Kasimba G
JF-Expert Member
- Jan 19, 2011
- 3,428
- 2,609
Kwa nchi kama Marekani, huwa hawaruhusu mwanadiplomasia kuwa Rais. Huwa wanafanya hivyo kwa maksudi maalum kuwa, mwanadiplomasia hawezi kuwa na maamuzi magumu,hoja zake huwa zinapunguzwa ukali, majibu ya mwanadiplomasia huwa siyo makali/magumu hata maamuzi yake pia ni hivyohivyo.
Kwa mwanadiplomasia hawezi kusema nduguyangu hujapendeza atasema ingekuwa vizuri kama ungevaa au ungejitengeneza vingine, huwa, kwa mtu mzito hawezi kuelewa ujumbe wa kidiplomasia. Watendaji wengi ni wazito na ujumbe wa kidiplomasia hawawezi kuuelewa, mfano, posho za wabunge, Mwanadiplomasia mheshimiwa Rais alitoa changamoto kuwa walitafakali! Watendaji wakaona hapa ulaji!!! Ni kwamba huwa hawawezi kuelewa ujumbe wa kidiplomasia.
Watanzania na waafrika wengi huwa wanapochagua kiongozi hawazingatii historia au kazi alizowahi kufanya mtu anaye omba kuchaguliwa kuwa kiongozi ,ambapo, ni kosa kubwa saana. Rais wa nchi huwa ni amirijeshi mkuu, Huwa hatakiwi awe mwanadiplomasia kama wamarekani wanavyofanya, kwa kuwa mwanadiplomasia maamuzi yake ya kidiplomasia hayako moja kwa moja, maamuzi huwa yanajifichaficha, ajenda haiko wazi!
Kwa Mh. Dr. Kikwete kweli anadhihirisha uanadiplomasia wake kwa maamuzi yake ambayo huwa yanazingatia pande mbili, yaani hayataki kuumiza upande wowote, mkosa/mtuhumiwa na mwenyehaki, mfano, kesi za EPA n.k. Hapo diplomasia ilizingatiwa!
Je kwa vigezo hivyo Watanzania walifanya kosa kumchagua amiri jeshi mwanadiplomasia? na je wanatambua kosa walilifanya ili wasije kurudia teana na ikiwezekana wafanye kama wamarekani au iwemo katika katiba kabisa kuwa mwanadiplomasia asiwe Rais wa nchi kamwe?
Nawasilisha.
Kwa mwanadiplomasia hawezi kusema nduguyangu hujapendeza atasema ingekuwa vizuri kama ungevaa au ungejitengeneza vingine, huwa, kwa mtu mzito hawezi kuelewa ujumbe wa kidiplomasia. Watendaji wengi ni wazito na ujumbe wa kidiplomasia hawawezi kuuelewa, mfano, posho za wabunge, Mwanadiplomasia mheshimiwa Rais alitoa changamoto kuwa walitafakali! Watendaji wakaona hapa ulaji!!! Ni kwamba huwa hawawezi kuelewa ujumbe wa kidiplomasia.
Watanzania na waafrika wengi huwa wanapochagua kiongozi hawazingatii historia au kazi alizowahi kufanya mtu anaye omba kuchaguliwa kuwa kiongozi ,ambapo, ni kosa kubwa saana. Rais wa nchi huwa ni amirijeshi mkuu, Huwa hatakiwi awe mwanadiplomasia kama wamarekani wanavyofanya, kwa kuwa mwanadiplomasia maamuzi yake ya kidiplomasia hayako moja kwa moja, maamuzi huwa yanajifichaficha, ajenda haiko wazi!
Kwa Mh. Dr. Kikwete kweli anadhihirisha uanadiplomasia wake kwa maamuzi yake ambayo huwa yanazingatia pande mbili, yaani hayataki kuumiza upande wowote, mkosa/mtuhumiwa na mwenyehaki, mfano, kesi za EPA n.k. Hapo diplomasia ilizingatiwa!
Je kwa vigezo hivyo Watanzania walifanya kosa kumchagua amiri jeshi mwanadiplomasia? na je wanatambua kosa walilifanya ili wasije kurudia teana na ikiwezekana wafanye kama wamarekani au iwemo katika katiba kabisa kuwa mwanadiplomasia asiwe Rais wa nchi kamwe?
Nawasilisha.