Mwalionaje hili la kupongeza hadharani Polisi walioua?

Polisi wa tanzania wana leseni ya kuua.
Hata usipokuwa jambazi wanakuunganishia tu kuwa ulikuwa jambazi na wamekufukuza toka posta hadi mbezi kwa msuguri huku mkirushiana risasi,
wakati ukweli ni kuwa wewe ulikuwa umetoka kibaruani na polisi wamekuvizia ili wamwage damu yako.
Mwaka jana miezi karibuni na mwishoni, mfanya biashara maarufu tundduma aliuawa na polisi kwa kusingiziwa kuwa ni jambazi.
Baada ya kifo chake wananchi wa tunduma walifanya sana fujo hadi kikosi maalum kutoka mbeya mjini kikatumwa tunduma.
Baada ya mazishi hamna hatua yoyote polisi waliyoichukua dhidi ya wauaji na huo ukawa ni mwisho wa mchezo.

Police need to be extra careful katika hili, still polisi wa Tanzania siwaamini intelijinsia yao.

Hawa jamaa nitawaamini tu wakifumua fumua mifumo yao ya zamani na kuongeza nguvu kwenye upelelezi wa kisasa.

Ok, how do we know those guys were robbery? if were robbery, si ni kazi yao wanalipwa mshahara , sherehe ya nini????

manesi wote nao wakichoma sindano wafanya sherehe!
 
Kwa hili sina cha kuongeza ila cha msingi tu ht kama mtandao upo wananchi hatutakiwi kuwaonyesha km unauogopa tunatakiwa kuwaonyesha kwamba ht jup mtandao wao pia inawezekana kuuangamiza km wananchi watashirikiana kwani ndugu kitu gani mshahara wa dhambi ni mauti.je kama polisi wangeuwawa kazini ht ndugu wa polisi wangesikitika tn sana.so hata km mtandao upo yakitimia yametimia.hata nyie vibaka subirini siku yenu stupid
 
Kiranga, jee jambazi anajua hiyo rule of law wakati anapokushambulia na machine gun? Au wanapokuja kwako as a group na kukushambulia kwa mapanga?
 
Brother Kova naona kitambi tu kinazidi kuchomoza..

Nway, hakuna ubaya wa kuua mtu aliye na mitutu. Ni wazi jamii inatakiwa ilindwe kwanza kabla ya kujua vitu vingine kama kudhihirisha hao watu ni majambazi au la.
 
watoa maoni wengi nafikiri mnaishi nje ya Tanzania/afrika. Polisi wa kikosi maalumu cha kupambana na majambazi kinajulikana kwa hiyo pamoja na kusema ni makosa kuwaonyesha hadharani wale vijana, mimi sioni kama ni kosa kwa sababu wao hawafanyi upelelezi ila wanaitwa kukiwa tayari mambo yameiva kwa hiyo wanatumia utaalam tu.
 
Tunachopaswa kufahamu ni kwamba mlinda usalama yeyote anayebeba silaha na kusimama ama kutembea nayo, awe aliwahi kuua jambazi au raia mwema ama hajawahi, mbele ya Jambazi ni Adui! Jambazi anauwezo wa kulipa kisasi dhidi ya mlinda usalama yeyote yule kwa kuuawa kwa mwenzake. Kuonekana kwa hawa askari wetu haina maana ya kuwafanya maadui mbele ya majambazi ama familia zao zinazonufaika zikijua zinachopokea ni haramu, tangia hapo ni maadui tu.
 
Hili bni tatizo la watendaji wetu, wanadhani publicity ndiyo njia ya kuwafanya waonekane wanachapa kazi
 
KatuPilisi.jpg
 
Mimi sina tatizo nalo kama walioua kweli ni majambazi maana wanaweza kuuwa raia wema kabisa na kusingizia kwamba waliouwawa ni Majambazi na hili limeshatokea.
 
