Mwanafunzi kulipwa zaidi ya mfanyakazi wa kima cha chini!!

Ms Judith

JF-Expert Member
Dec 24, 2010
2,563
918
Posho elimu ya juu yapanda kwa Sh 2,500/-

SERIKALI itaongeza fedha za kujikimu kwa wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu nchini kutoka Sh. 5,000 ya sasa hadi Sh. 7,500 katika mwaka huu wa fedha.

Kauli hiyo ilitolewa bungeni jana na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, Dk. Shukuru Kawambwa, alipokuwa akisoma hotuba yake ya Makadirio ya Matumizi ya Fedha kwa Wizara yake kwa mwaka huu.

Alisema, kiasi cha Sh. bilioni 77.8 kitatumika kwa suala hilo na wanafunzi 91,568 wa elimu ya juu wa mwaka wa kwanza na wanaoendelea na masomo na kwa wanaosoma shahada za uzamili na uzamivu, wanatarajiwa kupewa mikopo kwa mwaka 2011/12.

Alisema katika mwaka huu wa fedha, Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) itaimarisha utoaji na urejeshaji wa mikopo kwa kuainisha taarifa za wakopeshwaji na zile za Tume ya Vyuo Vikuu, Baraza la Mitihani na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa.

Alisema pia Bodi hiyo itasogeza huduma za utoaji mikopo karibu na wananchi kwa kuanzisha ofisi ya kanda Zanzibar.

Akisoma maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii kuhusu wizara hiyo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Margaret Sitta , alisema ili kuimarisha uwezo wa Serikali kuendelea kutoa mikopo kwa wanafunzi, Kamati yake ilishauri Serikali itafute mbinu mbadala za kupata fedha ili kuinua uwezo wa kutoa mikopo mwaka hadi mwaka.

Alisema, ili kuimarisha urejeshwaji wa mikopo iliyotolewa tangu mwaka 2006, kiundwe chombo mahususi chini ya Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu, ili kufuatilia ukusanywaji wa marejesho ya mikopo iliyokwishatolewa.

Alisema, taarifa za mikopo husika zitambulike kwa walengwa ili kurahisisha ukusanyaji wa fedha hizo kwa ushirikiano wa mwajiri na Bodi ya Mikopo na kuwa fedha za marejesho ya mikopo hiyo zitambulike bayana, kwa kuonekana katika taarifa ya utekelezaji wa majukumu kila mwaka.

Pia Kamati ilishauri utoaji vitambulisho vya Taifa ukamilike ili kutambua wanafunzi wanaokopa na waliokopa na uraia wao, ambapo pia Kamati ilishauri kuwapo udhibiti wa karo hasa katika vyuo visivyo vya Serikali.

Mbunge wa Viti Maalumu, Diana Chilolo (CCM), alishauri kutokana na utata katika urejeshwaji wa mikopo, Serikali itoe fedha hizo bure kwa wanafunzi badala ya kuwakopesha.

Akiwasilisha maoni ya Kambi ya Upinzani, Msemaji Mkuu wa Kambi hiyo kwa Wizara ya hiyo Cristowaja Mtinda, alisema kutokana na muundo wa Bodi ya Mikopo na uendeshaji mbaya, kuna haja ikavunjwa kwani imeshindwa kuifanya elimu ya juu ipatikane kwa kila mwanafunzi anayestahili.

Alisema Bodi hiyo ilitoa mikopo kwa wanafunzi 91,568 mwaka uliopita, lakini ilikusanya marejesho ya mikopo yenye thamani ya Sh. bilioni 7.9 kati ya Sh. bilioni 21 zilizotarajiwa kukusanywa.

“Kutokana na sababu hizo, Serikali iazimie kuivunja Bodi hii, pamoja na kufanya uchunguzi huru wa fedha zilizotumika chini yake hadi sasa na kujiridhisha kama waliopewa dhamana hii hawakutumia nafasi zao kujinufaisha binafsi,” alisema.

