Mwanafunzi kizimbani kwa tuhuma za kutupa kichanga

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,720
21,779
Mwanafunzi kizimbani kwa tuhuma za kutupa kichanga Send to a friend Wednesday, 29 September 2010 09:17 0diggsdigg

Joseph Lyimo, Mbulu

JESHI la Polisi mkoani Manyara linamshikilia mwanafunzi wa kidato cha nne wa Shule ya sekondari Genda, wilayani Mbulu kwa tuhuma ya kukitupa kitoto kichanga ****** baada ya kuzaa.

Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Parmena Sumary, mwanafunzi huyo ambaye hakutajwa jina lake anadaiwa kutupa kichanga hicho Septemba 23 saa 6:30 mchana.

Sumary alisema kichanga hicho kiliokotwa na mtu mmoja kikiwa kizima wakati akipita karibu na choo hicho.

Alisema baada ya kukiokota kichanga hicho mtu huyo alikipeleka hospitali ya wilaya hiyo kitoto hicho na jeshi hilo lilifanikiwa kumkamata mwanafunzi huyo.

Mwanafunzi huyo alikiri kufanya kitendo hicho cha kutupa mtoto kwa madai kuwa alifanya hivyo ili aweze kufanya mtihani wa kuhitimu kidato cha nne utakaofanyika mwezi Oktoba.


Kamanda Sumary alisema mwanafunzi huyo atafikishwa mahakamani muda wowote mara baada ya kutoka hospitalini hapo ambapo hadi hivi sasa amelazwa.
 
Mwanafunzi kizimbani kwa tuhuma za kutupa kichanga Send to a friend Wednesday, 29 September 2010 09:17 0diggsdigg

Joseph Lyimo, Mbulu

JESHI la Polisi mkoani Manyara linamshikilia mwanafunzi wa kidato cha nne wa Shule ya sekondari Genda, wilayani Mbulu kwa tuhuma ya kukitupa kitoto kichanga ****** baada ya kuzaa.

Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Parmena Sumary, mwanafunzi huyo ambaye hakutajwa jina lake anadaiwa kutupa kichanga hicho Septemba 23 saa 6:30 mchana.

Sumary alisema kichanga hicho kiliokotwa na mtu mmoja kikiwa kizima wakati akipita karibu na choo hicho.

Alisema baada ya kukiokota kichanga hicho mtu huyo alikipeleka hospitali ya wilaya hiyo kitoto hicho na jeshi hilo lilifanikiwa kumkamata mwanafunzi huyo.

Mwanafunzi huyo alikiri kufanya kitendo hicho cha kutupa mtoto kwa madai kuwa alifanya hivyo ili aweze kufanya mtihani wa kuhitimu kidato cha nne utakaofanyika mwezi Oktoba.


Kamanda Sumary alisema mwanafunzi huyo atafikishwa mahakamani muda wowote mara baada ya kutoka hospitalini hapo ambapo hadi hivi sasa amelazwa.

Inasikitisha sana kwa kiumbe ambacho hakina kosa kutelekezwa. Jambo la Msingi wampe huyo mwanafunzi ruhusa ya kufanya mitihani na baada ya mitihani ndio kesi yake iendelee. Ni mawazo yangu.
 
Inaonyesha haja ya msingi ya kutokukatisha elimu ya wanaopatwa na janga hili.

Mabinti wakijua hawaachishwi shule pengine baadhi ya watoto watasalimika kutupwa.
 
Elimu mbofu, Afya mbofu, Mazingira mbofu. We need change. Chagua SLAA 2010.
 
Elimu mbofu, Afya mbofu, Mazingira mbofu. We need change. Chagua SLAA 2010.
nasikitika kutoelewa hii post... sijui slaa atasababishaje watoto wadifanye mapenzi kabla ya muda na bila kinga??

the problem is systemic and we need to address it comprehensively na sio kisiasa-siasa with one or two sweeping statements
 
Back
Top Bottom