Zamani wakati nchi ilikuwa nchi kulikuwa na watu wanaitwa coroners kazi yao ilikuwa kuchunguza vifo kama hivyo. Sasa hivi hicho cheo hakipo na polisi wanafanya wanavyotaka kama ni jambazi si jambazi sio juu yao.

Kuna haja ya kurudisha utaratibu ule wa zamani (coroners), hata kama walikuwa majambazi kweli, walitakiwa kukamatwa sio kuuwawa, kwa nini kila siku majambazi wauawe badala ya kukamatwa?????? Jamani huu sio upungufu wa utendaji kwenye jeshi letu la polisi.

ARE YOU FOR REAL????
Unaweza kweli kumkamata mtu anayekurushia risasi,tena akiwa na silaha za kivita?Get serious!!!!When it comes to someone using silaha kwenye wizi,let the police do their work!Sipingani na wazo lako la Coroners BUT we have Medical Examiners ambao wame-replace kazi za Coroners.
 
Bila wasiwasi nathubutu kusema mpishi wa haya yooote ya kuja kwenye TV na media kwa ujumla ni kazi ya Kova.Huyu mkuu ndio amekuwa kama msemaji wa polisi kila siku hakauki kwenye media akijaribu kunua trust yetu au kwa kupenda umaarufu wake binafsi na matokeo yake anapitiliza sasa.
Kama suala ni kuwapongeza vijana wake basi kuna namna nyingi za kuwapongeza lakini hadi kuwaleta kwenye media halikuwa na ulazima au umuhimu wowote,labda wangeliandika kwa ufupi tu kwenye tovuti yao mahali ambako pia halijaandikwa.
 
Luninga jana usiku na magazeti ya leo yametoa picha za Polisi walioua majambazi pale magomeni majuzi wakipongezwa hadharani.
Suala zima la kupongeza hao Polisi sio baya lakini nahofia pale jambo hilo linapofanyika hadharani tena kwa sherehe. Tujue kuwa jambo la kuua binadamu sio jema hata kama anayeuawa ni jambazi. Nazungumzia lile tendo la kuua binadamu. Sio suala la kutambia. Kama jeshi la Polisi limeua majambazi, basi, walioua wanatakiwa kutojulikana kabisa. Kama ni kupongezwa, ingetangazwa tu kuwa wamepongezwa lakini bila kujulikana kwa wananchi ni nani aliyepongezwa.
Tukumbuke kuwa hao waliouawa wana familia zao ambazo zinaweza kulipiza kisasi au kundi lile la majambazi linaweza kuwa na mtandao mkubwa zaidi ya wale waliouawa hivyo likalipiza kisasi baada ya kuwatambua wale waliohusika na mauaji ya wenzao.
Kwa wenzetu huwa naona Polisi wakiwa wamevaa "ninja" ili wasitambulike kirahisi.
Kwa wanajeshi (JWTZ), sikuwahi kusikia mwanajeshi akitamba kuwa wakati wa vita aliua watu kadhaa. Ndio maadaili yao. Kuua sio kuzuri hata kama ni lazima kufanya hivyo.
Tusiwaonyeshe vijana wetu hadharani pale wanapokuwa wametumia ujasiri wao kulinda usalama wa raia. Ndugu zao, majirani, Polisi wenzao, hata wakienda baa sasa wanajulikana "yule aliua jambazi".
Unachojadili ni kizuri, lakini kama hatujui maudhui ya mapolisi kuonyeshana hadharani sio sawa kuwararua.

Kweli ipo hatari hata kati yao mapolisi wenyewe, maana kuna kutafuta umaarufu na ipo siku wanaweza kulengeana silaha wenyewe. Si unakumbuka wanavyouana hata kwa kugombania wanaake tu? kumbuka pale Ukonga miaka michache iliyopita ma FFU walipouana, kisa ati dem wake kachukuliwa na polisi mwenzie, au demu kamgomea kumpa alichozoea kupata kwa kuwa kapata mwenye rank kubwa zaidi.