Alisema baada ya Bodi hiyo kuvunjwa, Serikali iunde chombo kipya kitakachojulikana kama Mamlaka ya Taifa ya Kugharimia Elimu ya Juu (TAHEFA), ambacho kitachukua majukumu yote ya Bodi.

chanzo: HabariLeo | Posho elimu ya juu yapanda kwa Sh 2,500/-
 
Ni ongezeko la 50% tu bila shaka kima cha chini kitaongezeka kwa zaidi ya 50% unless the government applies the irrational decisions.
 
Mwanafunzi posho 7500 * 30 = 225,000


Mfanyakazi wa serikali: Net Salary 200,000
  1. Kodi ya nyumba
  2. Ada za Watoto
  3. Chakula cha familia
  4. Matibabu
  5. Umeme na Maji ...................................
Kufanya kazi bongo yataka uzalendo wa hali ya juu.
Afadhali ya Mkopo wa Chuo.
 
Ni ongezeko la 50% tu bila shaka kima cha chini kitaongezeka kwa zaidi ya 50% unless the government applies the irrational decisions.

soma hii

Nimepata habari za uhakika kutoka kwa Mkuu wangu wa kitengo cha rasilimali watu(Head of Human Resource-HHR) kuwa ongezeko la mshahara kwa wafanyakazi wa serikali ni asilimia kumi na moja(11%) kwa kima cha chini na asilimia nane nukta sita(8.6%) kwa wengine wote.

Kwa hiyo kama mtu alikuwa akipata mshahara wa Tsh 135,000 ataongezewa kwa 11% atapata Tsh 149,850 ikiwa ni ongezeko la Tsh 14,850 na yule aliyekuwa mathalani akipata mshahara wa Tsh 520,000 ataongezewa kwa 8.6% atapata Tsh 564,720 ikiwa ni ongezeko la Tsh 44,720.

My Take:
Habari ndiyo hiyo,naona serikali inafanya dhihaka,watu tumesubiri ongezeko la mishahara tukategemea tutapata angalau asilimia 30 lakini wameleta siasa.Kwa ongezeko hili maisha yetu yatazidi kuwa magumu ukizingatia kuwa bei ya mafuta ya dizeli na petroli haishuki ,mafuta ya taa yameongezwa bei na umeme ndio huo wa mgao uuwwiiiiiiii!!!!

inapatikana hapa: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-la-mshahara-kwa-wafanyakazi-wa-serikali.html
 
Mwanafunzi posho 7500 * 30 = 225,000


Mfanyakazi wa serikali: Net Salary 200,000
  1. Kodi ya nyumba
  2. Ada za Watoto
  3. Chakula cha familia
  4. Matibabu
  5. Umeme na Maji ...................................
Kufanya kazi bongo yataka uzalendo wa hali ya juu.
Afadhali ya Mkopo wa Chuo.

mkuu, hiyo net ya 200,000/- wanapata wangapi? hebu soma post #4 nne hapo juu kuna nyepesi nyepesi
 
Mie yangu macho. Mtazamo wangu, tuangalie pia elimu ya huyo anayepokea kima cha chini serikalini.
 
Miss Judith hujambo dada!

Kwa mtindo huu hata sie wazee wa siku nyingi itabidi tujifanye wanafunzi ili tupate udhamini wa serikali.

Ndio maana hata mtoto wa rais anaishi kimjini mjini maana Tsh 149,850 utafanyia nini jamani kama sio kututia majaribuni kuomba rushwa.
Ni heri Tsh 225,000 ya mwanafunzi ambayo hana pressure ya maisha
 
Miss Judith hujambo dada!

Kwa mtindo huu hata sie wazee wa siku nyingi itabidi tujifanye wanafunzi ili tupate udhamini wa serikali.

