Mwanafunzi China auwawa kwa kuchomwa kisu

engmtolera

JF-Expert Member
Oct 21, 2010
5,150
1,437
NDUGU wana Jf,habari
napenda niwape habari iliyotokea saa moja lililopita,kuwa hapa china Yangling katika chuo nisomacho NORTHWEST A&F UNIVERSITY mwanafunzi kutoka Bangradeshi ameuwauwa na raia wa kichina kwa kuchomwa kisu,mwanafunzi huyo ameuwawa chumbani kwake bwenini wakati akiwa anajiandaa na mtihani kesho,Ndugu wana jf tupo ktk mazingira magumu kwani watanzania hapa tupo wawili mmoja anatokea Moshi na mimi natokea Morogoro,hivyo tunaomba mjue kuwa chochote chaweza tokea kwa sisi ndugu zenu tulio hapa china
hii ni taarifa tu nawaomba wapeni taarifa na ndugu zetu walio china ktk vyuo vingine wajihadhari na hili


mapinduzi daimaaaaaa
 
Poleni sana. Muwe waangalifu na epukeni mambo yanayoweza kuwaweka katika mgongano na wenyeji wenu.
 
Thadharini na wabangaladeshi na watu kutoka maeneo ya Pakistani hao ni kama hawana akili vizuri ,wao ni hasira tu na hawachagui cha kukupiga kama ni kisu au shoka chochote kilichopo karibu basi kwake ni silaha ya maangamizi,na zaidi hawajui au hawana time ya kupigana kwa ngumi sijui urushe kichwa ,wao ni watu wa kutumia njia za mkato kumaliza mapigano au ugonvi ,kesi baadae maana hawajali kufa kutokana na shida za nchini kwao. Na wengine wasomali maana hawa ukimtizama tu na akikushitukia kama unamdeku basi ujue ni vita na maswali kibao. Hao wachina sio watu wa ugonvi lazima kutakuwa na jambo tu,sasa huko imekuwa kuviziana ,hebu tafuta sababu tuone.
 
NDUGU wana Jf,habari
napenda niwape habari iliyotokea saa moja lililopita,kuwa hapa china Yangling katika chuo nisomacho NORTHWEST A&F UNIVERSITY mwanafunzi kutoka Bangradeshi ameuwauwa na raia wa kichina kwa kuchomwa kisu,mwanafunzi huyo ameuwawa chumbani kwake bwenini wakati akiwa anajiandaa na mtihani kesho,Ndugu wana jf tupo ktk mazingira magumu kwani watanzania hapa tupo wawili mmoja anatokea Moshi na mimi natokea Morogoro,hivyo tunaomba mjue kuwa chochote chaweza tokea kwa sisi ndugu zenu tulio hapa china
hii ni taarifa tu nawaomba wapeni taarifa na ndugu zetu walio china ktk vyuo vingine wajihadhari na hili


mapinduzi daimaaaaaa

Poleni sana ila kwa experience ya nje ya nchi nakushauri kama alivyokushauri Jasusi kuwa muwe waangalifu na wenyeji mara nyingi ni wivu, tabia na visasi kwa unavyojua culture za nchi zinatofautiana sana kwako jambo unaweza kuliona dogo kumbe ni tusi kwao. Pia kama kumetokea hivyo ni bora kama mnatoka chuo muwe pamoja maana inasaidia saa zengine.
 
Muwe waangalifu, especially na mabinti wa huko..
Tumepoteza wengi e.g. kule Urusi kutokana na wivu wa kimapenzi wanaokuwanao wenyeji
 
ndugu wana jf,habari
napenda niwape habari iliyotokea saa moja lililopita,kuwa hapa china yangling katika chuo nisomacho northwest a&f university mwanafunzi kutoka bangradeshi ameuwauwa na raia wa kichina kwa kuchomwa kisu,mwanafunzi huyo ameuwawa chumbani kwake bwenini wakati akiwa anajiandaa na mtihani kesho,ndugu wana jf tupo ktk mazingira magumu kwani watanzania hapa tupo wawili mmoja anatokea moshi na mimi natokea morogoro,hivyo tunaomba mjue kuwa chochote chaweza tokea kwa sisi ndugu zenu tulio hapa china
hii ni taarifa tu nawaomba wapeni taarifa na ndugu zetu walio china ktk vyuo vingine wajihadhari na hili


mapinduzi daimaaaaaa

mbona hukutueleza chanzo cha mauaji hayo ni nini? Kindly do some investigation a bit ili utujuze
 
mbona hukutueleza chanzo cha mauaji hayo ni nini? Kindly do some investigation a bit ili utujuze