Majambazi yakiona watu wanapongezana kwa kuwaua huenda nao wakaanza kustaafu, maana watajua uhai wao hauna thamani tena. Mbona wao huua? Polisi sio wakati wote huua, isipokuwa kama wanapambana na wenye silaha. Usisahau majambazi wengi wamepitia military training, wanazichambua vizuri silaha na wanaamini imani ya zamani kwamba polisi kazi ake ni kuvunja miguu na sio kuua. Polisi wa kikosi maalum training zao karibu sawa na JWTZ kwa maana ya kupambana na adui. Wanalenga vyote, ama kifua kushoto au mguu au vyote. Hata watoto wakijua kwamba jambazi hana thamani wataogopa kujiandikisha profession ya ujambazi, watajua hailipi.

Majambazi yakiingia kwako utamaliza sala zote wala hayajali kitu. Kumbuka mtu maarufu kwa jina la Jombi pale Mbeya aliyekuwa anatamba na kundi lake enzi za Mkapa ikamzima. Sasa amekuwa mtoto mpole anahubiri vijana wasipende ujambazi maana una mwisho mbaya. Yeye hakuuwawa, ni kuswekwa gerezani kwa amri ya Rais Mkapa, na hiyo ni kwa sababu Jombi et al walimvamia binti mdenish na kumfanya vibaya watu karibia 10, akaona bora kufa akajifia Nairobi. Kama umewahi kufanyiwa kitu kibaya na kibaka yeyote hutakuwa na chembe ya huruma kwa kibaka anayechomwa moto. Tena utawaonyesha na watoto wako waone ilivyo vibaya kuwa kibaka.

Leka
 
Mimi sina tatizo nalo kama walioua kweli ni majambazi maana wanaweza kuuwa raia wema kabisa na kusingizia kwamba waliouwawa ni Majambazi na hili limeshatokea.

Kila siku inakuwa hivyo na hapo ndipo unapokuja umuhimu wa kuwa na inquest au kitu kama hiki ili kama ikionekana vinginevyo basi polisi wanashitakiwa kwa mauaji hapa badala ya kufanya inquest eti tunapongezana na watu wanatoa hela kupongeza.

Tunakwenda wapi na tunafanya nini???????

Ukiwapa polisi wigo mkubwa wa kutumia silaha hujui kesho au keshokutwa target itakuwa nani, wanaweza kuwa politicians na mkiuliza mtaambiwa oh tulikuwa tunajilinda things like that.

Ndio maana kuna mipaka ya kila kitu, tuamke jamani huu usingizi wa pono utaisha lini.
 
ARE YOU FOR REAL????
Unaweza kweli kumkamata mtu anayekurushia risasi,tena akiwa na silaha za kivita?Get serious!!!!When it comes to someone using silaha kwenye wizi,let the police do their work!Sipingani na wazo lako la Coroners BUT we have Medical Examiners ambao wame-replace kazi za Coroners.

Sio lazima kukamata, polisi wazuri wanawadisable majambazi sio kuua kama wangejua tactics na wangekuwa trained hiyo ni kazi ndogo sana.

What do you mean silaha ya kivita? hii ni lugha ya polisi kujustify kuuwa wananchi, hata kama ni jambazi polisi hana mamlaka ya kuuwa mtu.

Hii ya Medical examiners can you appraise me ni lini coroners walikuwa replaced????? The Inquests Act is still law Chapter 24 of the laws na kazi za Coroner chini ya sheria hiyo ni:

4. Functions of Coroners' Courts
(1) The function of a Coroner's Court shall be to inquire into the
death of any person who–
(a) is reasonably suspected to have died violently or of
unnatural causes;

(b) dies a sudden death the cause of which is unknown;
(c) dies while in official custody, or in consequence of the
execution of a sentence passed on him;
(d) dies or is found dead in such place and in such circumstances
as to require an inquest in pursuance of the provisions of any
written law.
 
Back
Top Bottom