa habari hii Bwana Ezekiel Kamwanga katuletea habari bila kufanya utafiti wa kutosha,kuna mambo matatu makubwa ambayo nimeyaona hayajakaa vizuri.
[1] Bwana Ezekiel kwa maksudi anajaribu kudanganya wasomaji wake kwamba General Tyre ilipata mkopo wa 10 bilion mwaka 2007 kitu ambacho si kweli hata kidogo.General Tyre ilipata mkopo wa u$ 10 milioni kutoka NSSF serekali ikiwa mdhamini mwaka 2005 hadi kufikia mwezi december 2005 fedha zote tayari zilikuwa zimeshaliwa.General Tyre ilijaribu kupata mkopo mwingine wa u$ 3 milion mwaka 2007 lakini hawakufanikiwa.
[2]Aliyeidhinsha mkopo wa General Tyre ni B P Mramba wakati huo alikuwa waziri wa fedha Bi Z Maghji alikuwa waziri wa utali na malialisi.kwa lugha rahisi Bi Maghji kwenye hili dili la u$ 10 Milioni hakuhusika kabisa.
[3]Mheshimiwa Z maghji alipokuwa waziri wa fedha alizuia mkopo mwingine wa u$ 3 milioni kwenda general Tyre ambao waziri mkuu wa wakati huo Mheshimiwa E Lowassa na waziri wa Viwanda,biashara na masoko Mheshimiwa B P Mramba walishinikiza zitolewe lakini Bi Maghji akisaidiwa kwa kiasi kikubwa na mkurugenzi wa viwanda Bi Pallangyo walikataa kutoa fedha hadi board na managemant ya General Tyre watakapotoa maelezo ya kina namna fedha za mwanzo [u$10 mil] zilivyotumika kitu ambacho kilishindikana kufanyika.Najua Mama meghji ana madhaifu yake lakini katika suala la General Tyre alisimama kidete na alikuwa akisikiliza na kuzingatia ushauri wa wataalamu.Mama Meghji aliweza kuzuia upotevu wa u$ 3 milioni kama angewasikiliza Mheshimiwa Lowassa na Mramba.
Mwandishi wa habari hii Bwana Ezekiel Kamwanga katuletea habari bila kufanya utafiti wa kutosha,kuna mambo matatu makubwa ambayo nimeyaona hayajakaa vizuri.
[1] Bwana Ezekiel kwa maksudi anajaribu kudanganya wasomaji wake kwamba General Tyre ilipata mkopo wa 10 bilion mwaka 2007 kitu ambacho si kweli hata kidogo.General Tyre ilipata mkopo wa u$ 10 milioni kutoka NSSF serekali ikiwa mdhamini mwaka 2005 hadi kufikia mwezi december 2005 fedha zote tayari zilikuwa zimeshaliwa.General Tyre ilijaribu kupata mkopo mwingine wa u$ 3 milion mwaka 2007 lakini hawakufanikiwa.
[2]Aliyeidhinsha mkopo wa General Tyre ni B P Mramba wakati huo alikuwa waziri wa fedha Bi Z Maghji alikuwa waziri wa utali na malialisi.kwa lugha rahisi Bi Maghji kwenye hili dili la u$ 10 Milioni hakuhusika kabisa.
[3]Mheshimiwa Z maghji alipokuwa waziri wa fedha alizuia mkopo mwingine wa u$ 3 milioni kwenda general Tyre ambao waziri mkuu wa wakati huo Mheshimiwa E Lowassa na waziri wa Viwanda,biashara na masoko Mheshimiwa B P Mramba walishinikiza zitolewe lakini Bi Maghji akisaidiwa kwa kiasi kikubwa na mkurugenzi wa viwanda Bi Pallangyo walikataa kutoa fedha hadi board na managemant ya General Tyre watakapotoa maelezo ya kina namna fedha za mwanzo [u$10 mil] zilivyotumika kitu ambacho kilishindikana kufanyika.Najua Mama meghji ana madhaifu yake lakini katika suala la General Tyre alisimama kidete na alikuwa akisikiliza na kuzingatia ushauri wa wataalamu.Mama Meghji aliweza kuzuia upotevu wa u$ 3 milioni kama angewasikiliza Mheshimiwa Lowassa na Mramba.