Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,720
- 21,779
Mwanafunzi kizimbani kwa tuhuma za kutupa kichanga Send to a friend Wednesday, 29 September 2010 09:17 0diggsdigg
Joseph Lyimo, Mbulu
JESHI la Polisi mkoani Manyara linamshikilia mwanafunzi wa kidato cha nne wa Shule ya sekondari Genda, wilayani Mbulu kwa tuhuma ya kukitupa kitoto kichanga ****** baada ya kuzaa.
Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Parmena Sumary, mwanafunzi huyo ambaye hakutajwa jina lake anadaiwa kutupa kichanga hicho Septemba 23 saa 6:30 mchana.
Sumary alisema kichanga hicho kiliokotwa na mtu mmoja kikiwa kizima wakati akipita karibu na choo hicho.
Alisema baada ya kukiokota kichanga hicho mtu huyo alikipeleka hospitali ya wilaya hiyo kitoto hicho na jeshi hilo lilifanikiwa kumkamata mwanafunzi huyo.
Mwanafunzi huyo alikiri kufanya kitendo hicho cha kutupa mtoto kwa madai kuwa alifanya hivyo ili aweze kufanya mtihani wa kuhitimu kidato cha nne utakaofanyika mwezi Oktoba.
Kamanda Sumary alisema mwanafunzi huyo atafikishwa mahakamani muda wowote mara baada ya kutoka hospitalini hapo ambapo hadi hivi sasa amelazwa.
Joseph Lyimo, Mbulu
JESHI la Polisi mkoani Manyara linamshikilia mwanafunzi wa kidato cha nne wa Shule ya sekondari Genda, wilayani Mbulu kwa tuhuma ya kukitupa kitoto kichanga ****** baada ya kuzaa.
Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Parmena Sumary, mwanafunzi huyo ambaye hakutajwa jina lake anadaiwa kutupa kichanga hicho Septemba 23 saa 6:30 mchana.
Sumary alisema kichanga hicho kiliokotwa na mtu mmoja kikiwa kizima wakati akipita karibu na choo hicho.
Alisema baada ya kukiokota kichanga hicho mtu huyo alikipeleka hospitali ya wilaya hiyo kitoto hicho na jeshi hilo lilifanikiwa kumkamata mwanafunzi huyo.
Mwanafunzi huyo alikiri kufanya kitendo hicho cha kutupa mtoto kwa madai kuwa alifanya hivyo ili aweze kufanya mtihani wa kuhitimu kidato cha nne utakaofanyika mwezi Oktoba.
Kamanda Sumary alisema mwanafunzi huyo atafikishwa mahakamani muda wowote mara baada ya kutoka hospitalini hapo ambapo hadi hivi sasa amelazwa.