Watanzania always ni wapole sana hutasikia mwanafunzi yeyote wa kigeni ameuawa hapa Tanzania iwe kwa wivu wa kimapenzi wala mambo mengine may be iwe bahati mbaya sana ila kweli kwa wenzetu nchi hasa za westers europe na Asia hawapendi kabisa wageni jitahidini sana muwe mnachukua tahadhari mara zote hasa kwenye madisco,clubs na kutembea usiku pia kutembea mchana pekeyenu!muwe macho na hilo!ila sasa nashangaa tukio hili mtu kafuatwa chumbani ni hostel au alikua anaishi mtaani
 
napenda kutoa taarifa kwa mujibu wa taarifa za kiintelijensia kama ifuatavyo:
wasifu wa jamaa alikuwa ni mwanafunzi wa Phd. na alikuwa nimpole naasiye na maneno mengi sana pindi uongeapo na mtu mwenyekujali muda wake na masomo. siku ya tukio inasemekana alikuwa chumbani kwake na huyo muuaji wa kichina alikuwa akipita na kugonga gonga milango ili afunguliwe, lakini alipofika mlango wa mwisho kwenye chumba cha mwsho cha mrehemu alivunja mlango na kuingia. Marehemu aliyekuwa anaishi gorofa inavyoonekana alifanikiwa kumkimbia muuaji(mchina) na kukimbilia gorofa ya 3 akiomba msaada huku akikimbizwa na huyo mtoaroho(mchina). Bahati yake ilikuwa mbaya kwani hakukua na watu imara wakuweza kuzuia tukio hilo kutokana na muuwaji kuwa na kisu nakuanza kumshambulia mbaghaladeshi wa watu mpaka kumuua. Kisha mchina huyo alisikika akisema 我杀了他
(l killed him) na kama unaweza njoo na wewe nikuuwe alisikika hivyo.
Baada ya tukio hilo ilichukua muda wa 30min kwa wahusika police kufika eneo la tukio bila ya ambulance kwaajili ya kumchukuwa mtu huyo kwenda huspitali kwasababu tulihisi kama angekuwa bado anauzima, lakini ilichukuwa kama muda wa masaa matatu nakuona mwili ikitole na police ukiwa umefunikwa nakutoweka nao kwaharaka kwenda kuhifadhiwa hospital.
Hii ndiyo taarifa ya private intelligence agent(me)
 
napenda kutoa taarifa kwa mujibu wa taarifa za kiintelijensia kama ifuatavyo:
wasifu wa jamaa alikuwa ni mwanafunzi wa Phd. na alikuwa nimpole naasiye na maneno mengi sana pindi uongeapo na mtu mwenyekujali muda wake na masomo. siku ya tukio inasemekana alikuwa chumbani kwake na huyo muuaji wa kichina alikuwa akipita na kugonga gonga milango ili afunguliwe, lakini alipofika mlango wa mwisho kwenye chumba cha mwsho cha mrehemu alivunja mlango na kuingia. Marehemu aliyekuwa anaishi gorofa inavyoonekana alifanikiwa kumkimbia muuaji(mchina) na kukimbilia gorofa ya 3 akiomba msaada huku akikimbizwa na huyo mtoaroho(mchina). Bahati yake ilikuwa mbaya kwani hakukua na watu imara wakuweza kuzuia tukio hilo kutokana na muuwaji kuwa na kisu nakuanza kumshambulia mbaghaladeshi wa watu mpaka kumuua. Kisha mchina huyo alisikika akisema 我杀了他
(l killed him) na kama unaweza njoo na wewe nikuuwe alisikika hivyo.
Baada ya tukio hilo ilichukua muda wa 30min kwa wahusika police kufika eneo la tukio bila ya ambulance kwaajili ya kumchukuwa mtu huyo kwenda huspitali kwasababu tulihisi kama angekuwa bado anauzima, lakini ilichukuwa kama muda wa masaa matatu nakuona mwili ikitole na police ukiwa umefunikwa nakutoweka nao kwaharaka kwenda kuhifadhiwa hospital.
Hii ndiyo taarifa ya private intelligence agent(me)