Ndio maana hata mtoto wa rais anaishi kimjini mjini maana Tsh 149,850 utafanyia nini jamani kama sio kututia majaribuni kuomba rushwa.
Ni heri Tsh 225,000 ya mwanafunzi ambayo hana pressure ya maisha

mi sijambo kabisa mpendwa,

kwa kweli mambo mengine yanashangaza sana! imagine huyo mwanafunzi analelewa na mzazi mlezi aliyeko kwenye category ya kima cha chini, ina maana anamzidi kipato mzazi/mlezi wake anayemlea na cha kushangaza, chanzo cha mapato yao ni kimoja, SERIKALI!
 
Mwanafunzi posho 7500 * 30 = 225,000


Mfanyakazi wa serikali: Net Salary 200,000
  1. Kodi ya nyumba
  2. Ada za Watoto
  3. Chakula cha familia
  4. Matibabu
  5. Umeme na Maji ...................................
Kufanya kazi bongo yataka uzalendo wa hali ya juu.
Afadhali ya Mkopo wa Chuo.

Bila ya kuwa mwizi au mdokozi kwa mshahara huo huwezi kuendesha maisha na ukayafrahia
 
Mie yangu macho. Mtazamo wangu, tuangalie pia elimu ya huyo anayepokea kima cha chini serikalini.

mwanafunzi akiwa chuoni kabla hajahitimu huwa ana elimu gani? kama ana elimu ya sekondari inashawishi kuwa ni haki amzidi mzazi/mlezi wake mwenye limu ya sekondari kama yeye na aliyeko kazini?
 
Kama serikali imeona ya kuwa sh. 5,000 haimtoshi mwanafunzi wa chuo. Imeshindwa nini kuona ugumu wa maisha ya mfanyakazi wake mwenye familia.

Huyo mfanyakazi mwenye familia hajui kuandamana kuishinikiza serikali, inaonyesha anaridhika na hicho kipato kiduchu dili nyingi mtaani anapiga
 
mi sijambo kabisa mpendwa,

kwa kweli mambo mengine yanashangaza sana! imagine huyo mwanafunzi analelewa na mzazi mlezi aliyeko kwenye category ya kima cha chini, ina maana anamzidi kipato mzazi/mlezi wake anayemlea na cha kushangaza, chanzo cha mapato yao ni kimoja, SERIKALI!

Pasipo imani ni vigumu kuishi Tanzania.

Serikali na taasisi zake ina baadhi ya watumishi watumishi wanakula na kusaza ili hali wengine wengi wakiangukia kwenye chini ya dola moja kwa siku.
 
Posho elimu ya juu yapanda kwa Sh 2,500/-

SERIKALI itaongeza fedha za kujikimu kwa wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu nchini kutoka Sh. 5,000 ya sasa hadi Sh. 7,500 katika mwaka huu wa fedha.

Kauli hiyo ilitolewa bungeni jana na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, Dk. Shukuru Kawambwa, alipokuwa akisoma hotuba yake ya Makadirio ya Matumizi ya Fedha kwa Wizara yake kwa mwaka huu.

Alisema, kiasi cha Sh. bilioni 77.8 kitatumika kwa suala hilo na wanafunzi 91,568 wa elimu ya juu wa mwaka wa kwanza na wanaoendelea na masomo na kwa wanaosoma shahada za uzamili na uzamivu, wanatarajiwa kupewa mikopo kwa mwaka 2011/12.

Alisema katika mwaka huu wa fedha, Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) itaimarisha utoaji na urejeshaji wa mikopo kwa kuainisha taarifa za wakopeshwaji na zile za Tume ya Vyuo Vikuu, Baraza la Mitihani na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa.

Alisema pia Bodi hiyo itasogeza huduma za utoaji mikopo karibu na wananchi kwa kuanzisha ofisi ya kanda Zanzibar.