mimi nimeshawaasa sana waafrika wenzangu kuhusu hili, waache kutembea ovyo kwenye maclub na sehemu zote za starehe na mazingira hatarishi. Waafrika wengi wamekufa kutokana na ajali au kama yalivyomkuta huyo jamaa, polisi wa nje wakisikia ni muafrika basi watakuja baada ya 30 mins which is too late.. na ukifika hospital ktk nchi za far east nyingi wakiona muafrika wanakunyanyapaa mpk unakufa. Wengi wamepotea kwa njia hizi yani hata kama una hela hazikusaidii
 
napenda kutoa taarifa kwa mujibu wa taarifa za kiintelijensia kama ifuatavyo:
wasifu wa jamaa alikuwa ni mwanafunzi wa Phd. na alikuwa nimpole naasiye na maneno mengi sana pindi uongeapo na mtu mwenyekujali muda wake na masomo. siku ya tukio inasemekana alikuwa chumbani kwake na huyo muuaji wa kichina alikuwa akipita na kugonga gonga milango ili afunguliwe, lakini alipofika mlango wa mwisho kwenye chumba cha mwsho cha mrehemu alivunja mlango na kuingia. Marehemu aliyekuwa anaishi gorofa inavyoonekana alifanikiwa kumkimbia muuaji(mchina) na kukimbilia gorofa ya 3 akiomba msaada huku akikimbizwa na huyo mtoaroho(mchina). Bahati yake ilikuwa mbaya kwani hakukua na watu imara wakuweza kuzuia tukio hilo kutokana na muuwaji kuwa na kisu nakuanza kumshambulia mbaghaladeshi wa watu mpaka kumuua. Kisha mchina huyo alisikika akisema 我杀了他
(l killed him) na kama unaweza njoo na wewe nikuuwe alisikika hivyo.
Baada ya tukio hilo ilichukua muda wa 30min kwa wahusika police kufika eneo la tukio bila ya ambulance kwaajili ya kumchukuwa mtu huyo kwenda huspitali kwasababu tulihisi kama angekuwa bado anauzima, lakini ilichukuwa kama muda wa masaa matatu nakuona mwili ikitole na police ukiwa umefunikwa nakutoweka nao kwaharaka kwenda kuhifadhiwa hospital.
Hii ndiyo taarifa ya private intelligence agent(me)

hujasema bado,sababu hasa ni ipi iliyomfanya huyo mchina kuua?kujua chanzo cha ugomvi wao ndiyo muhimu ili iwe fundisho kwenu mnaoishi huko china na hata nchi nyingine pia
 
NDUGU wana Jf,habari
napenda niwape habari iliyotokea saa moja lililopita,kuwa hapa china Yangling katika chuo nisomacho NORTHWEST A&F UNIVERSITY mwanafunzi kutoka Bangradeshi ameuwauwa na raia wa kichina kwa kuchomwa kisu,mwanafunzi huyo ameuwawa chumbani kwake bwenini wakati akiwa anajiandaa na mtihani kesho,Ndugu wana jf tupo ktk mazingira magumu kwani watanzania hapa tupo wawili mmoja anatokea Moshi na mimi natokea Morogoro,hivyo tunaomba mjue kuwa chochote chaweza tokea kwa sisi ndugu zenu tulio hapa china
hii ni taarifa tu nawaomba wapeni taarifa na ndugu zetu walio china ktk vyuo vingine wajihadhari na hili


mapinduzi daimaaaaaa

Xiongdi bui bu qi ...
 
POLENI sana ndugu zetu, chukueni tahadhali. Huyo muuaji ni mwanafunzi mwenzenu na je kesha kamatwa, au kaishia ki namna?
 
POLENI sana ndugu zetu, chukueni tahadhali. Huyo muuaji ni mwanafunzi mwenzenu na je kesha kamatwa, au kaishia ki namna?
alisubiri aje kukamatwa na alikamatwa, akipelekwa huku akilia, sijui kilichoendelea tena. lakini nahisi, atafikishwa kunakoshahili na hatimaye kunyongwa. mwiho wa kuwasilisha
 
Tumekuwa tukisikia katika vyombo vya habari Wachina wakiua watu bila sababu huko China. Tumesikia wakati fulani mmoja alivamia sule ya chekechekea na kuanza kuchama watoto visu. Nadhani waningiwa na ukichaa fulani hivi.
 
Hii habari tija yake ni nini? mbangladeshe na watanzania wawili katika hicho chuo nk? then! alafu ipo Jukwaa la Siasa?! Moderators mnakula karanga na watoto wa mtendeni tu au mko nyuma ya pazia!
 
Hii habari tija yake ni nini? mbangladeshe na watanzania wawili katika hicho chuo nk? then! alafu ipo Jukwaa la Siasa?! Moderators mnakula karanga na watoto wa mtendeni tu au mko nyuma ya pazia!

ni mbwembwe tu za mtoa mada.
Poleni sana jamani.
Huyo mchina amechukuliwa hatua gani?
 
napenda kutoa taarifa kwa mujibu wa taarifa za kiintelijensia kama ifuatavyo:
wasifu wa jamaa alikuwa ni mwanafunzi wa Phd. na alikuwa nimpole naasiye na maneno mengi sana pindi uongeapo na mtu mwenyekujali muda wake na masomo. siku ya tukio inasemekana alikuwa chumbani kwake na huyo muuaji wa kichina alikuwa akipita na kugonga gonga milango ili afunguliwe, lakini alipofika mlango wa mwisho kwenye chumba cha mwsho cha mrehemu alivunja mlango na kuingia. Marehemu aliyekuwa anaishi gorofa inavyoonekana alifanikiwa kumkimbia muuaji(mchina) na kukimbilia gorofa ya 3 akiomba msaada huku akikimbizwa na huyo mtoaroho(mchina). Bahati yake ilikuwa mbaya kwani hakukua na watu imara wakuweza kuzuia tukio hilo kutokana na muuwaji kuwa na kisu nakuanza kumshambulia mbaghaladeshi wa watu mpaka kumuua. Kisha mchina huyo alisikika akisema 我杀了他
(l killed him) na kama unaweza njoo na wewe nikuuwe alisikika hivyo.
Baada ya tukio hilo ilichukua muda wa 30min kwa wahusika police kufika eneo la tukio bila ya ambulance kwaajili ya kumchukuwa mtu huyo kwenda huspitali kwasababu tulihisi kama angekuwa bado anauzima, lakini ilichukuwa kama muda wa masaa matatu nakuona mwili ikitole na police ukiwa umefunikwa nakutoweka nao kwaharaka kwenda kuhifadhiwa hospital.
Hii ndiyo taarifa ya private intelligence agent(me)

Poleni wote mlioguswa na msiba huo.

Ni taarifa ya kusikitisha,
Kwa siku za hivi karibuni kumekuwa na wimbi la mauaji kwa kutumia visu,unaona mtu ameejichokea maisha anakwenda shule ya chekechea kuua watoto,inatisha mno. Mbali na wivu wa kimapenzi wachina hawajatulia kabisa kiakili.

Jambo jingine la kushangaza ni kuwa hata ikitokea ajali,hawa wenzetu hawako sharp kusaidia majeruhi,watawaacha hapo mpaka polisi waje,na hata polisi wakija watafanya taratibu zao za kipolisi halafu ndo wanawapeleka hospitali.Kama ni maiti zitakaa hapo bila kufunikwa hata kama ni masaa kadhaa,hali hii inashangaza sana,nilisha wahi shuhudia mtu amegongwa anamaumivu lakini watu wanamuangalia tu,eti wanasubiri polisi.Inaudhi.
 
alisubiri aje kukamatwa na alikamatwa, akipelekwa huku akilia, sijui kilichoendelea tena. lakini nahisi, atafikishwa kunakoshahili na hatimaye kunyongwa. mwiho wa kuwasilisha
Poleni/inasikitisha sana. Kumbe ni kweli huko China wananyongwa papo kwa papo? Nasikia hata dreva akigonga na kuua kwa bahati mbaya?
 
Back
Top Bottom