Akisoma maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii kuhusu wizara hiyo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Margaret Sitta , alisema ili kuimarisha uwezo wa Serikali kuendelea kutoa mikopo kwa wanafunzi, Kamati yake ilishauri Serikali itafute mbinu mbadala za kupata fedha ili kuinua uwezo wa kutoa mikopo mwaka hadi mwaka.

Alisema, ili kuimarisha urejeshwaji wa mikopo iliyotolewa tangu mwaka 2006, kiundwe chombo mahususi chini ya Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu, ili kufuatilia ukusanywaji wa marejesho ya mikopo iliyokwishatolewa.

Alisema, taarifa za mikopo husika zitambulike kwa walengwa ili kurahisisha ukusanyaji wa fedha hizo kwa ushirikiano wa mwajiri na Bodi ya Mikopo na kuwa fedha za marejesho ya mikopo hiyo zitambulike bayana, kwa kuonekana katika taarifa ya utekelezaji wa majukumu kila mwaka.

Pia Kamati ilishauri utoaji vitambulisho vya Taifa ukamilike ili kutambua wanafunzi wanaokopa na waliokopa na uraia wao, ambapo pia Kamati ilishauri kuwapo udhibiti wa karo hasa katika vyuo visivyo vya Serikali.

Mbunge wa Viti Maalumu, Diana Chilolo (CCM), alishauri kutokana na utata katika urejeshwaji wa mikopo, Serikali itoe fedha hizo bure kwa wanafunzi badala ya kuwakopesha.

Akiwasilisha maoni ya Kambi ya Upinzani, Msemaji Mkuu wa Kambi hiyo kwa Wizara ya hiyo Cristowaja Mtinda, alisema kutokana na muundo wa Bodi ya Mikopo na uendeshaji mbaya, kuna haja ikavunjwa kwani imeshindwa kuifanya elimu ya juu ipatikane kwa kila mwanafunzi anayestahili.

Alisema Bodi hiyo ilitoa mikopo kwa wanafunzi 91,568 mwaka uliopita, lakini ilikusanya marejesho ya mikopo yenye thamani ya Sh. bilioni 7.9 kati ya Sh. bilioni 21 zilizotarajiwa kukusanywa.

"Kutokana na sababu hizo, Serikali iazimie kuivunja Bodi hii, pamoja na kufanya uchunguzi huru wa fedha zilizotumika chini yake hadi sasa na kujiridhisha kama waliopewa dhamana hii hawakutumia nafasi zao kujinufaisha binafsi," alisema.

Alisema baada ya Bodi hiyo kuvunjwa, Serikali iunde chombo kipya kitakachojulikana kama Mamlaka ya Taifa ya Kugharimia Elimu ya Juu (TAHEFA), ambacho kitachukua majukumu yote ya Bodi.

chanzo: HabariLeo | Posho elimu ya juu yapanda kwa Sh 2,500/-

Miss J .. kumbuka hizi fedha wakopeshwa... toka bodi ya mikopo... so usijali kuhusu fedha wapewazo....
 
Huo si mkopo tu.......utarudishwa tu jamani!!!!!!!!!!!!!!



Miss J .. kumbuka hizi fedha wakopeshwa... toka bodi ya mikopo... so usijali kuhusu fedha wapewazo....

Basi ni vema na waalimu nao wapewe hii mikopo isiyokuwa na riba..., Hapa issue sio kwamba wanafunzi wanapata pesa nyingi.., issue ni kwamba waalimu hawapewi fedha za kutosha. Sasa kama serikali imetambua kwamba pesa hizo hazimtoshi mwanafunzi kujikimu, iweje idhani kwamba pesa pungufu ya hizo inamtosha mwalimu tena mwenye familia na majukumu zaidi?

Bad enough ni kwamba huenda huyo huyo mwanafunzi atakuja kuwa mwalimu baadae.., so how are you preparing him for the future..., si huku ndio kuhalalisha rushwa...?, cause people have got to eat
 
Back
Top Bottom